Vigogo wapya wa urais 2015

Vigogo wapya wa urais 2015

Rais wetu wa 2015 ni STEVEN MASATU WASIRA kiboko wa chadema mkipenda sawa mkatae sawa ila habari ndiyo hiyo!!

:shock:
A%20S%20embarassed.gif
 
Mkuu who are you by the way kutaka tuamini hisia zako ati kati ya hao hakuna hata mmoja mwenye nia ya kugombea urahisi are you seriously au umekurupuka mkuu kutoka usingizini? Yaani Nchimbi hana nia na Urahisi -----unachekesha !!!!!! Acha uvivu wa kufikiria , fuatilia historia ya chaguzi za CCM, kisha utuambie ni nani jina lake liliteuliwa kugombea Urahisi bila kuwa member wa CC?

Mimi ni mwananchi wa kawaida sana,NCHIMBI Bado kidogo,kashkash zilizomkuta bado huyu kijana,ingawa yuko 40s,but kwa duru za Tanzania bado kidogo,sio sana.ile safu yote inampenda/imechaguliwa na mwenyekiti mkuu wa kaya,assume mkuu wa kaya akamwambia rafiki yake chukua form hii CC Utapita tu iko upande wangu hapo si mtu anapita?angalia tena ile safu ya watu 14 utaniambia.ile ni kwa ajili ya kumpitisha mtu yeyote,mkuu akimchagua Migiro agombee,CC Itamtosa?Ile CC Iko very strategic ile CC ya watu 14.au akimchagua anaempenda CC Itamtosa?anyway siasa za bongo zinaenda kinyume nyume,changanya na za kwako na mbayuwayu.
 
KWA UFUPI
NI DK SALIM,NCHIMBI,MWINYI,MIGIRO NA WASSIRA


UCHAGUZI wa wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanywa na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho Jumatatu wiki hii mjini Dodoma, ni kama unabadili mwelekeo wa siasa za ndani za chama hicho kikongwe nchini.

Tangu Rais Jakaya Kikwete aingie madarakani miaka saba iliyopita na kupewa kofia ya uenyekiti wa CCM, chama hicho kimekuwa kwenye minyukano ya siasa za visasi kiasi kwamba hakijawahi kuwa na utulivu wa kisiasa kama ilivyo sasa, miezi michache baada ya kufanyika mabadiliko kadhaa ya kiuongozi.

Uteuzi na baadaye uchaguzi wa wajumbe wa Kamati Kuu umeweka kando baadhi ya vigogo wa kisiasa hasa waliokuwa wakitajwa katika harakati za kuusaka urais katika uchaguzi wa 2015 na kuziingiza sura mpya ambazo huenda baadhi yao wanaweza kuingia katika kinyang’anyiro hicho.

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ni vigogo ambao wamekuwa wakitajwa kupiga mbio hizo, lakini waliwekwa kando katika Kamati Kuu ya sasa.

Pia majina ya mawaziri na wizara zao kwenye mabano Profesa Mark Mwandosya (Ofisi ya Rais – Kazi Maalumu), Dk John Magufuli (Ujenzi), Dk Harrison Mwakyembe (Uchukuzi) pamoja na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Katibu Mkuu wa UVCCM, Martin Shigela, pia hayakuwa sehemu ya waliopendekezwa kuingia katika CC ambacho ni chombo cha kufanya uamuzi mkubwa ndani ya CCM.

Profesa Mwandosya licha ya kuwa na matatizo ya kiafya, amekuwa akitajwa kuwa mmoja wa watu muhimu katika mustakabali wa siasa za sasa za Tanzania wakati Dk Magufuli na Dk Mwakyembe wamekuwa wakipigiwa chapuo na umma kwamba huenda wangefaa kuwania urais kutokana na kasi katika utendaji kwenye wizara wanazoziongoza.

Badala yake Kamati Kuu inawajumuisha makada ambao siyo wapya, lakini ambao wanaweza kutumika kubadili sura na mwelekeo wa siasa ndani ya CCM hasa tunapoelekea 2015, akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Dk Salim Ahmed Salim.

Hatua hiyo inaweza kuwa ni hatua ya kujaribu kujipanga kwa CCM katika kuzipa sura mpya siasa za ndani ya chama hicho. Dk Salim kama ilivyo kwa Profesa Mwandosya, alikuwa mpinzani wa Kikwete katika kinyang’anyiro cha urais wa 2005, ambaye bado anatizamwa kuwa mtu mwenye uwezo licha ya kwamba umri wake ni mkubwa.

Wengine ambao kuingia kwao katika Kamati Kuu ya CCM kunaweza kuwa na maana ya kubadili siasa za urais ni pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi na mwenzake kutoka Tanzania Visiwani ambaye alipata kuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha.

Dk Nchimbi anarejea Kamati Kuu ambako aliingia kwa mara ya kwanza akiwa na umri mdogo pale alipochaguliwa kuongoza Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na kuongoza jumuiya hiyo kwa miaka kumi mfululizo. Kwa mujibu wa kanuni za CCM, wenyeviti wa jumuiya za chama huwa ni wajumbe wa CC kwa mujibu wa nyadhifa zao. Nchimbi amekuwa mjumbe wa CC kwa miaka 10.

Hali kadhalika, Dk Mwinyi ni mmoja wa makada wa CCM ambaye amekuwa ndani ya CC kwa muda mrefu, wakati Nahodha alikuwa akiingia ndani ya kamati hiyo alipokuwa Waziri Kiongozi wa SMZ (kwa wadhifa wake).

Nahodha, Dk Mwinyi na Dk Nchimbi kwa nyakati tofauti wote wamepita katika wizara nyeti ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Dk Mwinyi wakati alipokuwa waziri, naibu wake alikuwa Dk Nchimbi ambaye baadaye alihamishiwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na sasa Mambo ya Ndani.

Dk Nchimbi alichukua nafasi ya Nahodha ambaye sasa yupo ulinzi.
Mwingine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Sera na Uratibu), Steven Wassira ambaye katika siku za karibuni ametokea kuwa moja ya nguzo kuu za CCM katika kujibu hoja mbalimbali ndani na nje ya Bunge, kusuluhisha migogoro ya kichama na kupambana na wapinzani wakuu wa chama chake, ambacho ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).


Wassira aliongoza kwa kupata kura nyingi miongoni mwa makada wa CCM waliochaguliwa kuwa wajumbe wa NEC kupitia uchaguzi wa kitaifa, lakini amekuwa akitajwa kwamba ni mmoja wa wanaokusudia kuchukua fomu za urais katika uchaguzi wa 2015.

Katika mazingira ya kawaida hii ni CC mpya ya mwisho kuundwa na Rais Kikwete akiwa Mwenyekiti wa CCM kwani ndiyo inayotazamiwa kukivusha chama hicho katika kinyang’anyiro cha 2015 ambacho yeye hatogombea kwani atakuwa amemaliza muda wake.

Umekuwa ni utaratibu wa CCM kwamba ni vigumu kumteua mgombea urais ambaye si mjumbe wa Kamati Kuu na kitendo cha baadhi ya vigogo wa kisiasa kuwekwa kando kunaweza kutafsiriwa kwamba ni kuwaweka kando katika kuwania nafasi hiyo na kuwapa fursa makada wengine ambao wanaonekana kuwa ‘watulivu’.

Licha ya kwamba Rais Kikwete ni mwenyekiti, lakini uwapo makamu wake, Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kunakipa nguvu chama hicho kuendeleza utulivu uliopo na kupitia kwao, CCM wanaweza kufanya uamuzi mgumu ambao utawashangaza wengi kwa kumteua mgombea ambaye hafikiriwi na wengi kupeperusha bendera ya chama hicho.Pia aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Asha-Rose Migiro ambaye ameteuliwa hivi karibuni katika sekretarieti mpya, naye amekuwa akitajwa kwamba huenda akachukua fomu ya kugombea urais katika chama hicho.

Kwa upande wa Dk Mohammed Shein naye huenda akachukua fomu ya kugombea urais wa Muungano baada ya kuweza kufanya kazi na upinzani bila ya mikwaruzo mikubwa huko Zanzibar. Hata hivyo, CCM kama itatupa karata yake kwa Dk Shein itabidi kufanya kazi ya ziada kumnadi.


Source: Mwananchi
hii ni sawasawa na kifufua pan africa sports club
 
Rahisi Kikwekwe ameshusha thana hadhi ya urais. Nao everibode ini dhisi kauntri wishezi tu bi a prezida!!!
 
Ni sehemu tu ya siasa lakini kutokuwa ndani ya cc hakuzuii kuteuliwa kuwania uraisssss
 
Mkuu ni kweli mtu anaweza kuteuliwa hata akiwa nje ya kamati kuu lakini ukiwa ndani ya kamati kuu unakuwa na advantage kiasi. Kwa mfano mimi naamini CCM ikiendelea kusumbuliwa na CHADEMA hadi kwenye 2015 basi CCM itaibuka na Dr. John Pombe Magufuli ambaye inaaminika akisimama tu basi uchaguzi utakuwa umeisha na CCM kushinda kwa kishindo.

Lakini pia kuingizwa kwa Dr. Salim Ahmed Salim kwenye CC sijui kuna maana gani. Mimi nilidhani baada ya masaibu yaliyomkuta mwaka 2005, Dr. Salim asingekubali tena kuingia kwenye siasa angeamua kujipumzisha akila pensheni yake. Lakini sasa amekubali kuingia NEC na kisha CC. Kuna nini hapa? Je Dr. Salim Ahmed Salim anaweza kuwa kete ya CCM akiwa kama compromising candidate? Mkuu Mchambuzi hekima zako kidogo katika suala hili tafadhali, hasa kuhusu CC na mustakabali wa CCM mwaka 2015.

Haya ni maoni yangu tu:

Kwanza - CC ya awamu ya nne haina nguvu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma – mkapa, mwinyi, nyerere kwani:

Basically, moja ya kazi zake ni kutengeneza agenda mbalimbali ambazo zinapelekwa NEC na kupitishwa kama maamuzi ya Chama, misimamo n.k. Sasa kwa zamani, wajumbe wa CC walitokana na wajumbe wa NEC ambao walikuwa ni wajumbe wazito na wenye influence na heshima ya kweli ndani ya NEC na Chama kwa ujumla kwa mujibu wa kanda, mikoa na taifa; hawa walikuwa na influence, respect, followers and loyalists wengi sana kwenye NEC, kwahiyo agenda nyingi zikipitishwa CC kupelekwa NEC, kulikuwa na almost 100% guarantee kwamba zitaungwa mkono; Nyakati hizi hali ni tofauti hasa baada ya mtandao kuchukua uongozi wa nchi 2005 kwani baada ya EL kujiuzulu 2008, ambae alikuwa ni key to ushindi wa JK 2005, na ambae amekuwa mjumbe wa NEC tangia 1982, ameondoka na loyalists, followers wengi, na wale waliobaki ni loyalists and followers wa kiti, not necessarily mwenyekiti.

Pili, ingawa in theory CC ndio chombo chenye nguvu kuliko vyote ndani ya CCM, in practice ni NEC hasa kutokana na Mwalimu kuona umuhimu wa maamuzi kufanywa na watu walio wengi zaidi ndani ya chama kama njia ya kukuza demokrasia na kupunguza misuguano kimaamuzi. Wakati wa Nyerere NEC ilikuwa na nguvu kuliko bunge la CCM na hata Katiba ya JMT (1977), na hali hii bado ipo kidogo katika nyakazi hizi. Kwahiyo focus yetu iwe zaidi katika NEC kuelekea 2015, CC is almost irrelevant katika kutupatia mgombea Urais unless wale wasiotakiwa waamue kutogombea kwa maamuzi yao wenyewe.

Tatu, ni dhahiri kwamba CCM imeshindwa kuvunja makundi, badala yake, CCM imefanikiwa kusimamisha vita hivi visiwe in public huku ikifanya nothing much kuvisimamisha in private kwani vita bado ni moto na vitazidi kushika kasi kuelekea 2015. Pia tumeshaona jinsi gani uchaguzi wa NEC ni kina nani walikuwa na nguvu kati ya makundi yote tajwa yaliyopo, na jinsi gani juhudi kubwa zilielekezwa huko compared to CC; Kuzima mapenzi ya wana CCM kwa viongozi Fulani Fulani imeshindikana, kilichobakia na kinachoendelea sasa ni kucheza tu na psychology za wana CCM lakini pia umma kwamba kiti kikikuacha kwenye cheo Fulani, basi ina maana kwamba wewe haufai, na hii ni kwa mtindo wa zidumu fikra sahihi za wenyekiti wa CCM, kwani waumini wa hizi fikra bado wapo na watasaidia kuvuruga candidacy za watu Fulani Fulani kueleka 2015. So kuelekea 2015, wapo wana CCM ambao wataamini kwamba Fulani kaachwa kwa sababu hafai na hii itafanya safari ya wahusika kuelekea 2015 kuwa na bumps kidogo. Lakini pia kama njia ya kutuma ujumbe kwamba chama kinajaribu ku-heal siasa za makundi, pia imeonekana ni busara players wote wa makundi wasiteuliwe kuingia kwenye CC, huku hoja yangu in green hapo juu ikiendelea kufanya kazi;

Nne ni suala la Magufuli na Salim; Tukianza na Salim, zote ni efforts to heal makundi, hasa kumfanya yeye na wafuasi wake waegemee zaidi mmoja, na sio upande mwingine au wasiwe wana hang hang tu kwani wakiwa wapo wapo tu, ni rahisi sana kwa wao to sympathize na upande mwingine au kuwa open kusombwa na mgombea atakayekuwa na nguvu kuelekea 2015. Will it work? That remains to be seen. Otherwise iwapo mwalimu nyerere alijaribu mara mbili na Salim na kushindwa, sioni jinsi gani uongozi wa sasa wa CCM utaweza kupitisha kugombea Urais. He first needs to sort out tatizo lake na wenye chama (CCM/ASP) upande wa Zanzibar. Kuhusu Magufuli, pamoja na potentials zake kuwa juu, tatizo ni kwamba wenye chama hawamtaki kwani wao hawaangalii utendaji wa kazi bali ni usisi na uwao. Sioni magufuli kutumika unless dakika ya mwisho analysis iwe kwamba zinahitajika kura za kanda ya Ziwa na maeneo ya Tabora ili CCM ishinde kwa urahisi 2015 dhidi ya Chadema.

Mwisho – kwa jinsi hali ilivyo sasa, mgombea yoyote ambae atakuwa anaungwa mkono na kiti, huyo ataangukia pua, mgombea mwenye nafasi ya kupitishwa na NEC May 2015 kwa kura nyingi in the top three na pia kupita uchaguzi wa Rais November 2015 ni Yule ambae atakuwa hana support ya Kiti wakati wa mchakato wa kupata mgombea. Vinginevyo CCM itashinda urais 2015 lakini tutarajie CCM kupata ushindi wa asilimia ndogo kuliko zote katika historia ya taifa – just over 50%, na ushindi wa namna hii upo wazi kwa mgombea yoyote atae simamishwa na CCM iwe ni Lowassa, Migiro, Mwakyembe, Membe, Magufuli, Sita, Mwandosya, January Makamba etc.

Again, haya ni maoni yangu tu Bwana Kimbunga, nasimama kupingwa;
 
Kwa vile ndani ya CCM hata na hao wanaotajwa hakuna hata mmoja ambaye ameonyesha dhahiri kukerwa na ufisadi na umasikini wa Tanzania zaidi ya kuwa watetezi wa Chama hata kinapokiuka misingi ya kuundwa kwake basi HAKUNA anayefaa kuwa Raisi wa nchi hii kwa siku zijazo.
 
Dr Salim walijichanganya wenyewe MAGAMBA kumpa kashfa nzito mwaka 2005 ili Handsome apite, sidhani kama yupo radhi kukubali kugombea Urais!!
 
Ushabiki pembeni: Stephen masato wassira a.k.a tyson(ccm), a.k.a gombe/sokwe(cdm) ndiyo mtu mwenye nguvu ktk hao vigogo...hakuna magufuli wala mwakyembe urais 2015, na cdm hasimami na huyu mzee, hasa dr. Slaa...kampeni 2015 ni wassira(ccm), slaa(cdm) midahalo ya kumwaga kama kenya, tena ni kama raila odinga kwa umri..sura mbaya sio ufisadi,wassira cdm haina jibu.atapeta sababu hagawi chama na umoja ndiyo ushindi...
 
ushabiki pembeni: Stephen masato wassira a.k.a tyson(ccm), a.k.a gombe/sokwe(cdm) ndiyo mtu mwenye nguvu ktk hao vigogo...hakuna magufuli wala mwakyembe urais 2015, na cdm hasimami na huyu mzee, hasa dr. Slaa...kampeni 2015 ni wassira(ccm), slaa(cdm) midahalo ya kumwaga kama kenya, tena ni kama raila odinga kwa umri..sura mbaya sio ufisadi,wassira cdm haina jibu.atapeta sababu hagawi chama na umoja ndiyo ushindi...
Mkuu Tyson ana upepo..someni rai la jana title Kwanini Wasira, Wasira CCM?
 
Rais wetu wa 2015 ni STEVEN MASATU WASIRA kiboko wa chadema mkipenda sawa mkatae sawa ila habari ndiyo hiyo!!

Yaani Sizimwa awe Rais wa nani? Nitaomba uraia Rwanda!! Nani aongozwe na Kiumbe wa Gombe na Mahale?
 
yaani sizimwa awe rais wa nani? Nitaomba uraia rwanda!! Nani aongozwe na kiumbe wa gombe na mahale?
hoja za kigovi ndio zitafanya chadema ikose mvuto 2015..kilaza: Zuia kwa hoja sasa kiumbe cha gombe ndio nini?ataletwa huyo tuone atakavyo wakimbiza rwanda..mnapigwa mkubali sio kuvuruga amani, hacheki kama fastjet..kz kz
 
hoja za kigovi ndio zitafanya chadema ikose mvuto 2015..kilaza: Zuia kwa hoja sasa kiumbe cha gombe ndio nini?ataletwa huyo tuone atakavyo wakimbiza rwanda..mnapigwa mkubali sio kuvuruga amani, hacheki kama fastjet..kz kz

political immaturity..elections is about votes, not inflammatory language..wasira shows he can win votes cdm, take note he might serve the 2015 defeat if nominated..wanaccm wanahasira na cdm kuliko wanavyofikiri lazima uchaguzi watataka mtu akawaabhibu jukwaani "Wassira"...anakuja na so far its proven chadema leaders have no answer for him..ccm wins again na huyo huyo mwarobaini wenu..
 
Pamoja na yote hayo panga pangua yeyote kutoka ccm mwaka 2015 atabaki kuwa mgomgea na wala siyo rais naomba mninukuu na mwaka huo mtajionea wenyewe: Kutakuwa na thread inayosema '' maneno ya makunda yatimia'' baada ya hapo msinitafute kwa utabiri mwingine! Sawa wangwana?
 
Urais si kuangalia sura bali ukomavu uzoefu uadilifu uzalendo na msimamo na sioni kinachomkosa wasira na sidhani tutachagua kwa ushabiki!
 
Urais si kuangalia sura bali ukomavu uzoefu uadilifu uzalendo na msimamo na sioni kinachomkosa wasira na sidhani tutachagua kwa ushabiki!

Watu watatu muhimu katika siasa za CCM kuelekea 2015 ni hawa; 1. Prof. Mark Mwandosya 2. Peter Kayanza Pinda 3. Asha Rose Migiro. Hawa ndiyo the best three watakaokwenda NEC na mmoja wao kupeperusha bendera ya CCM 2015.
 
Back
Top Bottom