Elections 2010 Vigezo vinavyotumiwa na tume kupata idadi ya viti maalum kwa kila chama

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Wana JF nisaidie kwa hili; Inasemekana idadi ya viti maalum hutolewa na NEC kwa chama cha siasi, kulingana na uwiano wa jumla ya kura za urais na wabunge walizopigiwa wagombea wa chama husika; kama hivyo ndivyo, kura za wabunge wanaochaguliwa bila kupingwa zinapatikanaje ili kuweza kukamilisha zoezi hilo.Jambo la pili, kwa mujibu wa ibara ya 66 ya katiba bunge la Tanzania linaundwa na wabunge wa aina nne; waliochaguliwa kuwakilisha majimbo, wa viti maalum, waliochaguliwa na Baraza la wawakilishi na Mwanasheria mkuu wa serikali. sasa hao wabunge wa kupita bila kupingwa wanao wakilisha majimbo bila ya ridhaa ya majimbo husika, wanatokana na kifungu kipi cha katiba? Isingelikuwa vyema angalau wakapigiwa za ndiyo? naomba mchango wenu.
 
Back
Top Bottom