VIDEO: Mbunge aliyempongeza Diamond Platnumz

Status
Not open for further replies.

Maboso

JF-Expert Member
Feb 18, 2013
5,164
5,761
May 13 2016 ilikuwa ni zamu ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwasilisha Bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2016/2017. Katika kipindi cha kupokea michango ya maoni kutoka kwa Wabunge, Mbunge wa Ulanga Goodluck Mlinga akaguswa na harakati za staa wa Bongo flava Diamond Platnumz

Ingekuwa amri yangu tungechonga sanamu la Diamond tukaliweka kwenye mnara wa Askari, ule mnara tumeuchoka. Ametufikisha mbali naameitangaza nchi yetu huko mbele

Serikali hatuna mpango wowote wa kuwasaidia wanamuziki, wanapenya wenyewe tunaenda kukutana nao mbele na sisi tunajifanya kuwasaidia. Yuko wapi Mr. Nice?,hatujawawekea mfumo mzuri, ninaongea haya nikiyamaanisha’

Unaweza kumcheki kwenye hii video hapa chini…


Credits to: Millard Afrael Ayo
 
Lugha tatizo, Mantiki ya mbunge huyo ni kuionyesha Serikali jinsi inavyodandia mafanikio ya wasanii baada ya kutoka.

Ametumia lugha ya picha kuelezea ubora wa Mondi juu ya sanamu mashuhuri.

Ukweli hoja ya babies amegusa pabaya
 
Nyimbo kali za msimu huu

Kwetu - Raymond

Moyo mashine - Benpol

Jike shupa - Nuh Mziwanda

Say my name - Shishi baby


Nyimbo mbovu kabisa msimu huu

Aje - King Kiba

Chura - Snura

Colours of Africa - Mafikizolo ft Diamond Plutnumz
 
Kuishi kwingi kuona mengi, atakuja kusema baba wa taifa awe samatta
 
Nyimbo kali za msimu huu

Kwetu - Raymond

Moyo mashine - Benpol

Jike shupa - Nuh Mziwanda

Say my name - Shishi baby


Nyimbo mbovu kabisa msimu huu

Aje - King Kiba

Chura - Snura

Colours of Africa - Mafikizolo ft Diamond Plutnumz
mbna kama hiyo ya shishi ilistahili kukaa kundi B pia?
 
Hata mimi na mkubali diamond lkn huyu mbunge mapenzi yake kwa diamond yamepitiliza
 
Hajitambui huyu ... hv anapataje ubunge ! mtu kama huyu l fill very sorry for him
Mkuu sio yeye tu asie jitambua hata hao waliomchagua ndio zaidi ya wasio jitambua.
Ivi unaanzia wapi kuchaguwa mtu kama huyu kileta bungeni.
Mtu asie jua hata maana ya lile sanamu analo liongelea unaanzia wp kulifaninisha lile sanamu na daimond?
Kama ameona anahoja ya kuweka kumbukumbu za daimond hii nchi ni kubwa sana na ina sehemu nyingi tu za kuweka sananamu la daimond bila kuvunja sanamu lolote lile.
Muhim ni angejenga hoja yenye mantiki tukamuelewa sio kuropokwa tu.
 
Kuna mambo kaongea zaid ya sanamu, naona mme nyofoa moja tuu

Jamaa maana yake ilikuwa nzuri tuu, wala syo tatizo
 
Huyo mbunge yupo sahihi kabisa, tena na mimi naongezea TUJENGE MASANAMU YA DIAMOND KILA MKOA TZ NZIMA.
 
Nyimbo kali za msimu huu

Kwetu - Raymond

Moyo mashine - Benpol

Jike shupa - Nuh Mziwanda

Say my name - Shishi baby


Nyimbo mbovu kabisa msimu huu

Aje - King Kiba

Chura - Snura

Colours of Africa - Mafikizolo ft Diamond Plutnumz

hapana wimbo wa chura uingie kundi A , pia wimbo wa BADO harmonize uingie kundi hilo
 
Lugha tatizo, Mantiki ya mbunge huyo ni kuionyesha Serikali jinsi inavyodandia mafanikio ya wasanii baada ya kutoka.

Ametumia lugha ya picha kuelezea ubora wa Mondi juu ya sanamu mashuhuri.

Ukweli hoja ya babies amegusa pabaya

Kwa hiyo sanamu walo iweka hawakuwa na mantiki.Kashauriane mtafute sehemu nyingine sio mtuondolee historia zetu!!
 
Mkuu sio yeye tu asie jitambua hata hao waliomchagua ndio zaidi ya wasio jitambua.
Ivi unaanzia wapi kuchaguwa mtu kama huyu kileta bungeni.
Mtu asie jua hata maana ya lile sanamu analo liongelea unaanzia wp kulifaninisha lile sanamu na daimond?
Kama ameona anahoja ya kuweka kumbukumbu za daimond hii nchi ni kubwa sana na ina sehemu nyingi tu za kuweka sananamu la daimond bila kuvunja sanamu lolote lile.
Muhim ni angejenga hoja yenye mantiki tukamuelewa sio kuropokwa tu.
Hi hi unaezakuta Goli la mikono kama mkuch.......
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom