Hekima94
Member
- Mar 16, 2017
- 32
- 91
Habari Wakuu,
Kwanza nitangulize shukrani zangu kwa MUNGU muweza wa yote kwa kuwa hapa muda huu na kushare na nyinyi mawazo haya.
Vijana wenzangu sisi ndio tupo wengi katika nchi zetu hususani Tanzania hivyo basi kama tukiamua kuchukua hatua yoyote ile ya kimaendeleo tunaweza kufanikiwa sana.
Lakini mabadiliko huanzia ndani kwenda nje hivyo basi kwanza tujitahidi kujijenga wenyewe kifikra ndiyo tuweze kusonga mbele.
Huwezi kujenga nyumba kama hujaandaa ardhi vizuri kwa kuchimba msingi mzuri namaanisha tuziweke akili zetu tayari kwa kufanya maendeleo.
1. Tutoe fikra za kikoloni vichwani mwetu, unachofundishwa kuhusu Afrika ni sehemu ndogo sana ya ukweli halisi kwa hiyo soma sana makala na vitabu mbalimbali kujua ukweli halisi.
2. Tutumie vizuri simu zetu haswa smartphones, tutumie muda mwingi kujifunza vitu vipya vyenye tija katika maisha yetu mfano: Unaweza ukaamua kusoma makampuni mbalimbali katika sekta yako yanayopatikana nchi ya jirani. Hapa utajifunza vingi sana.
3. LOVE au UPENDO, utajiuliza imekuwaje tena nimeliingizia hili suala. Nguzo kuu ya amani ulimwenguni kote ni Upendo yaani ukiwa na unampenda binaadamu mwenzako huwezi mtendea uovu hivyo matatizo ya dunia hii yanasababishwa na chuki, ubinafsi yaani kukosa upendo mioyoni mwetu na njia nzuri ya kukuza upendo ni kuangalia mtu au kitu bila kukihukumu mfano: Mtu amekutukana, usikubali kukasirika narudia usikubali kukasirika maana husababisha akili ikudai hukumu kutokana na hasira alizokupa na kusababisha maamuzi ya hovyo lakini ukitulia na kupotezea narudia jitahidi kupotezea utajikuta mwenye amani sanaa..
Kwanza nitangulize shukrani zangu kwa MUNGU muweza wa yote kwa kuwa hapa muda huu na kushare na nyinyi mawazo haya.
Vijana wenzangu sisi ndio tupo wengi katika nchi zetu hususani Tanzania hivyo basi kama tukiamua kuchukua hatua yoyote ile ya kimaendeleo tunaweza kufanikiwa sana.
Lakini mabadiliko huanzia ndani kwenda nje hivyo basi kwanza tujitahidi kujijenga wenyewe kifikra ndiyo tuweze kusonga mbele.
Huwezi kujenga nyumba kama hujaandaa ardhi vizuri kwa kuchimba msingi mzuri namaanisha tuziweke akili zetu tayari kwa kufanya maendeleo.
1. Tutoe fikra za kikoloni vichwani mwetu, unachofundishwa kuhusu Afrika ni sehemu ndogo sana ya ukweli halisi kwa hiyo soma sana makala na vitabu mbalimbali kujua ukweli halisi.
2. Tutumie vizuri simu zetu haswa smartphones, tutumie muda mwingi kujifunza vitu vipya vyenye tija katika maisha yetu mfano: Unaweza ukaamua kusoma makampuni mbalimbali katika sekta yako yanayopatikana nchi ya jirani. Hapa utajifunza vingi sana.
3. LOVE au UPENDO, utajiuliza imekuwaje tena nimeliingizia hili suala. Nguzo kuu ya amani ulimwenguni kote ni Upendo yaani ukiwa na unampenda binaadamu mwenzako huwezi mtendea uovu hivyo matatizo ya dunia hii yanasababishwa na chuki, ubinafsi yaani kukosa upendo mioyoni mwetu na njia nzuri ya kukuza upendo ni kuangalia mtu au kitu bila kukihukumu mfano: Mtu amekutukana, usikubali kukasirika narudia usikubali kukasirika maana husababisha akili ikudai hukumu kutokana na hasira alizokupa na kusababisha maamuzi ya hovyo lakini ukitulia na kupotezea narudia jitahidi kupotezea utajikuta mwenye amani sanaa..