Vijana CHADEMA kupigwa msasa Ujerumani

Vijana CHADEMA kupigwa msasa Ujerumani

Hakuna kinachoendelea mkuu cdu ni cristian part ya ujerumani na cmd ni roman christian church part ya tanzania ! Cdm ni zaidi uijuavyo ktk hidden ajenda ! Wenye akili waliangalie hili kwa jicho la hekima sio kukurupuka ! Sisi wa kigoma tunalijua hili zaidi na chama iliyokuwa ya utaifa mbele !
 
Hakuna kinachoendelea mkuu cdu ni cristian part ya ujerumani na cmd ni roman christian church part ya tanzania ! Cdm ni zaidi uijuavyo ktk hidden ajenda ! Wenye akili waliangalie hili kwa jicho la hekima sio kukurupuka ! Sisi wa kigoma tunalijua hili zaidi na chama iliyokuwa ya utaifa mbele !
Zitto, Sabrina na Mhonga hawalijui hili ila wewe ndio unajua! Mbona serikali ya Ujerumani inafadhali serikali yetu na huulizi? Akili kwapani
 
kwa upande wangu sioni tabu kwa chama kuwa rafiki na chama kingine hata kama hicho chama kina mlengo wa Dini,
cha muhimu hapa ni kuwa makini na hapo baadae tusije jikuta baada ya kuingia madarakani CDM wakatakiwa kulipa FADHIRA kwa chama wahisani kwa kuwapa mikataba yenye unafuu hii ndio hoja yangu

Hata ujerumani si wote ni wakristo na CDU kimeshika atamu si kwa kuwa ni chama cha kikristo ila ni kwa kuwa na misingi na sera zilizokubalika kwa jamii husika

Maoni yangu hayaingiliani na mtu yeyote yule
 
Chama tawala nchini Ujerumani, Christian Democratic Union (CDU), ambacho ni chama rafiki na Chama Cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) kimesema kitawapa nafasi za mafunzo nchini humo vijana viongozi wa Chadema, kusomea maadili na uongozi.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema hayo mwishoni mwa wiki baada ya mazungumzo ya faragha yaliyomshirikisha pia Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa na viongozi wengine wa juu, na ujumbe wa CDU, uliokuwa ukiongozwa na Rais wa zamani wa Ujerumani, Profesa Dk. Horst Kohler.

Alisema katika mazungumzo yao, Kohler alisema dhamira ya kuwapa nafasi za masomo vijana viongozi wa Chadema inalenga kuwafanya wawe viongozi wenye maadili mazuri kwa taifa lao.

"Tumekubaliana ambapo tutapata nafasi za masomo kwa vijana ambao ni viongozi wa Chadema kwenda kusomea uongozi na maadili nchini Ujerumani," alisema.

Hata hivyo, Mbowe ambaye pia ni kuingozi wa Upinzani Bungeni, hakusema lini mpango huo unatarajiwa kuanza.

Alisema walizungumzia pia suala la amani ambapo Kohler aliwaeleza viongozi hao umuhimu wa kuimarisha amani na mshikamano uliopo.

"Amani ni kitu muhimu sana na sisi tuna dhamira hiyo ya kuimarisha amani na mshikamano wa kitaifa uliopo, japo CCM wanafikiri Chadema sio chama kinachotetea amani," alisema.

Alisema mawazo hayo ni potofu na limejengeka baada ya kuona maandamano waliyokuwa wakiyafanya nchi nzima.

Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, alisema maandamano ni suala la msingi kwa wananchi kudai haki zao.



CHANZO: NIPASHE
 
We mgogo nini, Chsadema...Anyway thanx 4 the news.
 
Tusitumie hasira jamani ni uhuru wa mawazo let them talk tutarekebishana taratibu with concrete reason and evidence.
 
Mbowe(30).jpg

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe​

Chama tawala nchini Ujerumani, Christian Democratic Union (CDU), ambacho ni chama rafiki na Chama Cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) kimesema kitawapa nafasi za mafunzo nchini humo vijana viongozi wa Chadema, kusomea maadili na uongozi. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema hayo mwishoni mwa wiki baada ya mazungumzo ya faragha yaliyomshirikisha pia Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa na viongozi wengine wa juu, na ujumbe wa CDU, uliokuwa ukiongozwa na Rais wa zamani wa Ujerumani, Profesa Dk. Horst Kohler.

Alisema katika mazungumzo yao, Kohler alisema dhamira ya kuwapa nafasi za masomo vijana viongozi wa Chadema inalenga kuwafanya wawe viongozi wenye maadili mazuri kwa taifa lao. "Tumekubaliana ambapo tutapata nafasi za masomo kwa vijana ambao ni viongozi wa Chadema kwenda kusomea uongozi na maadili nchini Ujerumani," alisema.

Hata hivyo, Mbowe ambaye pia ni kuingozi wa Upinzani Bungeni, hakusema lini mpango huo unatarajiwa kuanza. Alisema walizungumzia pia suala la amani ambapo Kohler aliwaeleza viongozi hao umuhimu wa kuimarisha amani na mshikamano uliopo. "Amani ni kitu muhimu sana na sisi tuna dhamira hiyo ya kuimarisha amani na mshikamano wa kitaifa uliopo, japo CCM wanafikiri Chadema sio chama kinachotetea amani," alisema.Alisema mawazo hayo ni potofu na limejengeka baada ya kuona maandamano waliyokuwa wakiyafanya nchi nzima.
Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, alisema maandamano ni suala la msingi kwa wananchi kudai haki zao.



CHANZO: NIPASHE
 
Hivi maadili yepi hayo tunayohitaji kwenda kujifunza ujerumani? Kwa nini wasitusaidie kujenga kachuo ketu ka maadili na uongozi hapa hapa ili vijana wafundishwe maadili ya kitanzania na akina prof Safari na Dr Lwaitama?
 
Ni dalili nzuri sana ambayo dunia imeanza kuelewa ubora wa vijana wa Chadema katika ideology ya uongozi, kwani vijana rahisi kufundishika na kufuata maelekezo wangali fresh maana wakishakomaa mifupa hawawezi kuwa flexable na matokeo yake ni kufua gamba la nje tu wakati huwezi kujipinda kuruka vihunzi.
 
Hivi maadili yepi hayo tunayohitaji kwenda kujifunza ujerumani? Kwa nini wasitusaidie kujenga kachuo ketu ka maadili na uongozi hapa hapa ili vijana wafundishwe maadili ya kitanzania na akina prof Safari na Dr Lwaitama?

ecoli inauma eeeh?
 
Hivi maadili yepi hayo tunayohitaji kwenda kujifunza ujerumani? Kwa nini wasitusaidie kujenga kachuo ketu ka maadili na uongozi hapa hapa ili vijana wafundishwe maadili ya kitanzania na akina prof Safari na Dr Lwaitama?

Kwa nini ANC walipiga kambi Morogoro kilichopo chuo cha Kilimo cha Sokoine kujifunza toka TANU na CCM? Hujakumbuka vyama mbalimbali vilivyofurika Tanzania enzi za kupigania uhuru barani afrika? Utashangaa nini kinachoendelea kwa vijana wa Chadema? Ulimwengu wa leo ni wa kubadilishana uzoefu na kufunzana mbinu bora za uongozi, hatuishi isolated man, we are in the global village, You know what I'm saying!
 
hili ni jema sana kwa cdm,na ni ishara tosha kuwa cdm sasa inatanuka nje ya mipaka ya nchi,lakini zaidi sana ni kuwa hii ni ishara nyingine nzuri kuwa cdm inatambulika na harakati zake zinakubalika hata na mataifa mengine,kwanini wasiwasaidie vijana wa sisiem?WANAJUA mtoto wa nyoka ni nyoka
 
I want to join the programme, but how to join please?!
 
The CDU is Christian-based, applying the principles of Christian democracy, and emphasizes the "Christian understanding of humans and their responsibility toward God", though people adhering to any religion as well as non-religious people are allowed to be members of the CDU. The CDU's policies derive from Political Catholicism, Catholic social teaching and political Protestantism, as well as fiscal conservatism and national conservatism.
Asante ndugu malaria sugu kwa kunimezua ujinga niliokua nao.
 
[h=1]Baraza la Vijana wa CHADEMA Linakaribisha Maombi ya Kushiriki Mafunzo ya Wanasiasa Vijana Nchini Ujerumani Agosti 2012[/h]


chadema.jpg

Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) limekuwa na kawaida ya kutoa fursa za mafunzo ya makada wake ndani na nje ya Tanzania.


Dira ya BAVICHA ni kuona vijana ni nguvu ya mabadiliko ya kidemokrasia kwa maendeleo yao na ya taifa.

Kwa awamu hii BAVICHA limepanga kupeleka kada wake kwenye mafunzo ya wiki moja kwa wanasiasa vijana (Summer School) Berlin, nchini Ujerumani.



BAVICHA inawaalika vijana wa CHADEMA watakaopenda kushiriki mafunzo hayo kutuma barua ya maombi ya kushiriki, ikiambatana na wasifu unaojitosheleza (CV).



BAVICHA inahimiza vijana kutuma maombi kwa kuwa taarifa za waombaji zitahifadhiwa katika kumbukumbu (data bank) kwa ajili ya fursa nyingine zinazojitokeza.



Mwombaji pia anatakiwa ataje mawasiliano yake, namba ya kadi yake ya uanachama, tarehe ya kujiunga na chama na aeleze ushiriki wake ndani ya BAVICHA na Chama pamoja na matarajio yake ndani ya BAVICHA na CHADEMA kwa ujumla.



Maombi yatumwe kwa
Katibu Mkuu wa BAVICHA kupitia
bavicha@chadema.or.tz na nakala info@chadema.or.tz
kabla ya tarehe 10/03/2012.
 
Back
Top Bottom