Vijana wana jukumu la kulikomboa Taifa

Vijana wana jukumu la kulikomboa Taifa

DENG XIAOPING

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2022
Posts
2,392
Reaction score
2,599
- Habari Wanajamii wenzangu. Awali ya yote ningependa kumnukuu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Kuhusu jukumu la vijana katika Taifa.

Mwl. Nyerere anasema “Tunataka kuona katika Taifa hili vijana jeuri na wenye kujiamini , si vijana waoga ,akina ndiyo bwana mkubwa, vijana wenye ujasiri wa kuhoji na kupiga Vita mfumo wa jamii isiyo shabihiana na matakwa na matalajio ya jamii ya Kitanzania. Tunataka vijana waasi dhidi ya mfumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa”.

EkT0IrMX0AAIFi-.jpg


- Taifa lolote lenye kuhitaji maendeleo chanya ndani ya jamii pasina shaka linawahitaji vijana walio na utimamu wa mwili na akili ili kuweza kukamilisha hayo.

- Pia taifa lolote lenye kuhitaji ukombozi wa watu wake kimwili na kifikra litawahitaji zaidi vijana wabebe jukumu hilo la kukomboa watu wote kakika nyanja za kifikra na kimwili kwa kuwa vijana wamebeba matumaini mengi ya taifa kuliko watoto na wazee.ndio maana wakati wa harakati za ukombozi wa mataifa mbalimbali kutoka kwenye vifungo vya kikoloni walioshiriki zaidi harakati hizo walikuwa vijana wengi Sana na sio wazee wala watoto.

- Mada yangu imejikita kuonesha ni kiasi gani vijana walibeba matumaini ya ukombozi wa mataifa yao katika umri mdogo kabla na baada ya ukoloni na kupelekea mataifa yao kukomboka Katika namna moja au nyingine katika ngazi ya kiuchumi , kiutawala na hata kupelekea Uhuru wa mataifa yao.

1. MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE🇹🇿
- Mwalimu Kama kijana aliona anajukumu la kuleta ukombozi wa kimwili na kifikra katika Taifa letu hivo akaona ana jukumu la kupigania Uhuru wetu licha ya kuwa na umri mdogo wakati huo alipoanza harakati za kudai Uhuru Tanganyika akiwa na miaka Thelathini na moja [31], zilizo zaa matunda ya kupatikana kwa uhuru.

220px-Julius_Nyerere_cropped.jpg


2. BIBI TITI MOHAMMED🇹🇿
- Licha ya kuwa na umri mdogo wakati huo wa kudai Uhuru hilo haliku mzuia Biti Titi Mohammed yeye Kama kijana wa miaka Ishirini na nane [ 28 ] kuungana na mwalimu Nyerere na kupigania Uhuru wa Tanganyika mpaka kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika.

FDQMOJcWEAADpln.jpg


3. MARTIN LUTHER KING JR🇺🇸
- Pamoja ya kwamba alikuwa na umri wa miaka Ishirini na sita[26].umri huu hakumzui yeye kuanza na kupigania haki za watu weusi katika Taifa la marekani mpaka kuleta ukombozi haki za watu weusi marekani.

martin-luther-647_011516122755_0.jpg


4. MAO ZEDONG 🇨🇳
- Akiwa na umri wa miaka Ishirini na nane [ 28 ] Kama kijana alingua na baadhi ya vijana wa kichina na kutengeneza chama Cha kikomunisti na kuanza kupigani Uhuru wa China kutoka mdomoni mwa mabepari wa kichina na kupelekea kushinda Vita hivyo vya ukombozi na kupatikana kwa taifa huru la China.

Mao(0).jpg


5. KENNETH KAUNDA🇿🇲
- Katika umri wa miaka Ishirini na tano [25 ] hakukumzui kijana shupavu Kenneth Kaunda kushindwa kuanza harakati za kupigania Uhuru wa Zambia na kufanikisha kupatikana kwa Uhuru wa Zambia.

_110256618_kaundagetty976.jpg


6. SAMORA MACHEL🇲🇿
- Bwana Samora Machel katika umri wa miaka Ishirini na tisa [ 29 ] alianza harakati za kudai Uhuru wa wanamsumbiji licha ya kuwa kijana mdogo Ila alibeba dhamira za ukombozi wa nchi ya msumbiji.

12ca68_3b8cf7948e4f483d823dceb336ec4cf9~mv2.jpg


7. NELSON MANDELA🇿🇦
- Nelson Mandela Kama kijana katika umri wa miaka Thelathini na nne [ 34 ] alianza harakati za kupinga ubaguzi wa rangi na kupigania Uhuru wa watu weusi katika nchi ya Afrka Kusini.

image-placeholder-title.jpg


8. THOMAS SANKARA🇧🇫
- Katika umri wa miaka Thelathini na nne [ 34 ] Kama kijana hakukumzuia Thomas Sankara kufanya mapinduzi na kuiondosha utawala uliopo katika nchi ya Burkina Faso ili kuleta maisha Bora kwa wanaburkina faso.

tumblr_llvpxrLUSB1qgfbgio1_400.jpg


9. PATRICE LUMUMBA🇨🇩
- Licha ya kuwa na umri wa na umri wa miaka na Thelathini na tano [ 35 ] hali ya ukijana haikumzui Patrice Lumumba kushindwa kutetea rasilimali mali za Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo licha ya vitisho vikali alivyokutana navyo lakini aliendelea kutetea maslahi na rasilimali za wanakongo.

220px-Patrice_Lumumba,_1960(0).jpg


10. MU'AMMAR AL-QADHDHĀFĪ🇱🇾
- Gaddafi alibeba dhimira ndani ya moyo wake kuwatetea raia maskini ndani ya Libya hata alipofikia umri wa ukijana wa miaka Ishirini na Saba [ 27 ] ulikuwa Ni umri sahihi kwake kufanya mapinduzi ili kuwatetea wanalibya dhidi ya umasikini uliokuwa unawakabili.

1200px-Moamer_el_Gadafi_(cropped)(0).jpg


11. GEORGE WASHINGTON🇺🇸
- Katika umri wa ukijana kuelekea umri wa makamo miaka arobaini na tatu [43] ulikuwa ni wakati sahihi kwake kuweza kuunga mkono mapinduzi na kupigania Uhuru wa marekani kutoka kwa Muingereza.

7fe8e8268dd02acb00e3cdb643fa0bf9.jpg


12. ROBERT MUGABE🇿🇼
- Kama kijana wa miaka arobaini [ 40 ] Mugabe aliona anajukumu la kuungana na vijana wengine wakizimbabwe ili kupigania Uhuru wa nchi ya Zimbabwe kutoka kwa Muingereza.

7d737a10e2a09dccad1054e161d63d28.jpg


13. MAXIMILIEN ROBESPIERRE🇫🇷
- Katika mapinduzi ya kujikomboa kutoka katika tawala za kiimla hili liliweza kumsukuma kijana Maximilien Robespierre aliyekuwa na umri wa miaka Thelathini na moja [ 31 ] kuongoza mapambano ya kupinga utawala wa kiimla ndani ya nchi ya ufaransa.

Maximilien-Robespierre.jpg


14. PARK CHUNG-HEE🇰🇷
- Kamanda Park katika umri wake wa miaka arobaini na nne [ 44 ] hakukumzuia yeye Kama kijana na kuona ni umri sahihi kwake yeye ilikuweza kufanya mapinduzi ambayo yatabadilisha taswira nzima ya kiuchumi Korea ya kusini.
220px-Parkjunghee573.jpg


15. VLADIMIR LENIN🇷🇺
- Pamoja na vijana wengine Lenin aliweza kuongoza mapinduzi katika umri wa miaka arobaini na saba [ 47 ] ili kuweza kukomesha tawala ya kiimla ndani ya taifa la urusi na kuunda serikali ya wananchi.

1953_image2.jpeg


16. LEE KUAN YEW🇸🇬
Licha ya kuwa Kiongozi wa kwanza wa nchi huku akiwa na umri mdogo wa ukijana wa miaka Thelathini na sita [ 36 ] bwana Lee Kuan Yew hio hali haikumfanya kushindwa kuwakomboa Wanasingapore kutoka kwenye dimbwi la umasikini na kuwaletea maendeleo.

lee-kuan-yew_young.jpg


Swali: SISI KAMA VIJANA WA KITANZANIA TUNAJUKUMU GANI/TUFANYE NINI ILIKUWEZA KULETA UKOMBOZI WA PILI NDANI YA TAIFA LETU LA TANZANIA?
 
Mtego wa sasa unataka roho ya kikauzu kweli kweli. Kwasababu kwanza vijana waoga sana unaweza jitoa wao wakarudi nyuma wakakuachia msala.
 
Mtego wa sasa unataka roho ya kikauzu kweli kweli. Kwasababu kwanza vijana waoga sana unaweza jitoa wao wakarudi nyuma wakakuachia msala.
Ni nini shida kuu walionayo vijana wa Sasa Ni njaa Sana au uwoga wa kifo na mateso ndio umetawala ndani ya mioyo yao?🤔
 
"Tunataka kuona katika taifa hili, vijana jeuri na wenye kujiamini, si vijana waoga akina "ndio bwana mkubwa."
Vijana wenye wenye ujasiri wa kuhoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya kitanzania."
Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Mkuu 'Mjamaa wa Kisasa', ungekazia mada yako kwenye maneno haya, na kujikita katika Tanzania yetu hii zaidi ya kwenda kutafuta hiyo myamba mingine ya dunia, mada yako ingekuwa na uzito mkubwa sana!

Hapa hapa kwetu umewaacha akina Edward Mlinge Sokoine, akina Salim Ahmed Salim na wengine kadhaa, ambao pia wanastahili kuwa mifano kwa vijana unaowazungumzia hapa.

Vijana wetu, hasa huko ndani ya CCM wamekuwa mamluki, wapenda "kulamba sukari, na mambo mengine ya hovyo mengi. Hawa siyo vijana aliokuwa akiwahimiza Mwalimu Nyerere. Angewaona hawa leo angetamani kuwacharaza viboko, kama wale wa mlimani akina Samwel Sitta.

Hawa tulionao ndani ya CCM leo hii hawana matumaini yoyote katika taifa hili. Kizazi kizima kimepita kwa hasara tupu!

Katika miamba hao wengine wa dunia uliowa orodhesha hapo, sielewi umetumia 'criteria' gani; lakini ukiwaacha miamba kama akina Ho ch Minh, akina Fidel Castro na wengine wengi, inaonyesha kuwa hukutumia muda kutafakari undani juu ya uzito wa mada yako.
 
"Tunataka kuona katika taifa hili, vijana jeuri na wenye kujiamini, si vijana waoga akina "ndio bwana mkubwa."
Vijana wenye wenye ujasiri wa kuhoji na kupiga vita mifumo ya jamii isiyoshabihiana na matakwa na matarajio ya jamii ya kitanzania."
Mwl Julius Kambarage Nyerere...
Sio kwamba niliowaorodhesha ni wote la hasha hao ni baadhi tu Ila asante kwa kuniongezea wengine. Kuhusu kuonesha mchango wa vijana wote wa Tanzania waliokuwa shupavu katika ukombozi hilo ni somo pana lengine na sio Tanzania tu hata mataifa hayo yote niliyoyaorodhesha nitaanza kulichambua taifa moja baada jengine na kuongeza na mataifa mengine ya ziada ili kuonesha umuhimu wa vijana katika kuleta ukombozi wa kimwili na kifikra katika Taifa lolote hapa duniani
 
Mtego wa sasa unataka roho ya kikauzu kweli kweli. Kwasababu kwanza vijana waoga sana unaweza jitoa wao wakarudi nyuma wakakuachia msala.
vijana wa kitanzania hawajitambui hivyo wasijilinganishe na hao.vijana wa sasa wanawaza ufisadi na wanawatetea mafisadi kupora rasilimali za wanyonge.bado wako kwenye usingizi wa pona.mkitaka kuwajua someni threads zao humu ndani ndo mtajua akili za vijana wa kitanzania.wakilambishwa pipi wao hunogewa na utamu na kusahau ya nyuma.vijana wa kitz wamekuwa mzigo katika jamii hivyo mafisadi wanawatumia kama ngazi ya kufika kileleni.maisha yamewachanganya na wakakubali kuchanganywa.wamekuwa si tegemeo tene kwa taifa bali ni mzigo usiobebeka.wamekuwa makuwadi wa mabwenyenye na mabepali.
 
Elimu, Elimu, Elimu ndio kikwazo kikubwa, chama dola wameua mfumo wa elimu kwa makusudi ili status ago iendelee,ndio maana tunaanza kuona utawala wa kurithiana umeanza
 
vijana wa kitanzania hawajitambui hivyo wasijilinganishe na hao.vijana wa sasa wanawaza ufisadi na wanawatetea mafisadi kupora rasilimali za wanyonge.bado wako kwenye usingizi wa pona.mkitaka kuwajua someni threads zao humu ndani ndo mtajua akili za vijana wa kitanzania.wakilambishwa pipi wao hunogewa na utamu na kusahau ya nyuma.vijana wa kitz wamekuwa mzigo katika jamii hivyo mafisadi wanawatumia kama ngazi ya kufika kileleni.maisha yamewachanganya na wakakubali kuchanganywa.wamekuwa si tegemeo tene kwa taifa bali ni mzigo usiobebeka.wamekuwa makuwadi wa mabwenyenye na mabepali.
Mfano mwijaku,baba level,steve,machawa wote akilamba asali basi maisha burudani

Vijana wadogo wanafuga vitambi
Mtu kama huyu hawezi kukuelewa hata kidogo
 
vijana wa kitanzania hawajitambui hivyo wasijilinganishe na hao.vijana wa sasa wanawaza ufisadi na wanawatetea mafisadi kupora rasilimali za wanyonge.bado wako kwenye usingizi wa pona.mkitaka kuwajua someni threads zao humu ndani ndo mtajua akili za vijana wa kitanzania.wakilambishwa pipi wao hunogewa na utamu na kusahau ya nyuma.vijana wa kitz wamekuwa mzigo katika jamii hivyo mafisadi wanawatumia kama ngazi ya kufika kileleni.maisha yamewachanganya na wakakubali kuchanganywa.wamekuwa si tegemeo tene kwa taifa bali ni mzigo usiobebeka.wamekuwa makuwadi wa mabwenyenye na mabepali.
Kwa hiyo kifanyike nini ili kuondoa hili tatizo?
 
Ni Kama Kuna mifumo miwili ya elimu hapa nchini :-
i, Elimu ya watawala na
ii, Elimu ya watawaliwa
Na hili ndio tatizo kubwa linaloikabili hii young generation yetu, wengi wao hawana mwamko wa kubadili mwelekeo wa maisha yao na nchi kwa ujumla, ngoja tujiulize simple questions hapa,why mpaka leo nchi haina uwezo wa kuwaoa raia wake maji Safi wakati tumezungukwa na 3 huge lakes yenye fresh water?,why tunashindwa kama taifa kujilisha?,why quality ya education yetu intruding nyuma(ndio maana watawala wetu wanapeleka watoto wao kusoma nje ya nchi yetu,wakirudi moja kwa moja wanaingia kwenye system ya utawala),it's so sad
 
Na hili ndio tatizo kubwa linaloikabili hii young generation yetu, wengi wao hawana mwamko wa kubadili mwelekeo wa maisha yao na nchi kwa ujumla, ngoja tujiulize simple questions hapa,why mpaka leo nchi haina uwezo wa kuwaoa raia wake maji Safi wakati tumezungukwa na 3 huge lakes yenye fresh water?,why tunashindwa kama taifa kujilisha?,why quality ya education yetu intruding nyuma(ndio maana watawala wetu wanapeleka watoto wao kusoma nje ya nchi yetu,wakirudi moja kwa moja wanaingia kwenye system ya utawala),it's so sad
Daaah ni kweli juu ya hayo uyasemayo Ila inahitaji udhubutu wa sisi vijana ili kuleta mabadiliko katika Taifa letu
 
Back
Top Bottom