Wakuu.
Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu napenda kuwakumbusha vijana wa nchi hii, hasa wale wanaotoka familia masikini mijini na vijijini kuwa imewapasa kuelewa kuwa nchi hii inapelekeshwa na hawa wakoloni weusi wa CCM kwa sababu wao wana advantage moja ya kuwa na urahisi wa kuitafuna keki ya taifa.
Bahati mbaya sana sisi tuliozaliwa katika familia duni ambao kimsingi chanzo cha umaskini wa wazee wetu ni mifumo mibovu iliyoasisiwa na kuendelezwa na hawahawa ma-ccm kwa ajili ya kuhakikisha wanadumu katika utawala wa mabavu wakiteka akili za wazazi wetu kwa vizawadi vidogovidogo kama tisheti na kanga ha ahadi hewa kama milioni 50 kila kijiji.
Nawashauri tusikubali. Kwanza niwapongeze kwa kuendelea kuamka. muamko wa uchaguzi mwaka 2000, na 2015 tuuendeleze na sasa tukaze zaidi mpaka hawa wakoloni weusi watie akili. Hakuna cha Magufuli, hakuna cha nani hawa wakoloni wa CCM hawana jema na nchi hasa sisi watoto wa masikini.
Tuwakatae, tukatae hadaa zao. kama tutakubaliana kupiga kura tukawakatae kwenye sanduku la kura japo wataiba lakini ujumbe wataupata wakati wa kuhesabu hizo kura. Kama tutakubaliana hatuendi kupiga kura kishindo kiwafikie kwa kupata idadi ndogo ya waliojitokeza.
Nawakumbusha pia kuwa chama pekee mbadala cha kuondoa utawala wa hovyo wa CCM ni CHADEMA. Tushikamane na kusimama kwa ajili ya chama chetu. Vyama vingine ndo kama hivyo mnaona wenyewe wenzetu wana bei wameitwa Ikulu wanaunga juhudi wamevuta fungu akili zao wameziacha magogoni sasa wanafanya vituko.
Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu napenda kuwakumbusha vijana wa nchi hii, hasa wale wanaotoka familia masikini mijini na vijijini kuwa imewapasa kuelewa kuwa nchi hii inapelekeshwa na hawa wakoloni weusi wa CCM kwa sababu wao wana advantage moja ya kuwa na urahisi wa kuitafuna keki ya taifa.
Bahati mbaya sana sisi tuliozaliwa katika familia duni ambao kimsingi chanzo cha umaskini wa wazee wetu ni mifumo mibovu iliyoasisiwa na kuendelezwa na hawahawa ma-ccm kwa ajili ya kuhakikisha wanadumu katika utawala wa mabavu wakiteka akili za wazazi wetu kwa vizawadi vidogovidogo kama tisheti na kanga ha ahadi hewa kama milioni 50 kila kijiji.
Nawashauri tusikubali. Kwanza niwapongeze kwa kuendelea kuamka. muamko wa uchaguzi mwaka 2000, na 2015 tuuendeleze na sasa tukaze zaidi mpaka hawa wakoloni weusi watie akili. Hakuna cha Magufuli, hakuna cha nani hawa wakoloni wa CCM hawana jema na nchi hasa sisi watoto wa masikini.
Tuwakatae, tukatae hadaa zao. kama tutakubaliana kupiga kura tukawakatae kwenye sanduku la kura japo wataiba lakini ujumbe wataupata wakati wa kuhesabu hizo kura. Kama tutakubaliana hatuendi kupiga kura kishindo kiwafikie kwa kupata idadi ndogo ya waliojitokeza.
Nawakumbusha pia kuwa chama pekee mbadala cha kuondoa utawala wa hovyo wa CCM ni CHADEMA. Tushikamane na kusimama kwa ajili ya chama chetu. Vyama vingine ndo kama hivyo mnaona wenyewe wenzetu wana bei wameitwa Ikulu wanaunga juhudi wamevuta fungu akili zao wameziacha magogoni sasa wanafanya vituko.