Vijana wengi kwanini mnapenda kula ugoro?

Vijana wengi kwanini mnapenda kula ugoro?

Yap..ugoro umekuwa na soko sana baada ya kuberi kupigwa marufuku kuuzwa madukani au popote,yaani ilitangazwa kama ni mihadharati pia...umeinua maisha ya wamasai sana kwani arusha kwenye wazalishaji wakubwa na ugoro booora kuliko mahali pengine wanatengeneza kwa wingi na kusambaza mikoa mingi,huwa inapunguza hamu ya sigara kwa wavutaji "cronic"..bei ni ya chini na upatikanaji wake ni rahisi mno...nadhan wazalishaji wangetafuta namna ya kui pack vizuri na kui brand kama ilivyokuwa kwa kuberi...kama serikali inapiga vita matumizi ya tumbaku,ianze na wale wazalishaji sio watumiaji,i dont c any logic in stopping users...freedom of choice meen...!
 
Kurekebishana tabia hususan kwa vijana wa kiume wengi wao huwa nawaona nikiwa stand za magari pamoja na sehemu za makazi au wanapolinda wamasai.

Vijana wengi huwa wanapenda kula ugoro. Utakuta domo limemvimba utadhani kapigwa ngumi kumbe kajaza ugoro mdomoni.

Enzi za miaka ya nyuma staili ya kula ugoro mara nyingi ilikuwa kwa mabibi na mababu, ila miaka ya hivi karibun vijana nao sijui wanaharibikiwa nanini.

Nimeweka uzi huu ili tupate mawazo na jinsi ya kupata maoni. Ni starehe gani wanapata hawa vijana wa kiume?

Ningependa mtushirikishe kwa mawazo yenu.

Nb matusi hayaruhusiwi.

Huo ugoro wanatumia baada ya kupiga marufuku kuberi iliyokuwa inatoka India ambapo baadaye iliunganishwa katika madawa ya kulevya!
 
Yap..ugoro umekuwa na soko sana baada ya kuberi kupigwa marufuku kuuzwa madukani au popote,yaani ilitangazwa kama ni mihadharati pia...umeinua maisha ya wamasai sana kwani arusha kwenye wazalishaji wakubwa na ugoro booora kuliko mahali pengine wanatengeneza kwa wingi na kusambaza mikoa mingi,huwa inapunguza hamu ya sigara kwa wavutaji "cronic"..bei ni ya chini na upatikanaji wake ni rahisi mno...nadhan wazalishaji wangetafuta namna ya kui pack vizuri na kui brand kama ilivyokuwa kwa kuberi...kama serikali inapiga vita matumizi ya tumbaku,ianze na wale wazalishaji sio watumiaji,i dont c any logic in stopping users...freedom of choice meen...!

inasemekana kuberi zipo ila zinauzwa kwa kificho kama bange vile na bei yake ipo juu ndo maana vijana wakaamua kufakamia ugoro!
 
Wanauonea sana mmea ambao haujatengenezwa kiwandani wala kuchakachuliwa wala kuongezewa kemikali.

Sigara kwa kweli ina madhara mengi sana lakini hatuipigi vita sababu inatengenezwa kiwandani/viwandani, na mbaya zaidi nje ya pakiti wanaweka na onyo kabisa sigara ni hatari kwa afya yako. Hapa huwa nashindwa kuelewa kabisa kwanini kitu chenye athari kubwa kiendelee kuhalalishwa mimi naona bora waipige marufuku.

Ulimwengu tulionao sasa tunakula na kunywa sumu kila siku bila ya sisi kujijua matokea yake vifo vya ghafla vinakuwa vingi, magonjwa yasioeleweka ambayo enzi za ujana wangu babu mimi wala hayajakuwepo
 
Ugoro ni kilevi pasua kichwa zaidi ya vyote. Kama ndio mara ya kwanza kubwia aiseee ukizidisha lazima uny'ee na kutapika. Unastimu mbovu yenye karaha vibaya sana na huisha haraka sana.
Ila sasa kama unataka kuwa tajiri haraka sana lima tumbaku ya ugoro, sindika na uuze mwenyewe. Ndugu hapana chezea faida yake. Ekali moja ya tumbaku ya ugoro/gozo inaweza kukuzalishia mpaka zaidi ya millioni 15 wakati gharama ya kupanda hekari mpaka kuuza haifiki millioni1.
Mwaka kesho nimejipanga kuanza kulima hii kitu sitaki umasikini mie!
 
Back
Top Bottom