Losambo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 2,611
- 867
Tokea Mh. Lowasa ajiunge na Chadema na kupitishwa kuwa mgombea wa urais, ndiye mgombea anayekumbana na VIKWAZO VIKUBWA na pia ndiyo mgombea pekee ambaye ana MIUJIZA MINGI.
VIKWAZO.
1. Kashfa za Ufisadi. Ni takribani miaka nane tokea aujiuzuru uwaziri mkuu lakini leo hii ndiyo mtu pekee anayeonekana kama fisadi wakati mafisadi wapo wengi tu huko alipotoka. Hao wote hawaonekani lakini yeye tu ndiyo anaandamwa!! Rejea sakata la DR. Slaa, Prof. Lipumba wote walionyesha kutoridhishwa na ujio wa Lowasa kwa sababu ni fisadi!
2. Afya. Ni wazi afya ya Mh. Lowasa ni tofauti na pindi alipokuwa anajiuzuru. Hilo limetumiwa kumkashifu sana na watesi wake kiasi cha kumdhalilisha majukwani kuwa hawezi hata kupenga kamasi!! Kwangu mimi ni dhihaka ya hali ya juu kwa mtu ambaye bado hujafa!
3. Mfumo. Lowasa anapambana na mfumo mzima wa serikali ambayo ni kama wamejiapiza hata iweje hawezi kupewa nchi!! Mfumo huu ni ule wa wahafidhina wavaa suti kushuka chini!!!
4. Propaganda. Ni wazi kauli zake zinachukuliwa kipekee, kama ya hivi karibuni ya kusema aombewe na Waluthelani na nyinginezo nyingi!
5. RUSHWA. Hii ni miongoni mwa tuhuma kubwa alihusishwa kukatwa na kamati ya maadili eti alikuwa anahonga watu wafanye maagizo!!
MAAJABU YAKE.
1. KUZIDI KUKUBALIKA. Kadri muda unavyozidi kwenda ndivyo nyota ya Mh. Lowasa inavyozidi kung'aa na kuwashangaza wapinzani wake. Taarifa mpaka zinawashangaza inakuwaje mikutano yake inajaza watu wengi tena wenye kuonyesha matumaini makubwa tofauti na CCM ambao huonekana wamechoka kila wanapoambiwa Magufuli ndiyo muiba wa matatizo yao???? Rejea mapokezi na nyomi katika mikutano kisha baada ya mkutano watu kumfuata mpaka alipofikia!!! Mf. Dodoma, Kigoma, Iringa n.k
2. UNABII KUZIDI KUTIRIRIKA! Baadhi ya viongozi maarufu wa dini na ambao wanakubalika katika jamii kutoa maono waziwazi kuwa Mh. Lowasa ndiye rais ajaye! Mfano, Mch. Mwingira, Kakobe na hata Marehemu Sheikh Yahya! Haya mambo katika ulimwengu wa kiroho si ya kupuuza hata kidogo. Kumbuka 2005 na 2010 maono kama haya yalishawahi kutolewa na ikawa hivyo.
3. KUSHINDWA KWA PROPAGANDA. Propaganda hizi kila zinapobuniwa na kutekelezwa huleta mrejesho hasi kwa Lowasa! Rejea sakata la Dr. Slaa kumshambulia Mh. Lowasa kama fisadi papa!! Ni wazi tuhuma zake zimemrudia mwenyewe kwa kuonekana na mtu mwenye wivu uliopitiza, anayetawaliwa na mke wake, mbinafsi n.k Pia CCM kuonekana kumnunua na kuonekana ni muendelezo wa siasa za maji taka!!!
Hata Hamprey Polepole pamoja na jitihada zake za kumchafua bado watanzania wamempuuza na kumuona kama vuvuzela la CCM! Ni kama hana madhara!
4. MFUMO. Kwa kuwa Lowasa anaonekana kutaka kushindana na mfumo uliolea, ilitegemewa mfumo huo umsaliti kwa kutopata habari nyeti ya kinachoendela jikoni. Tofauti na hiyo, amekuwa akipata habari muhimu sana ambazo zinapangwa na kumsaidia kujipanga n.k Hali kadhalika naye katika hilo hayupo salama sana kutokana na kuwa na wavaa suti wengi walijivisha ngozi ya kondoo. Katika hili ni kama piga nikupige!
Huo ndiyo miujiza wa Mh. Lowasa licha ya vikwazo vyote anavyokumbana navyo!
MWISHO SASA JIULIZE KWA NINI?
Jibu ni jepesi sana, ni kwa sababu CCM imechokwa kutokana na;
1. Kujisahau kama watalawa kwa muda mrefu.
2. Chama kuendeshwa kama asasi ya mtu binafsi.
3. Umaskini ambao watu wanaamini umesbabishwa na CCM yenyewe n.k
Nawasilisha.
VIKWAZO.
1. Kashfa za Ufisadi. Ni takribani miaka nane tokea aujiuzuru uwaziri mkuu lakini leo hii ndiyo mtu pekee anayeonekana kama fisadi wakati mafisadi wapo wengi tu huko alipotoka. Hao wote hawaonekani lakini yeye tu ndiyo anaandamwa!! Rejea sakata la DR. Slaa, Prof. Lipumba wote walionyesha kutoridhishwa na ujio wa Lowasa kwa sababu ni fisadi!
2. Afya. Ni wazi afya ya Mh. Lowasa ni tofauti na pindi alipokuwa anajiuzuru. Hilo limetumiwa kumkashifu sana na watesi wake kiasi cha kumdhalilisha majukwani kuwa hawezi hata kupenga kamasi!! Kwangu mimi ni dhihaka ya hali ya juu kwa mtu ambaye bado hujafa!
3. Mfumo. Lowasa anapambana na mfumo mzima wa serikali ambayo ni kama wamejiapiza hata iweje hawezi kupewa nchi!! Mfumo huu ni ule wa wahafidhina wavaa suti kushuka chini!!!
4. Propaganda. Ni wazi kauli zake zinachukuliwa kipekee, kama ya hivi karibuni ya kusema aombewe na Waluthelani na nyinginezo nyingi!
5. RUSHWA. Hii ni miongoni mwa tuhuma kubwa alihusishwa kukatwa na kamati ya maadili eti alikuwa anahonga watu wafanye maagizo!!
MAAJABU YAKE.
1. KUZIDI KUKUBALIKA. Kadri muda unavyozidi kwenda ndivyo nyota ya Mh. Lowasa inavyozidi kung'aa na kuwashangaza wapinzani wake. Taarifa mpaka zinawashangaza inakuwaje mikutano yake inajaza watu wengi tena wenye kuonyesha matumaini makubwa tofauti na CCM ambao huonekana wamechoka kila wanapoambiwa Magufuli ndiyo muiba wa matatizo yao???? Rejea mapokezi na nyomi katika mikutano kisha baada ya mkutano watu kumfuata mpaka alipofikia!!! Mf. Dodoma, Kigoma, Iringa n.k
2. UNABII KUZIDI KUTIRIRIKA! Baadhi ya viongozi maarufu wa dini na ambao wanakubalika katika jamii kutoa maono waziwazi kuwa Mh. Lowasa ndiye rais ajaye! Mfano, Mch. Mwingira, Kakobe na hata Marehemu Sheikh Yahya! Haya mambo katika ulimwengu wa kiroho si ya kupuuza hata kidogo. Kumbuka 2005 na 2010 maono kama haya yalishawahi kutolewa na ikawa hivyo.
3. KUSHINDWA KWA PROPAGANDA. Propaganda hizi kila zinapobuniwa na kutekelezwa huleta mrejesho hasi kwa Lowasa! Rejea sakata la Dr. Slaa kumshambulia Mh. Lowasa kama fisadi papa!! Ni wazi tuhuma zake zimemrudia mwenyewe kwa kuonekana na mtu mwenye wivu uliopitiza, anayetawaliwa na mke wake, mbinafsi n.k Pia CCM kuonekana kumnunua na kuonekana ni muendelezo wa siasa za maji taka!!!
Hata Hamprey Polepole pamoja na jitihada zake za kumchafua bado watanzania wamempuuza na kumuona kama vuvuzela la CCM! Ni kama hana madhara!
4. MFUMO. Kwa kuwa Lowasa anaonekana kutaka kushindana na mfumo uliolea, ilitegemewa mfumo huo umsaliti kwa kutopata habari nyeti ya kinachoendela jikoni. Tofauti na hiyo, amekuwa akipata habari muhimu sana ambazo zinapangwa na kumsaidia kujipanga n.k Hali kadhalika naye katika hilo hayupo salama sana kutokana na kuwa na wavaa suti wengi walijivisha ngozi ya kondoo. Katika hili ni kama piga nikupige!
Huo ndiyo miujiza wa Mh. Lowasa licha ya vikwazo vyote anavyokumbana navyo!
MWISHO SASA JIULIZE KWA NINI?
Jibu ni jepesi sana, ni kwa sababu CCM imechokwa kutokana na;
1. Kujisahau kama watalawa kwa muda mrefu.
2. Chama kuendeshwa kama asasi ya mtu binafsi.
3. Umaskini ambao watu wanaamini umesbabishwa na CCM yenyewe n.k
Nawasilisha.