Vijana wa ACT-Tanzania, BAVICHA na UVCCM na mawazo yao duni katika Siasa

mawazobinafsi

Member
Aug 15, 2014
44
14
UTANGULIZI
Watu tunaotaka kuwaunga mkono katika mageuzi tunaanza kuwaogopa. Inasikitisha wachumia tumbo kuwa vinara wa siasa.

MADA
Ni ukweli usiopingika kwamba, siasa kwetu ni kuhubiri chuki na propaganda za uongo baada ya kuangalia ni jinsi gani tutashindanisha sera na utekelezaji wake ulivyo ili kumkomboa mtanzania. Ni tofauti kwa nchi tulizowaiga, siasa kwako ni demokrasia hasa na honest kwa kila mtu. watu wanashindanisha sera na utekelezaji. Lazima tukili kwamba umasikini huu inaoongezeka unatokana na siasa zetu.

Siasa zimeongeza matumizi yetu kwenda kwenye utekelezaji wa vitu visiofaa badala ya maendeleo (majority welfare). Inasikitisha kuona fedha nyingi zimeelekweza kwenye KAMPENI kugharamia vitu visivyo na msingi kama (kununua kanga na tisheti kama takrima, matumizi ya chopa n.k)

Ni ukweli usipingika vijana wengi humu JF ni bora mkalime badala ya kufanya siasa kwani mmekuwa na mawazo tendegu kwa kufikili siasa ni CHUKI na kusambaza PROPAGANDA ZA UONGO. Inakera kuona maeno kama, UDINI, UKABILA, USALITI, na LUGHA ZA LAANA zikitumika.

Inasikitisha kuona vijana wa BAVICHA, ACT na UVCCM mnatumika na kushabikia upuuzi baada ya kujadili changamoto za uchumisiasa. Siasa kama zenu ndio zimeleta machafuko mbalimbali barani Africa.

TUJADILI
Hatma ya siasa zetu katika kutatua changamoto mbalimbali za demokrasia na uchumi. Kwa siasa hizi tutafika tunapopataka au tutachukiana tu?

Critical thinkers tujadili tuokoe Tanzania yetu
 
Ukweli asilimia mia moja. Njaa na ukosefu wa ajira vimewafanya hawa vijana kuwa wafuasi wa watu binafsi badala ya sera za chama. Pathetic.

Mada za kiuchumi na biashara ambazo zingewakomboa kiuchumi na kuwapatia ajira zikiwekwa mitandaoni hawachangii, wao ni Zitto, Lowassa na Dr Slaa tu. Hawaambiliki hawa vijana, lakini sio kosa lao, kama taifa hatuwalei vijana kwa misingi ya kuthamini utu na kufanya kazi kwa bidii. Tunawalea kwa misingi ya JIKOMBE UKOMBOLEWE, yaaani jipendekezeee wweeeee, mpige mzee Warioba, mtukane Lowassa, onyesha makalio yako makubwa then utapewa ukuu wa wilaya. Hata hao vijana wa hivyo vyama ndoto zao ni hizo. Hii nchi haitaondokana na umaskini kwa kutegemea hawa vijana waoga na wanaojikombakomba
 
Wanasiasa ndio chanzo cha yote haya ndio wanaowajaza ujinga hawa vijana
Utashangaa viongozi wametangaza kufukuzana tena kwa mbwembwe ,baadaye haohao tena wanageuka na kutangaza usaliti kwa waliowafukuza unategemea nini kwa vijana wasioweza kuchanganua mambo.
Kati ya aliyemfukuza mwenzake na aliyefukuzwa nani msaliti?
 
BAVICHA wamezidi kwa kweli wana siasa za ukanjanja .dunia nzima sijawahi kukutana na genge lenye matusi kama bavicha. Inasikitisha sana kwani hawa ndo next generation Ya siasa japo wamepunguza kwa sasa lakini ni dhahri wanapoteza maana Ya siasa kwani wamejaa chuki na matusi kwani mtu unapoandika comment ambayo haipo kwenye upande wao yaani lazima ujiandae ki psychologia kusoma comment zinazofuata. Umesema uvccm, ACT , na bavicha. Mi nadhani BAVICHA ndo vinara wakifuatiwa na UVCCM , ACT bado wanaonyesha ustaarabu fulani ila kwa Kuwa ndio siasa wanazozikuta nadhani nao wananolewa taratibu . Hata comment yangu hii lazima nimeshajiandaa ki psychologia kwa wanaonifuata . Ninaamini kuna kundi kubwa zuri tu katika jamii ambalo halijihusishi na siasa kwa sababu Ya siasa za hovyo hovyo za Tanzania ila nadhani njaa ndo inasababusha.
 
BAVICHA wamezidi kwa kweli wana siasa za ukanjanja .dunia nzima sijawahi kukutana na genge lenye matusi kama bavicha. Inasikitisha sana kwani hawa ndo next generation Ya siasa japo wamepunguza kwa sasa lakini ni dhahri wanapoteza maana Ya siasa kwani wamejaa chuki na matusi kwani mtu unapoandika comment ambayo haipo kwenye upande wao yaani lazima ujiandae ki psychologia kusoma comment zinazofuata. Umesema uvccm, ACT , na bavicha. Mi nadhani BAVICHA ndo vinara wakifuatiwa na UVCCM , ACT bado wanaonyesha ustaarabu fulani ila kwa Kuwa ndio siasa wanazozikuta nadhani nao wananolewa taratibu . Hata comment yangu hii lazima nimeshajiandaa ki psychologia kwa wanaonifuata . Ninaamini kuna kundi kubwa zuri tu katika jamii ambalo halijihusishi na siasa kwa sababu Ya siasa za hovyo hovyo za Tanzania ila nadhani njaa ndo inasababusha.

Kipimo chako nini kuhusu Bavicha? Unawajua Bavicha wote? Wapo wangapi? Umewahi kukutana nao wapi wakitukana? Au na wewe unaleta mambo ya social networks MTU mfano Mimi naitwa uvungu, mwingine msalani, lako si pesa, lizabon n.k unawajua wewe? Hivi mm nikiamua kujifanya CHADEMA na nikatukana Act je ni kwel mm Bavicha? Fanya utafiti wa kutosha mitandao ya kijamii iko fake sana.mtoa hoja kaeleza vizuri sana kabase kote na si tu Bavicha,uvccm,act ni kundi kubwa LA vijana wa kitanzania ambao wapi kwenye hizi social networks ni tatizo.
 
UTANGULIZI
Watu tunaotaka kuwaunga mkono katika mageuzi tunaanza kuwaogopa. Inasikitisha wachumia tumbo kuwa vinara wa siasa.

MADA
Ni ukweli usiopingika kwamba, siasa kwetu ni kuhubiri chuki na propaganda za uongo baada ya kuangalia ni jinsi gani tutashindanisha sera na utekelezaji wake ulivyo ili kumkomboa mtanzania. Ni tofauti kwa nchi tulizowaiga, siasa kwako ni demokrasia hasa na honest kwa kila mtu. watu wanashindanisha sera na utekelezaji. Lazima tukili kwamba umasikini huu inaoongezeka unatokana na siasa zetu. Siasa zimeongeza matumizi yetu kwenda kwenye utekelezaji wa vitu visiofaa badala ya maendeleo (majority welfare). Inasikitisha kuona fedha nyingi zimeelekweza kwenye KAMPENI kugharamia vitu visivyo na msingi kama (kununua kanga na tisheti kama takrima, matumizi ya chopa n.k)

Ni ukweli usipingika vijana wengi humu JF ni bora mkalime badala ya kufanya siasa kwani mmekuwa na mawazo tendegu kwa kufikili siasa ni CHUKI na kusambaza PROPAGANDA ZA UONGO. Inakera kuona maeno kama, UDINI, UKABILA, USALITI, na LUGHA ZA LAANA zikitumika. Inasikitisha kuona vijana wa BAVICHA, ACT na UVCCM mnatumika na kushabikia upuuzi baada ya kujadili changamoto za uchumisiasa. Siasa kama zenu ndio zimeleta machafuko mbalimbali barani Africa.
TUJADILI
Hatma ya siasa zetu katika kutatua changamoto mbalimbali za demokrasia na uchumi. Kwa siasa hizi tutafika tunapopataka au tutachukiana tu?
Critical thinkers tujadili tuokoe Tanzania yetu
Kama wewe ni mzee ujue kuwa kile kinachofanywa na vijana ndio kile kilichoandaliwa na wazee wao waliowatangulia.
 
Nashukuru Ulukolokwitanga nyamnini NCHAGWA JOSEPH measkron Escrowseal1 uvungu laki si pesa Slimhamim Tukundane kwa michango yenu. Lakini lazima tukubali mustakabali wa siasa zetu baadae ni mbaya. Ila cha kuzikitika watu hata hoja kama hizi ambazo zingeweka misingi ya watu kubadilika kifikra hawachangii. Lakini ningiandika matusi-siasa ningepata watukanaji wengi. Ni ukweli usiopingika hoja za fikra endelezi hazina debate hata humu jukwaani ambako tulifikili ni jukwaa lake. Swali bado linabaki, tufanyaje? Maana BAVICHA, UVICCM na ACT bado hawajielewi
 
Last edited by a moderator:
Ingawa ni vigumu sana kuacha hizi siasa kwa vijana wenzangu ila naweza sema tukijitambua na kuona no sisi wakuleta au kuzuia maendeleo ndo tutafanikiwa kuacha siasa chafu,
Vijana wenzangu ebu tuwe tunatafuta hata vyanzo vingine vya habari sio kuwategemea tu viongozi wasiasa tunaowapenda mengine wanayachuja kwa malengo yao. Hivyo itatupa nafasi nzuri yakujua nini hitimisho la maisha yetu ya kisiasa na kufanya maamuzi mazuri kwa mstakabari wa nchi yetu
 
BAVICHA wamezidi kwa kweli wana siasa za ukanjanja .dunia nzima sijawahi kukutana na genge lenye matusi kama bavicha. Inasikitisha sana kwani hawa ndo next generation Ya siasa japo wamepunguza kwa sasa lakini ni dhahri wanapoteza maana Ya siasa kwani wamejaa chuki na matusi kwani mtu unapoandika comment ambayo haipo kwenye upande wao yaani lazima ujiandae ki psychologia kusoma comment zinazofuata. Umesema uvccm, ACT , na bavicha. Mi nadhani BAVICHA ndo vinara wakifuatiwa na UVCCM , ACT bado wanaonyesha ustaarabu fulani ila kwa Kuwa ndio siasa wanazozikuta nadhani nao wananolewa taratibu . Hata comment yangu hii lazima nimeshajiandaa ki psychologia kwa wanaonifuata . Ninaamini kuna kundi kubwa zuri tu katika jamii ambalo halijihusishi na siasa kwa sababu Ya siasa za hovyo hovyo za Tanzania ila nadhani njaa ndo inasababusha.

Wote mtaficha ukweli ila ACT ndo chanzo cha matusi wao wanaona ndo wanajitangaza kwa kutukana watu ZZK alishafukwa jengeni chama sio kuanza kuleta lawama
 
ndg mawazo binafsi.mi binafsi nakushukuru kwa kuja na mawazo . Binadamu ameumbwa kujifunza Hadi anapomaliza muda wake duniani. Binafsi nakushukuru kwa kuliona hili. Nadhani kama nilivyosema njaa ni mojawapo Ya janga linalotukumba vijana wengi kwani wengi hatujakuwa na kipato ama uhakika wa kutoka sasa wengi kwenye siasa wanatetea usawa wao ili ama Dr.slaa, zitto, ama mkulu wasikie na kuwapendelea kupata japo uhakika wa siku na wengi wanafanya hivyo wakijua kabisa. Siamini mtu Mwenye uchumi wake na uelewa kama atakaa kwenye siasa za kupigania individual person Mithiri Ya kujitoa mhanga. Kwa hiyo mmoja mmoja kama wewe ni watu muhimu wa kusaidia kuelemishana na si kwamba haisaidii inasaidia sana kwa Mfano nilisimama kidete kupinga lugha chafu kama uharo, mavi Ya bata, nk na nakiri kabisa Kuwa nimeona yakipungua

pili jamii inayofanikiwa Mara nyingi Ina viongozi wanaoona jamii nzima kama familia tu. Hivyo huchukua jukumu la kuwasiliana nao kama familia badara Ya kuwachukulia kama watu wenye uelewa na maamuzi yao. Mfano mzuri ni hayati baba wa Taifa kwani aliwaona watanzania kama familia na alikuwa na mtindo wa kuongea nao masuala mbali mbali na moja kwa moja ukiwa na mtindo huo hautawaacha nyuma vijana kwani watajengeka na utaifa unaimarika. Mfano mwingine ni bwana kagame huwa ana style Ya kuongea na watu wake na Mara nyingine kuna mambo muhimu akigusia Hadi anapunguza sauti akimaanisha Kuwa hili ni letu wanyarwanda hii ni dawa inayowaingia wananchi wote na wanakuwa na spirit Ya kuwajenga. Amewajenga jamaa Hadi ukiwa mtaani ukadondosha taka raia tu wanakuandama bila kusubiri jiji. Sasa kwa sasa nahsi tuna bahati mbaya kupata kiongozi anaetuona kama familia badara yake mtenda maovu analindwa, ukiua unapandishwa cheo, kijana akimtukana mtu usiyempenda anazawadiwa ukuu wa wilaya. Uongozi wa juu wa kitaifa una role kubwa katika kujenga jamii .

Tatu ni level Ya civilization, bado ni Ya chini kwa afrika nzima, exposure Pia ni ndogo sana ingawa IT inasaidia kwa kiasi kupunguza hili. Kwa mwafrika mtu ambae hayuko mlengo mmoja na wewe ni adui . Hii ni process itakayochukua muda mrefu sana na nadhani taratibu japo kwa mwendo wa kinyonga tunabadirika. Mfano mtu akiamua kufuata siasa zake tofauti na za Kwako kuna haja gani Ya ku label msaliti na kuaminisha watu Kuwa ni msaliti? Let them do their own way and continue with yours.akuna haja Ya kuzushiana , kuchafuana nk Kwa hiyo mchango wa viongozi ni mkubwa kuwajenga vijana.

Basi si nadhani tuendelee kuelimishana kama hivi itasaidia tulio wengi.
 
Ingawa ni vigumu sana kuacha hizi siasa kwa vijana wenzangu ila naweza sema tukijitambua na kuona no sisi wakuleta au kuzuia maendeleo ndo tutafanikiwa kuacha siasa chafu,
Vijana wenzangu ebu tuwe tunatafuta hata vyanzo vingine vya habari sio kuwategemea tu viongozi wasiasa tunaowapenda mengine wanayachuja kwa malengo yao. Hivyo itatupa nafasi nzuri yakujua nini hitimisho la maisha yetu ya kisiasa na kufanya maamuzi mazuri kwa mstakabari wa nchi yetu
Big up ndg ila pia tupunguze siasa na tuwe na moyo wa kujadiri mambo mengi yenye tija na ukombozi wa vijana kwani post kama hizo hazipati wateja kabisa. Je ni taifa gani lenye wana siasa tupu?
 
Ukweli asilimia mia moja. Njaa na ukosefu wa ajira vimewafanya hawa vijana kuwa wafuasi wa watu binafsi badala ya sera za chama. Pathetic.

Mada za kiuchumi na biashara ambazo zingewakomboa kiuchumi na kuwapatia ajira zikiwekwa mitandaoni hawachangii, wao ni Zitto, Lowassa na Dr Slaa tu. Hawaambiliki hawa vijana, lakini sio kosa lao, kama taifa hatuwalei vijana kwa misingi ya kuthamini utu na kufanya kazi kwa bidii. Tunawalea kwa misingi ya JIKOMBE UKOMBOLEWE, yaaani jipendekezeee wweeeee, mpige mzee Warioba, mtukane Lowassa, onyesha makalio yako makubwa then utapewa ukuu wa wilaya. Hata hao vijana wa hivyo vyama ndoto zao ni hizo. Hii nchi haitaondokana na umaskini kwa kutegemea hawa vijana waoga na wanaojikombakomba

mkuu,tatizo la hawa vijana sio umasikini wa kipato unaosababisha kujikomba komba ili waweze kupata chochote.Kama hii ni kweli,unataka tuamini kuwa hawa jamaa waoshabikiwa na vijana watakuwa wana pesa nyingi sana za kuweza kutosheleza vijana wote wanaowaunga mkono.Ukisema wanajikombakomba ili waonwe nalo maana yake ni kwamba hata hata wale wenzangu na mimi tutajikomba ili tupewe nafasi gani ya uongozi ilhali elimu yetu ni ya darasa la nne c.
Mimi naamini vijana hawa wamepungukiwa na uwezo wa kuchambua mambo na kufanya maamuzi stahiki.Hapa haya mambo yanachangiwa na elimu duni,kutokuelimika kwa wale waliopata elimu,kutofanya uchambuzi wa mambo(hili ni tatizo kubwa sana kwa vijana maana wao si wasomaji wala watu wanaopenda kufanya "critical thinking"), na ni watu wanaopenda kutafuniwa kila kitu (uvivu wa kufikiri,kutafuta habari sahihi).
 
UTANGULIZI
Watu tunaotaka kuwaunga mkono katika mageuzi tunaanza kuwaogopa. Inasikitisha wachumia tumbo kuwa vinara wa siasa.

MADA
Ni ukweli usiopingika kwamba, siasa kwetu ni kuhubiri chuki na propaganda za uongo baada ya kuangalia ni jinsi gani tutashindanisha sera na utekelezaji wake ulivyo ili kumkomboa mtanzania. Ni tofauti kwa nchi tulizowaiga, siasa kwako ni demokrasia hasa na honest kwa kila mtu. watu wanashindanisha sera na utekelezaji. Lazima tukili kwamba umasikini huu inaoongezeka unatokana na siasa zetu.

Siasa zimeongeza matumizi yetu kwenda kwenye utekelezaji wa vitu visiofaa badala ya maendeleo (majority welfare). Inasikitisha kuona fedha nyingi zimeelekweza kwenye KAMPENI kugharamia vitu visivyo na msingi kama (kununua kanga na tisheti kama takrima, matumizi ya chopa n.k)

Ni ukweli usipingika vijana wengi humu JF ni bora mkalime badala ya kufanya siasa kwani mmekuwa na mawazo tendegu kwa kufikili siasa ni CHUKI na kusambaza PROPAGANDA ZA UONGO. Inakera kuona maeno kama, UDINI, UKABILA, USALITI, na LUGHA ZA LAANA zikitumika.

Inasikitisha kuona vijana wa BAVICHA, ACT na UVCCM mnatumika na kushabikia upuuzi baada ya kujadili changamoto za uchumisiasa. Siasa kama zenu ndio zimeleta machafuko mbalimbali barani Africa.

TUJADILI
Hatma ya siasa zetu katika kutatua changamoto mbalimbali za demokrasia na uchumi. Kwa siasa hizi tutafika tunapopataka au tutachukiana tu?

Critical thinkers tujadili tuokoe Tanzania yetu

wee mkali mkuu, ure great thinker halisi
 
Back
Top Bottom