Vijana na mawazo potofu juu ya CHADEMA

Vijana na mawazo potofu juu ya CHADEMA

Na kama akili yako ni matope namna hii utakaa sana.

Tumekaa na ccm sasa miaka 37 kila walichokikuta wamekiua kuanzia vya kwae vyenyewe mfano sukita,jengo la kitega uchimi la umoja wa vijana nk.

Pia wametafuna reli,atc,viwanda vyote,mashamba ya umma,vyama vya ushirika,azimio la arusha,miiko ya uongozi,nyumba za srikali wameuziana viongozi,deni la taifa kulilipa mpaka tuuuze mkoa wa kigoma nk.

Sasa kwa akili yako tunapoiona chadema ni kama mkombozi na ni kama kuanza chekechea yenye matumaini ili kuelekea primary,o level,a level na hatimaye tupate digree ya maendeleo sisi ni wajinga?

Ccm tuliiamini nayo ikatuaminisha inaweza kutupa digree tukiwa darasa la kwanza lakini miaka 37 imeisha wamekula mpaka ubao wa kuandikia wamelamba chaki na hata viboko vya kuwaadhibia watukutu(miiko ya uongozi)wamekula tuwaeleweje?

Kama ingekuwa jeshini wewe ungekela risasi maana tumeingia aruwa wewe unataka kuturudiasha mutukula.

Toka mwaka huu umeanza hii ndio comment yenye akili kuliko zote katika jukwaa la siasa. My broda, this is thinking big..,
 
....

Vema Tutafakari Baadhi ya Mambo ya Msingi 1. 1. Hivi ni kwa Kiasi Gani Democrasia Imekuwa na kukomaa ndani ya Chadema?

Huko ccm demokrasia imekuwa kiasi gani? mbona watu wanaanzisha CCJ?

...Maana Kama Zitto Kabwe Anataka Kugombea Uenyekiti,Anaitwa MUHAINI,MSALITI,Anaonekana ni kikwazo cha Maendeleo ya Chadema…. Huko ni kukosa nidhamu

Hebu TEGEMEA Sambili tuambie toka CCM imeingia madarakani imefanya nini kukusu Bandari zetu sana sana ya Dar Es Salaam, ukiachia kauli ya PK kuhusu Bandari siku moja nilikuwa Zambia nikiwa naongea na watu fulani wakahamaki sana kwanini Tz hatujaendelea pamoja na kuwa na Bandari inayounganisha nchi karibu zote za maziwa makuu? sasa hivi Msumbiji wanajenga Bandari kubwa sana Nacara na Zambia na Malawi wanajenga barabara kuunganisha hiyo Bandari unadhani hilo likikamilika Bandari ya Dar Es Salaam itafanya kazi?

Kwanini serikali inakomaa kujenga Barabara ambazo kila baada ya miaka mitano inafanya reconstruction kwa gharama kubwa badala ya kufufua reli ya kati?

Viwanda vilivyokuwepo miaka ya 80 vimeenda wapi nakumbuka enzi hizo nilikuwa Morogoro nikiwa mdogo nikifurahi sana ninapowaona wafanyakazi wakichukuliwa na mabasi kwenda Kihonda viwandani...... CCM imefanya nini?

Tuna madini na rasilimali nyingi, mazao kama pamba, kahawa na chai nk ambavyo tungeweza kuuza nje na kupata fedha ya kigeni lakini shilingi yetu inashuka kila uchao sababu eti tuna import zaidi kuliko kuimport mbona nchi kama malawi wanaimport pamba na katani kidogo sana ukizingatia eneo lao la kijiografia lakini kwacha yao ina thamani kuliko shilingi yetu?

Hapo hatujaongelea jinsi tulivyoingizwa kingi na EPA, DOWANS nk nk.

Haya maswali yangejibiwa kwa ufasaha sidhani kama wanachi wangeichukia ccm na kushabikia upinzani
 
Wapo Vijana Wachache sana Wenye Matumaini Makubwa na Chadema,Wanaamini Kabisa ya Kwamba Kama Chadema Ikichukuwa Nchi,Watanzania Tunaweza Kuishi Kama Marekani au Ulaya Magharibi, Wanaamini Hakutakuwa na Njaa wala shida,Wanaamini Ajira Zitakuwa Nyingi Kama Mchanga wa Bahari,Kutakuwa na Barabara Sitasita Juu na Chini,Wanaamini Tanzania Nzima Inaweza Ikapigwa Cement Hivyo Watanzania Kutokanyaga Vumbi wala Matope,Wanaamini Chadema ndio Chama Pekee Kinachoweza Kupambana na Ufisadi na Ukiukwaji wa Democrasia ndani ya Nchi Hii.Wanaamini Chadema Inawapenda sana Vijana Kuliko CCM na Vyama Vingine vya Upinzani. Wanaamini Kabisa Kama Chadema Ikipewa Dolla Basi Tutashuhudia Kasi Kubwa ya Maendeleo,Uboreshwaji wa Elimu,Hospitari,Miundo Mbinu ya Maji,Barabara,Reli,Viwanja vya Ndege,Makazi. Lakini Kabla ya Kuwaunga Mkono Chadema ni Vema Tutafakari Baadhi ya Mambo ya Msingi 1. 1. Hivi ni kwa Kiasi Gani Democrasia Imekuwa na kukomaa ndani ya Chadema? Maana Kama Zitto Kabwe Anataka Kugombea Uenyekiti,Anaitwa MUHAINI,MSALITI,Anaonekana ni kikwazo cha Maendeleo ya Chadema….na Baadhi ya Viongozi kama Said Arfi,Dr Kitila Mkumbo…Wanalalamika Chadema Kuchaguliwa Viongozi na Mzee Edwin Mtei. Hivi ni Maendeleo yapi Yamefanywa na Chadema,Ndani ya Chadema Kama Taasisi na Tanzania Kama Nchi yetu Sote? Maana Chadema Ina Miaka 21 sasa Tangu Kuanziswa Kwake 1993,Licha ya Ruzuku Kubwa na Misaada Lukuki Inayopata Chadema, Viongozi wa Chadema Wameshindwa Kujenga Hata Ofisi ya Makao Makuu ya Chama Chao.Sasa Watawezaje Kuiletea Tanzania Maendeleo? Chadema Haijawahi Kutoa Hata Msaada wa Madawati kwenye Shule zetu za Kata,Wao Wamekalia Kulalamika na Kushinikiza Kuing’oa CCM Madarakani. 3. 3.Hivi ni Upendo Upi Chadema IInao kwa Vijana Hata Tuiamini na Kuiunga Mkono? Maana Chadema Haina Utofauti na Wilaya Mpya(Wilaya Isio na Ofisi,Watu wachache sana…),Vijana Wanapewa Nafasi za Kugombea Ubunge ndani ya Chadema kwa Sababu Nafasi Hizo Zipo Wazi,Bado Chama Hakina Wanachama wengi, Nafasi nyingi za Kugombea Zipo wazi Kutokana na Uchanga wa Chama Chenyewe. Lakini na Uchanga Kilionao Tunashuhudia Baadhi ya Viongozi Waking’ang’ania Madaraka,Je Kama Chadema Ikikomaao na Kuwa Kama Ilivyo CCM Kutakuwa na Nafasi ya Vijana Tena??Maana Vijana Kama Zitto Kabwe Wanaotaka Kugombea Uenyekiti Wanaitwa WAHAINI, WASALITI. Acha Niiunge Mkono CCM,Maana WAMETHUBUTU. Ng’ara CCM Ng’araaa.
Nadhani unaongela ugly scenario inayomkuta Lowasa sasahivi..Lowasa hajwahi isaliti CCM wala kununuliwa na upinzani km Zitto Ila tayari hadi mwenyeketi ambaye pia ni rais ameshaingia kwa miguu yote... Sijui ndio ukanda kwa vitendo au dini pia..time would tell...Nadhani hii habari uisongelee kwani sis nzuri sana kwa CCM wanaoifanyia kazi kwa vitendo kuliko umbea wako kwa CDM
 
Wapo Vijana Wachache sana Wenye Matumaini Makubwa na Chadema,Wanaamini Kabisa ya Kwamba Kama Chadema Ikichukuwa Nchi,Watanzania Tunaweza Kuishi Kama Marekani au Ulaya Magharibi, Wanaamini Hakutakuwa na Njaa wala shida,Wanaamini Ajira Zitakuwa Nyingi Kama Mchanga wa Bahari,Kutakuwa na Barabara Sitasita Juu na Chini,Wanaamini Tanzania Nzima Inaweza Ikapigwa Cement Hivyo Watanzania Kutokanyaga Vumbi wala Matope,Wanaamini Chadema ndio Chama Pekee Kinachoweza Kupambana na Ufisadi na Ukiukwaji wa Democrasia ndani ya Nchi Hii.Wanaamini Chadema Inawapenda sana Vijana Kuliko CCM na Vyama Vingine vya Upinzani.

Wanaamini Kabisa Kama Chadema Ikipewa Dolla Basi Tutashuhudia Kasi Kubwa ya Maendeleo,Uboreshwaji wa Elimu,Hospitari,Miundo Mbinu ya Maji,Barabara,Reli,Viwanja vya Ndege,Makazi.

Lakini Kabla ya Kuwaunga Mkono Chadema ni Vema Tutafakari Baadhi ya Mambo ya Msingi 1. 1. Hivi ni kwa Kiasi Gani Democrasia Imekuwa na kukomaa ndani ya Chadema?

Maana Kama Zitto Kabwe Anataka Kugombea Uenyekiti,Anaitwa MUHAINI,MSALITI,Anaonekana ni kikwazo cha Maendeleo ya Chadema….na Baadhi ya Viongozi kama Said Arfi,Dr Kitila Mkumbo…Wanalalamika Chadema Kuchaguliwa Viongozi na Mzee Edwin Mtei.

Hivi ni Maendeleo yapi Yamefanywa na Chadema,Ndani ya Chadema Kama Taasisi na Tanzania Kama Nchi yetu Sote?

Maana Chadema Ina Miaka 21 sasa Tangu Kuanziswa Kwake 1993,Licha ya Ruzuku Kubwa na Misaada Lukuki Inayopata Chadema, Viongozi wa Chadema Wameshindwa Kujenga Hata Ofisi ya Makao Makuu ya Chama Chao.Sasa Watawezaje Kuiletea Tanzania Maendeleo?

Chadema Haijawahi Kutoa Hata Msaada wa Madawati kwenye Shule zetu za Kata,Wao Wamekalia Kulalamika na Kushinikiza Kuing’oa CCM Madarakani. 3. 3.Hivi ni Upendo Upi Chadema IInao kwa Vijana Hata Tuiamini na Kuiunga Mkono?

Maana Chadema Haina Utofauti na Wilaya Mpya(Wilaya Isio na Ofisi,Watu wachache sana…),Vijana Wanapewa Nafasi za Kugombea Ubunge ndani ya Chadema kwa Sababu Nafasi Hizo Zipo Wazi,Bado Chama Hakina Wanachama wengi, Nafasi nyingi za Kugombea Zipo wazi Kutokana na Uchanga wa Chama Chenyewe.

Lakini na Uchanga Kilionao Tunashuhudia Baadhi ya Viongozi Waking’ang’ania Madaraka,Je Kama Chadema Ikikomaao na Kuwa Kama Ilivyo CCM Kutakuwa na Nafasi ya Vijana Tena??Maana Vijana Kama Zitto Kabwe Wanaotaka Kugombea Uenyekiti Wanaitwa WAHAINI, WASALITI.

Acha Niiunge Mkono CCM,Maana WAMETHUBUTU.

Ng’ara CCM Ng’araaa.
siwezi kushangaa maana hata kupe hun'gan'gania kwenye ng'ombe hata wakichinjwa yupo tu,
 
Nilijua context kabla sijasoma coment hii. Mawazo mengi ya ma-ccm ni mgando na hawajajiandaa kuachia dola. Nitajibu hoja hizi kwa rhetorical questions kama ifuatavyo;
1. Ni demokrasia gani unayoijua ndani ya ccm? Hii ya kumdamanga Lowasa anapotangaza nia ya kuomba ridhaa ya urais kupitia ccm? Au hujawahi sikia ndani ya ccm jina la mshindi wa ubunge au diwani limekatwa na akaletwa wa mwisho? Au huwajui wana ccm wanoshikiana hadi bastola wakati wa chaguzi? N.K ama kweli Demokrasia iko ccm!!!!!!!

Miaka 21 ya CDM bado ni kichanga? Tukumbushane wakati TANU kinaleta uhuru kilikuwa na umri gani? Na viongozi wake walikuwa wa umri upi? Sasa habari ya vijana kuwa viongozi na wanachama wa CDM inatoka wapi? Unajua Sitta wa mwaka 1965 alikuwa na umri gani? Acha ulimbukeni....

Naomba pia utuweke sawa ili tuweke kumbukumbu zetu sawa; ni lini ccm walijenga ofisi licha ya kuwa na umri wa miaka 37+15? Je hizi ofisi si zile zilizojengwa na, kama siyo wewe basi ni baba,mama au babu yako wakati wa mfumo kandamizi wa chama kimoja? Hujui kuwa waliojenga ofisi hizo hawakuwa wanachama wa ccm? Baba yangu mzazi marehemu mzee Wanzagi alibeba mawe kujenga ofisi ya mkoa wa Mwanza kwa kushurutishwa na hakuwahi kuwa mwanaachama wala mpenzi wa ccm.

MWISHO: Ujenzi wa nchi hii si wa miaka 5 peke yake kwa namna ma-ccm yalivyo ibomoa. CDM kitachukua labda miaka 20 kujenga tumaini jipya la watoto wetu. WEWE mchumia tumbo usiyejali maisha na destiny ya wajukuu zako ulaaniwe.

LOOK BEYOND YOUR NOSE.......

"It is better to die with living ideas than to live with dead ideas"
 
Back
Top Bottom