Clayton Paul
JF-Expert Member
- Aug 22, 2022
- 2,130
- 4,391
Kwanini Hatujitambui ?
Hili ni swali lilionisumbua kwa kipindi kirefu.
Nimekuwa nikikusanyishwa taarfia Toka utoto ila sikuwa naelewa nitazitumia wapi.
Kama mtoto nilipenda kuzikusanya kwa Matumizi ya baadaye maana kila kitu kwangu kilionekana kipya.
Lakini si Mimi pekee Mana mtindo huu nimeuona hata mashuleni na vyuoni.
Nimeona watu wakifunzwa kurudia kitu kile kile na Kisha wakipimwa wamekariri kwa kiasi gani.
Wakapimwa kwa Alama na zikawapa majina.
Tulijifunza kitu Fulani kinafanya kazi ila hatukufunzwa kilivumbuliwa vipi na ni kipi kilichofanya kikawa na maana Hadi kujifunza.
Tulimwagwa kwenye bwawa la Taarifa nyingi ambazo tusingeweza kubishania na kuzihoji.
Kwa Namna hii hatukuweza kujitambua kisawasawa Wala kufikiri kwaajili yetu. Kiwanda chaFikra ndani yetu kikafa kwamtindo huu. Tukafaulu kufikiri kupitia Mawazo ya wengine.
Na hii ndiyo pattern iliyosakinishwa vichwani mwetu na kupoteza uelewa wa asili.
Kwa uharibifu huu hatufikirii tukiwa tunafikiri.
Hatufikirii tukiwa katika makubaliano na mabishano zaidi ya kufungua karakana ya Hoja za waliowafunza waliotufunza.
Haya yamefanya tumeshindwa kufuatilia hata nyendo zetu huku tukijidanganya tunazifuatilia.
Yote haya ni uzao wa kushindwa kujua Matumizi sahihi ya Maarifa tuliyomwagiwa. Matokeo yake tunaanza kurudia tuliyo ambiwa kupinga hoja fulani au kujadili.
Hata humu ndani kwenye mijadala mingi huwa tunarejea majibu tuliyojazwa bila kuyapima na huu ni muendelezo wa kutojielewa.
Wafu na wafia Mfumo Wana tija katika mfumo pekee nje ya hapo ni uchafu.
Angalia watu wa dini na Wale wa Sayansi wanavyopigania kile walichoaminishwa kikapndikizwa ndani yao Kam ukweli.
Mwisho wa yote wote Hawa wako katika Safari moja ya kuusaka ukweli ambao Mara nyingi upo mbele ya macho Yao.
Shida ni rejea zilizojaa Vichwani ?
Akili zetu zimeenda wapi ?
Au tumeuzwa tukidanganywa tutauza ?
Nani akubadili kwa manufaa yako kipindi ananufaika na wewe kwa manufaa yake ?
Zipo pandikizi tulizowekwa Vichwani ambazo siku zote hutangulia mbele bila Sisi kujua Kama zipo
Pandikizi hizo ni Namna ya kufikiri zinazosafirishwa Toka kwa mtu mmoja Hadi mwingine na zinahakikisha aliyeharibiwa anaharibu wengi zaidi yake kuwa Kama Yeye bila kufahamu anaharibu
Sidhani Kama umepona haya Mana najua Mfumo huu huu umetumika kukutafuna akili zako Hadi ukajikuta Kama wenzako.
Uelewa usio was Asili ni wewe kutumia akili ya mtu katika kujadili nakuliona kila Jambo.
Uelewa usio was Asili ni jela huru ila wengi hujiona wanafikir kwa uelewa was Asili.
Punguza kujibariki na kujitukuza Kama wewe ni miongoni mean wale waliomka kumbe upo Kama Sisi.
Welcome To the System.
GENERATIONAL ATTACK
Welcome To the System.