Mkuu Samoche labda umeisahau hii nchi. Nchi yetu haina tabia ya kuajiri 'the best'. Labda kuwe na TISS na TAKUKURU za binafsi.
Mimi nimekuwepo kwenye 'interview panel' za baadhi ya mashirika ya Umma, nimekuwa nikionekana mnoko kwa kuwa sikuzote nimegombana nao sana. Yaani the best 3 kwenye 'interviews' huwa hawapati ajira na ndio maana wengi wanaenda sekta binafsi.
TISS, TAKUKURU, TRA, POLISI, JWTZ, BOT,TPA, TANESCO, WIZARA ZETU, IKULU, PMO, TLB e.t.c kumejaa mazezeta ambao wana vyeti tu lakini uwezo hakuna. Ndio maana ukiwa na uwezo mkubwa mfano uwe kama hao jamaa zetu watakuona 'threat' hawakuchukui ng'o.
Mashirika na Taasisi za serikali ambazo kidogo wanachukua watu wa maana ni TCRA, EWURA, UDSM, PPRA na siku hizi baada ya Utouh NAO.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.