twahil
JF-Expert Member
- May 31, 2011
- 4,100
- 2,793
Ndg. Zangu nimeamua kuandika hapa ili tuone tutawasaidia vipi vijana wa K'KOO MTAA WA MZIZIMA-BONDENI.Juzi nilishangaa kuwaona baadhi ya wabunge wakilia kutokana na athari za madawa ya kulevya hapa nchini.Hakika nimejionea live bila chenga kwa kuona vijana wakitumia madawa hayo na bangi kwao ni sawa na kuvuta sigara.Kilichonisikitisha zaidi ni utumiaji wa bangi na dawa za kulevya hadharani na kila kona masaa yote utakuta vikundi mbali2 vya vijana wanavuta bangi,kibaya zaidi kuna shule iko karibu na kiwanda cha bia ina ukuta mrefu utakuta vijana wanafunzi wamejumuika na vijana wa mtaa huo vijiweni wakivuta bangi.MWEMA U WAPI,KOVA U WAPI,USALAMA WA TAIFA MU WAPI.NJOONI HUKU TUOKOE KIZAZI CHA NCHI HII.Vijana wamekuwa matahira ghafla huku.Au haka kakipande si tanzania?.kama huamini rafiki njoo upitepite huku utalia.Kabonde kote kananuka bangi huku vijana wakiwa matahira ghafla.