Maili tatu
JF-Expert Member
- Aug 8, 2020
- 830
- 1,076
Vijana wapi hao?, Kama ni wa hapa Tanzania basi hakuna hao vijana tunaowaota hapa!, tatizo halikuanza hivi karibuni kwani lilianza zamani toka awamu za mwanzo kabisa, viongozi wajamaa hapa nchini walikuwa wanaongea tu ila ndani ya mioyo yao na vikao vyao ni tofauti, vikaoni huko mathalani vya vyama ilikuwa ni mwendo wa kukubali tu hakuna kupinga, ukipinga au kuleta wazo jipya hata Kama hujatoka nje ya lengo basi jua kabisa mkitoka kikaoni wewe jiandae kwa kupewa kesi na kashkash za hapa na pale au kuondolewa chamani au kuharibiwa kabisa career yako, ujamaa ulikuwa mzuri kwenye Mambo kadhaa ila pia uliharibu kabisa na kupoteza kujiamini kwa vijana wengi na kubaki kulamba mamlaka tu, hali hii ilirithiwa kila awamu hadi kuja kushtuka loooh miaka imeenda na kuzidi kubaki na watu wa ajabu kama sasa...si umeona mwenyewe vijana hao hao wa jana ndiyo wameliingiza taifa kwenye ulimwengu wa corporatocracy.