Vicky Kamata afunga Ndoa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Likwelile

Ashura9

JF-Expert Member
Oct 21, 2012
740
485
Vicky Kamata Afunga Ndoa na Dk. Likwelile


upload_2016-3-19_22-24-1.jpeg
upload_2016-3-19_22-24-1.jpeg




Dk Servacius Likwelile.

Dar es Salaam, Geita-Tanzania. Mbunge wa Viti Maalamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Vicky Kamata amefunga ndoa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile.

Dk Likwelile amefunga ndoa hiyo baada ya mkewe wa awali kufariki dunia Mei mwaka 2014.

Kwa hatua hiyo, Dk Likwelile amemfuta machozi mbunge huyo kijana baada ya ndoa yake ya awali aliyotarajia kuifunga na Charles Pai kukwama dakika za mwisho wakati wa maandalizi yote ya msingi kukamilika.

Habari ambazo Tanzania Daima imezipata, zilieleza kwamba mbunge huyo ambaye ni msanii wa muziki wa kizazi kipya , alifunga ndoa hiyo Septemba mwaka jana katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Geita.

Habari zinaeleza kuwa wawili hao baada ya kufunga ndoa, hawakuwa na sherehe kubwa bali walikuwa na ‘pati mchapalo’ iliyofanyika nyumbani kwa Dk Likwelile na kuwashirikisha baadhi ya wana ndugu na marafiki wa pande zote mbili.

“Wamefunga ndoa bomani, hakukuwa na sherehe bali kulikuwa na hafla ndogo iliyofanyika nyumbani na wanafamilia wachache ndio walioshiriki,” alisema mtoa habari wetu ambaye alikuwa mmoja wa watu wachache walioshuhudia ndoa hiyo.

Alipotafutwa kwa njia ya simu kuthibitisha taarifa hizi, Kamata alikiri kufunga ndoa hiyo, lakini hakuwa tayari kuzungumza zaidi.

“Umepata wapi hizi taarifa? Ila ni kweli nimefunga ndoa, ninachojua ni kwamba Dokta Likwelile ni mume wangu halali, namshukuru Mungu kwa hilo,” alisema kwa kifupi Vick na kukata simu.

Mei 24 mwaka 2014, Vick Kamata alikwama kufunga ndoa na Charles Pai baada ya kubainika kuwapo kwa kasoro kwenye nyaraka za mwanaume.

Hali hiyo ilisababisha mbunge kuugua ghafla kutokana na mshituko alioupata na kulazimika kulazwa katika Hospitali ya Tabata Genaral iliyopo Segerea. Ndoa hiyo ilikuwa ifungwe katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mkombozi, Sinza jijini Dar es Salaam na tayari kadi za mialiko zilikuwa zimesambazwa kwa watu mbalimbali wakiwamo wabunge.

Kamata ni msanii wa muziki aliyetamba na kibao chake cha “ Wanawake na Maendeleo” na pia ni mtetezi wa haki za wanawake.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima (Jumamosi Machi 19, 2016)
 
Anafananaje tena huyo dada? Nlikuwa naskia story zake tangu nipo masekondary and all i heard ni kwamba alikuwa chakula ya wakubwa..:p
Gazeti la Tanzania Daima likekwisha sasa ni Udaku tu, kwa nini hiyo habari hawakuikamilisha? Kwa nini hawatuambii kwamba marehemu Msanchi Simbeye hakuwa mke wa ndoa wa Dr na ndio maana hata hiyo harusi haikupata kibali cha kanisani. Kama vicky alibwagwa siku ya harusi na Dr. Ni mjane na wote ni wakristo tena wakatoliki, kwa nini hawakufungia hiyo ndoa kanisani? Je ni kweli Dr Likwelile hana mke wa ndoa? aliyezaa nae watoto? familia inayojulikana tangu wakati alipokua chuo kikuu kabla hata hajasemekana kuwa ni mume wa yule dada wa kwenye ofisi ya idara yake pale chuo kikuu? Je hakuna shauri linalohusu ndoa ya mhusika hapa ama kwenye vyombo vya dini, ama idara zinazohusika hata hili gazeti libebe habari isiyokamilika? Au tu walitaka kutoa umbea wa maisha ya watu, tena ya siri mbele ya jamii? wanamjengea ama kumdhalilisha katibu wetu mkuu? maana huyo dada hatumshangai kwa habari za ajabu ajabu,
 
Gazeti la Tanzania Daima likekwisha sasa ni Udaku tu, kwa nini hiyo habari hawakuikamilisha? Kwa nini hawatuambii kwamba marehemu Msanchi Simbeye hakuwa mke wa ndoa wa Dr na ndio maana hata hiyo harusi haikupata kibali cha kanisani. Kama vicky alibwagwa siku ya harusi na Dr. Ni mjane na wote ni wakristo tena wakatoliki, kwa nini hawakufungia hiyo ndoa kanisani? Je ni kweli Dr Likwelile hana mke wa ndoa? aliyezaa nae watoto? familia inayojulikana tangu wakati alipokua chuo kikuu kabla hata hajasemekana kuwa ni mume wa yule dada wa kwenye ofisi ya idara yake pale chuo kikuu? Je hakuna shauri linalohusu ndoa ya mhusika hapa ama kwenye vyombo vya dini, ama idara zinazohusika hata hili gazeti libebe habari isiyokamilika? Au tu walitaka kutoa umbea wa maisha ya watu, tena ya siri mbele ya jamii? wanamjengea ama kumdhalilisha katibu wetu mkuu? maana huyo dada hatumshangai kwa habari za ajabu ajabu,
sasa bro umezungumza sawa, lakini huyo katibu wenu mkuu hakusoma hizo habari za ajabuajabu za huyo dada? kujihusisha nae ndio kusema naye anahusika na habari za ajabuajabu vilevile ndio wakakutana....
 
Gazeti la Tanzania Daima likekwisha sasa ni Udaku tu, kwa nini hiyo habari hawakuikamilisha? Kwa nini hawatuambii kwamba marehemu Msanchi Simbeye hakuwa mke wa ndoa wa Dr na ndio maana hata hiyo harusi haikupata kibali cha kanisani. Kama vicky alibwagwa siku ya harusi na Dr. Ni mjane na wote ni wakristo tena wakatoliki, kwa nini hawakufungia hiyo ndoa kanisani? Je ni kweli Dr Likwelile hana mke wa ndoa? aliyezaa nae watoto? familia inayojulikana tangu wakati alipokua chuo kikuu kabla hata hajasemekana kuwa ni mume wa yule dada wa kwenye ofisi ya idara yake pale chuo kikuu? Je hakuna shauri linalohusu ndoa ya mhusika hapa ama kwenye vyombo vya dini, ama idara zinazohusika hata hili gazeti libebe habari isiyokamilika? Au tu walitaka kutoa umbea wa maisha ya watu, tena ya siri mbele ya jamii? wanamjengea ama kumdhalilisha katibu wetu mkuu? maana huyo dada hatumshangai kwa habari za ajabu ajabu,
kama mke aliyefariki ni " Msanchi Simbeye" imawezekana dr bado ana ndoa halali na nyingine haramu.
ila wakubwa wanafaidi duh!
 
Vicky Kamata Afunga Ndoa na Dk. Likwelile


View attachment 331018 View attachment 331019



Dk Servacius Likwelile.

Dar es Salaam, Geita-Tanzania. Mbunge wa Viti Maalamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Vicky Kamata amefunga ndoa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dk Servacius Likwelile.


Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima (Jumamosi Machi 19, 2016)

Hakufunga ndoa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango; amefunga ndoa na Dk. Servacius Likwelile ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango.
 
Back
Top Bottom