Vice President Samia Hassan instructs public servants to ensure justice for all

Halina uhusiano wowote kwa sababu Lema si Mtanzania. Inaposemwa "Justice for all" ni kwa Watanzania tu. Hata baadhi ndani ya CCM wameanza kusema hadharani tena bila woga wa kumung'unya. Mwinyi, "Nchi inaenda kama gari bovu haina sukani" Warioba, "Nchi imepoteza muelekeo" Butiku, "Rais anayejiona yeye ni Tembo hatufai Watanzania. Hawa si wapinzani hawa ni watu ambao wamewahi kushika nafasi za juu Serikalini katika awamu mbali mbali lakini hawaridhishwi na muelekeo wa nchi. Pamoja na wao kuwa wanachama wa muda mrefu tangu enzi za TANU hadi CCM lakini wameona umuhimu wa kujitokeza hadharani na kuonyesha kutoridhishwa na hali hali ya nchi. Hata hawa bila shaka watakuwa ni wapiga majungu wazuri sana wafanya ujinga na wamejaa porojo tu ambazo hazina msingi wowote ule.

Wacheni Majungu, swala la Lema lina uhusiano gani na aliyosema VP? Hakuna hata moja mwenye ushahidi kwamba Lema anashikiliwa bila kufuata taratibu na sheria za nchi. Mwenye ushahidi kama anao ana nafasi ya kuifungulia kesi Serikali ya Tanzania mahakama kuu. Huu ulimbukeni wa kutoa maneno ambayo hamuwezi kufanya ni ujinga, tuache porojo, hivi nyinyi kweli mngeweza kusimamia haki wakati Tanganyika ilipokuwa inagawanywa na wazungu? Au mngeweza kupigania haki kama kina Mkwawa et al. Hizi porojo fanyeni majumbani kwenu mmeuziwa mbuzi kwenye gunia mmekaa kimya mtaweza kweli kuongoza nchi kweli au mnaangalia pua zenu tu.
 
Halina uhusiano wowote kwa sababu Lema si Mtanzania. Inaposemwa "Justice fo all" ni kwa Watanzania tu. Hata baadhi ndani ya CCM wameanza kusema hadharani tena bila woga wa kumung'unya. Mwinyi, "Nchi inaenda kama gari bovu haina sukani" Warioba, "Nchi imepoteza muelekeo" Butiku, "Rais anayejiona yeye ni Tembo hatufai Watanzania. Hawa si wapinzani hawa ni watu ambao wamewahi kushika nafasi za juu Serikalini katika awamu mbali mbali lakini hawaridhishwi na muelekeo wa nchi. Pamoja na wao kuwa wanachama wa muda mrefu tangu enzi za TANU hadi CCM lakini wameona umuhimu wa kujitokeza hadharani na kuonyesha kutoridhishwa na hali hali ya nchi. Hata hawa bila shaka watakuwa ni wapiga majungu wazuri sana wafanya ujinga na wamejaa porojo tu ambazo hazina msingi wowote ule.

BAK: Mwinyi - Huyu alipewa fagio la chuma, je, alifanya nini nalo zaidi ya kuwa Mzee Rukhsa, huyu kwa kweli anyamaze tu nchi ilimshinda.

Warioba - Alikuwa Waziri Mkuu unaweza kusema hata kimoja alichofanikiwa. Naye ni sifuri, he should just keep quite and enjoy his pension kutokana na huruma ya Watanzania.

Kuwa muda mrefu madarakani hakumaanishi ndio hekima au kuwa na mawazo chanya ya kuliondoa taifa kwenye lindi la umasikini. Walikuwepo na walishindwa hawana cha kujivunia bali wamekalia majungu tu ili waendelee kuneemeka na pesa za walipa kodi kwa sababu hawakuleta mafaniko yoyote wanatapatapa tu sasa. Same goes to Jambazi Sugu ambaye hukumtaja . We should stop supporting these thieves. Hivi wanaweza kweli kusema chochote ambacho walifanikiwa? Lets be serious and say no kwa hawa makuwadi wa kufilisi juhudi za wengine kuleta maendeleo. Ingekuwa nchi nyingine hawa wangeozea jela.
 
Kwa kuwa hawakufanikiwa basi hawastahili kuongea hadharani kuhusu kutoridhika kwao na muelekeo wa nchi.

Kama kuozea jela hata Magufuli naye alistahili kuozea jela. Kakwapua nyumba za Serikali na nyingine kuishia kuhonga, kalidanganya Bunge kuhusu upotevu wa zaidi ya bilioni 100 pesa za walipa kodi na pia kanunua kivuko uozo kwa bilioni 8 na sasa kiko juu ya mawe haya yote yamo ndani ya ripoti ya CAG.

Usimsafishe Magufuli kama vile ufisadi wake hatuujui.

BAK: Mwinyi - Huyu alipewa fagio la chuma, je, alifanya nini nalo zaidi ya kuwa Mzee Rukhsa, huyu kwa kweli anyamaze tu nchi ilimshinda.

Warioba - Alikuwa Waziri Mkuu unaweza kusema hata kimoja alichofanikiwa. Naye ni sifuri, he should just keep quite and enjoy his pension kutokana na huruma ya Watanzania.

Kuwa muda mrefu madarakani hakumaanishi ndio hekima au kuwa na mawazo chanya ya kuliondoa taifa kwenye lindi la umasikini. Walikuwepo na walishindwa hawana cha kujivunia bali wamekalia majungu tu ili waendelee kuneemeka na pesa za walipa kodi kwa sababu hawakuleta mafaniko yoyote wanatapatapa tu sasa. Same goes to Jambazi Sugu ambaye hukumtaja . We should stop supporting these thieves. Hivi wanaweza kweli kusema chochote ambacho walifanikiwa? Lets be serious and say no kwa hawa makuwadi wa kufilisi juhudi za wengine kuleta maendeleo. Ingekuwa nchi nyingine hawa wangeozea jela.
 
Kwa kuwa hawakufanikiwa basi hawastahili kuongea hadharani kuhusu kutoridhika kwao na muelekeo wa nchi.

Kama kuozea jela hata Magufuli naye alistahili kuozea jela. Kakwapua nyumba za Serikali na nyingine kuishia kuhonga, kalidanganya Bunge kuhusu upotevu wa zaidi ya bilioni 100 pesa za walipa kodi na pia kanunua kivuko uozo kwa bilioni 8 na sasa kiko juu ya mawe haya yote yamo ndani ya ripoti ya CAG.

Usimsafishe Magufuli kama vile ufisadi wake hatuujui.
Siasa Siasa Siasa.
 
Kwa kuwa hawakufanikiwa basi hawastahili kuongea hadharani kuhusu kutoridhika kwao na muelekeo wa nchi.

Kama kuozea jela hata Magufuli naye alistahili kuozea jela. Kakwapua nyumba za Serikali na nyingine kuishia kuhonga, kalidanganya Bunge kuhusu upotevu wa zaidi ya bilioni 100 pesa za walipa kodi na pia kanunua kivuko uozo kwa bilioni 8 na sasa kiko juu ya mawe haya yote yamo ndani ya ripoti ya CAG.

Usimsafishe Magufuli kama vile ufisadi wake hatuujui.

Mkuu hizo ni ngonjera ambazo hata kwenye maji haziwezi kuelea, we have been there before, mmekalia ati aliuza nyumba mnamwogopa che-nkapa? Huyo ndio alikuwa rais na kushika mpini mmebaki kuwewesekaweweseka tu sasa. Hawa viongozi waliovurunda hawawezi leo hii kuwa dira ya nchi hii. Huyo Warioba na Mwinyi sera zao haziwezi kukubalika na mtu yoyote yule mwenye akili timamu duniani. JPM ana sifa kem kem hivi sasa sio Bongo tu worldwide. Kama wewe humkubali na unalikubali Jambazi Sugu jichunguze.

Sina sababu ya kumsafisha JPM, record yake inajulikana na yeye ndio rais mtakula mawe mwaka huu.
 
Ni ngojera ila unachoandika wewe si ngojera! Nani anayemuogopa fisadi Mkapa!? Mbona kajadiliwa sana humu kama mwizi na fisadi!? Huo ushahidi wa kumuogopa Mkapa uko wapi!? Wakati Mwinyi na Warioba wanavurunda Serikalinini Magufuli alikuwa ndani ya Serikali hizo pia hata hakutia neon hata kwa sekunde moja maana naye alikuwa busy akifanya ufisadi wake. Eti Magufuli ana sifa kem kem Bongo & World wide! Acha unafiki Mkuu. Mwenye sifa kem kem KAMWE mkewe hawezi kugoma kumfanyia kampeni za kuwa Kiongozi wa nchi. Aliyeshindwa kuongoza nyumba yake kamwe hawezi kuongoza nchi. Acha kutetea mtu ambaye hana chochote cha kumtetea.

Mama Janeth Magufuli agoma kukampeni, acharuka

Mkuu hizo ni ngonjera ambazo hata kwenye maji haziwezi kuelea, we have been there before, mmekalia ati aliuza nyumba mnamwogopa che-nkapa? Huyo ndio alikuwa rais na kushika mpini mmebaki kuwewesekaweweseka tu sasa. Hawa viongozi waliovurunda hawawezi leo hii kuwa dira ya nchi hii. Huyo Warioba na Mwinyi sera zao haziwezi kukubalika na mtu yoyote yule mwenye akili timamu duniani. JPM ana sifa kem kem hivi sasa sio Bongo tu worldwide. Kama wewe humkubali na unalikubali Jambazi Sugu jichunguze.

Sina sababu ya kumsafisha JPM, record yake inajulikana na yeye ndio rais mtakula mawe mwaka huu.
 
Ni ngojera ila unachoandika wewe si ngojera! Nani anayemuogopa fisadi Mkapa!? Mbona kajadiliwa samba humu kama mwizi na fisadi!? Huo ushahidi wa kumuogopa Mkapa uko wapi!? Wakati Mwinyi na Warioba wanavurunda Serikalinini Magufuli alikuwa ndani ya Serikali hizo pia hata hakutia neon hata kwa sekunde moja maana naye alikuwa busy akifanya ufisadi wake. Eti Magufuli ana sifa kem kem Bongo & World wide! Acha unafiki Mkuu. Mwenye sifa kem kem KAMWE mkewe hawezi kugoma kumfanyia kampeni za kuwa Kiongozi wa nchi. Aliyeshindwa kuongoza nyumba yake kamwe hawezi kuongoza nchi. Acha kutetea mtu ambaye hana chochote cha kumtetea.

Mama Janeth Magufuli agoma kukampeni, acharuka

Kwa hiyo alikuwa waziri na hakusema chochote, Je, unaweza kuthibitisha hayo maneno kwamba hakusema chochote? Weka ushahidi hapa.
 
Wewe kama unao ushahidi kwamba alitoa kauli kukemea kuvurunda kwa Warioba na Mwinyi hebu tuwekee hapa, au kukemea ufisadi mbali mbali ndani ya Serikali ambazo aliwahi kuwa Waziri. Ufisadi wa EPA, Richmond/Dowans, Escrow, IPTL, Kagoda, Meremeta, Ununuzi wa Rada kama unao ushahidi wa kuonyesha yeye akikemea hayo uweke hapa.

Kwa hiyo alikuwa waziri na hakusema chochote, Je, unaweza kuthibitisha hayo maneno kwamba hakusema chochote? Weka ushahidi hapa.
 
Wewe kama unao ushahidi kwamba alitoa kauli kukemea kuvurunda kwa Warioba na Mwinyi hebu tuwekee hapa, au kukemea uufusadi mbali mbali ndani ya Serikali ambazo aliwahi kuwa Waziri. Ufisadi wa EPA, Richmond/Dowans, Escrow, IPTL, Kagoda, Meremeta kama unao ushahidi wa kuonyesha yeye akikemea hayo uweke hapa.
Mkuu umetoa kauli ambayo huwezi kutoa back up then unaniuliza, unaonyesha huwezi kujibu hoja na hii issue unaifahamu kijuujuu zaidi. Sakata la Nyumba za serikali lilianza hata kabla Che-nkapa hajashika madaraka go find out where it originates.
 
Acha kuzungusha zungusha maneno. Huwa sikurupuki mimi.

Habari hii ilichapishwa kwenye gazeti la RAI miaka michache iliyopita ikisomeka...

Huyu Ndiye Pombe Magufuli:

- Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
- Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani

ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya ‘fujo’ katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

“Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi,” vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

“Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili,” chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.

Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.

Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.

Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.

Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.

Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.

“Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.

Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.

SALVA RWEYEMAMU
RAI


Mkuu umetoa kauli ambayo huwezi kutoa back up then unaniuliza, unaonyesha huwezi kujibu hoja na hii issue unaifahamu kijuujuu zaidi. Sakata la Nyumba za serikali lilianza hata kabla Che-nkapa hajashika madaraka go find out where it originates.
 
Posted 10/3/2015
Ufisadi wa kutisha waibuliwa







magufuli_clip.jpg

Waziri wa Ujenzi Dk. John Pombe Magufuli akikagua ujenzi wa kituo cha Mradi wa Mabasi yaendayo haraka (BRT) Morocco jijini Dar es Salaam siku za hivi karibuni. Picha na Maktaba
By Ibrahim Yamola, Mwananchi

In Summary
Ukaguzi maalumu uliofanywa na ofisi ya CAG katika kipindi cha mwaka wa fedha 2010/11 na 2011/12 umebaini kuwa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, bungeni Novemba 2013 kuwa fedha hizo zilitumika kwa miradi ya ujenzi wa barabara, haikuwa sahihi.

Dar es Salaam. Machungu ya Watanzania yakiwa hayajapoa kutokana na kashfa ya Sh306 bilioni kutoka katika Akaunti ya Tegeta Escrow, ufisadi mwingine wa zaidi ya Sh252 bilioni umeibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad ndani ya wizara ya ujenzi.

Ukaguzi maalumu uliofanywa na ofisi ya CAG katika kipindi cha mwaka wa fedha 2010/11 na 2011/12 umebaini kuwa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, bungeni Novemba 2013 kuwa fedha hizo zilitumika kwa miradi ya ujenzi wa barabara, haikuwa sahihi.

Kutokana na ufisadi huo, habari zilizolifikia Mwananchi zinasema CAG amependekeza hatua stahiki zichukuliwe kwa wahusika wa wizara ya ujenzi na wakala wa barabara ili kuleta imani na uwazi katika bajeti kwa jamii na wahisani.

“Wizara (ya ujenzi) ililidanganya Bunge kuwa kuna ujenzi wa barabara hizo wakati wakijua kwamba walikusudia kulipa madeni ya wakandarasi na washauri wa ujenzi wa barabara...mpango mkakati wa wakala wa barabara wa mwaka wa fedha 2011/12 pamoja na manunuzi ulioidhinishwa havikuonyesha utekelezaji wa mradi huo,” chanzo cha habari kilikariri ripoti ya CAG.

Matumizi hayo yasiyo sahihi yaliibuliwa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) Novemba 22, 2013 baada ya kutilia shaka kiasi hicho cha fedha na ofisi ya CAG kuagizwa kufanya ukaguzi.

Katika kikao hicho ambacho wizara ya ujenzi iliwakilishwa na Katibu Mkuu wake wa wakati huo, Balozi Herbert Mrango alihojiwa na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa CAG mwaka 2011/12.

Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo Sh348.1 bilioni zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililokuwa limetajwa kuwa ni la mradi maalumu hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni.

“Ni vizuri leo (ilikuwa Novemba 22 mwaka 2013) uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. Tunajua kwamba fedha hizi zilipunguzwa Sh95 bilioni na kupelekwa Wizara ya Uchukuzi, zilibakia Sh252.975 bilioni katika kifungu hicho lakini kuna bilioni 100 zimetumika visivyo,” alisema Zitto.

Alisema katika majumuisho ya bajeti wizara hiyo, Dk Magufuli na Dk Harrison Makyembe aliyekuwa Naibu waziri wa wakati huo aliyekuwa Waziri wa Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi walitoa maelezo yasiyo ya kweli bungeni kuhusu fedha hizo.

Zitto alikariri maneno yaliyorekodiwa kwenye Hansard ya Bunge yaliyosemwa na viongozi hao watatu.

“Tunaomba fedha Sh252 bilioni kwa ajili ya kuanzia kazi za ujenzi wa barabara.”

“Fedha hizi zitachangia miradi ya wafadhili,” haya yalikuwa maneno ya Dk Makyembe ambaye sasa ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati akifafanua majumuisho.

“Hizi ni fedha kwa ajili ya Counterpart fund,” alimkariri Lukuvi ambaye sasa ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakati akichangia hotuba ya wizara hiyo.

Chanzo cha habari kimeeleza kuwa ripoti ya CAG imeeleza kuwa, “Katika kikao cha kuanza ukaguzi huo Aprili 3, mwaka jana uongozi wa wizara ulithibitisha kwamba hakukuwa na barabara mpya bali walifanya hivyo baada ya kuona madeni yamekuwa makubwa kiasi cha Sh420 bilioni kama yalivyokuwa kwenye hesabu za wakala wa barabara za mwaka wa fedha 2010/11.”

Katika ukaguzi huo imebainishwa kuwa Sh3 bilioni hazikujulikana matumizi yake.

Taarifa zaidi zinasema baada ya wizara kupeleka fedha kwa wakala wa barabara, fedha hizo zilifanyiwa mchakato wa kuzigawa upya lakini nyaraka halisi zilizotumika kugawa fedha hizo hazikuwasilishwa kwa ukaguzi.

“Hata hivyo, kati ya Sh175.3 bilioni zilizopitia kwenye akaunti ya maendeleo ya wakala wa barabara, kiasi cha Sh3,048,365,229 hakikuweza kupatiwa maelezo jinsi kilivyotumika.

“Pia, kati ya malipo ya Sh77.7 bilioni yaliyofanyika kwa wakandarasi au washauri wa barabara moja kwa moja kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Novemba 30, mwaka 2011 kupitia barua ya kumbukumbu namba GA.65/263/01/VOL.XI Gavana Mkuu wa BoT, alikanusha kulipa asilimia 30 ya fedha hizo Sh30.6 bilioni.

“Gavana wa BoT amekanusha kulipa Sh30.6 bilioni kwa kampuni ya M/S Strabag Internationl Gmbn na M/S China-Engineering Corporation Co, kati ya Sh77.7 ambacho kilipelekwa BoT kwa ajili ya malipo kwa wakandarasi au washauri mbalimbali,” alifafanua zaidi mtoa habari hizi na kuongeza:

“Ukaguzi maalumu umeshindwa kuthibitisha malipo yenye jumla ya Sh47.1 bilioni sawa na asilimia 61 kama yalilipwa kwa walengwa waliokusudiwa kwa sababu Gavana wa BoT amesema kuwa kisheria hatakiwi kutoa taarifa za wateja.”

Pia, habari za ndani kutoka ofisi ya CAG zinadai kuwa, Sh13.4 bilioni za ujenzi wa barabara za mikoa zilitumika kulipia barabara binafsi na za halmashauri za wilaya ambazo hutengewa fedha kupitia mfuko wa barabara kinyume na makusudio yaliyopitishwa na Bunge.

“Pia, nimebaini kwamba baadhi ya miradi haikuwamo kwenye kasma zilizopitishwa na Bunge kwenye makisio ya mwaka wa fedha 2010/11 na miradi mingine ilitengewa fedha kidogo lakini wakala wa barabara alitumia fedha nyingi kulipia miradi hiyo bila kuonyesha jinsi alivyozipata,” chanzo cha habari kimekariri ripoti ya CAG.

Katika ukaguzi huo, ufisadi mwingine wa Sh36.6 bilioni ambazo ni malipo ambayo hayakutolewa taarifa kwenye ripoti za washauri au wakandarasi, jambo linaweza kuwapo kwa uwezekano mkubwa wa wakandarasi kuidai Serikali zaidi ya mara moja na kuitia Serikali hasara.

Mtoa habari wetu alisema kuwa Sh6.2 bilioni zilitumika kuwalipa wakandarasi ambao hawakuonyeshwa katika orodha ya madeni yaliyowasilishwa bungeni pamoja na malipo ya Sh6.6 bilioni yaliyokwishalipwa yaliombewa tena.

“Madeni hayo yalikuwa yamelipwa na wakala wa barabara katika mikoa husika. Hali hii inaashiria kwamba kwa hati ya madai moja kuna uwezekano wa mkandarasi kulipwa mara mbili au zaidi.

Katika mapendekezo ya jumla, chanzo chetu kimesema ofisi ya CAG imeishauri Serikali kusimamisha kuingia mikataba mipya ya ujenzi wa barabara na ilipe madeni ya wakandarasi yaliyopo kwa sasa ili kuepuka ukuaji wa deni hilo kwa siku za baadaye na kuwa mzigo kwa Taifa na wananchi.

“Serikali ihakikishe inaheshimu mikataba iliyowekwa kati yake na wakandarasi ili kuepuka malipo yenye riba na kushtakiwa na wakandarasi kutokana na kuvunja masharti yaliyowekwa kwenye mikataba,” kilifafanua chanzo chetu na kuongeza:

“Zabuni za ujenzi wa barabara mpya ziendane na fedha zilizotengwa katika mwaka wa fedha husika kama itakavyokuwa imeainishwa katika mpango wa manunuzi wa mwaka huo.”

Ukaguzi huo maalumu uliohusisha miradi 46 ya ujenzi wa barabara kuu na barabara za mikoa ambazo wakandarasi na washauri wa ujenzi wa barabara walitoa huduma kwa wakala wa barabara.

“Mbali na miradi hii 46, miradi yote ya wakala wa barabara ilikuwa imezalisha madeni ya jumla ya Sh420 bilioni kama yalivyo kwenye hesabu za wizara kufikia mwaka wa fedha 2010/11,” kilieleza chanzo chetu.

Sakata hili limeibuka wakati lile la uchotwaji wa fedha za Akautni ya Tegeta Escrow halijapoa na hadi sasa limesababisha Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko madogo ya baraza lake la mawaziri kufuatia kumfukuza kazi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka huku Profesa Sospeter Muhongo alitangaza kuachia wadhifa wa Waziri wa Nishati na Madini.

Mbali na hao, pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alitangaza kujiuzuru huku Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akimsimamisha kazi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi kupisha uchunguzi wa sakata hilo.

Katika mlolongo wa hatua za kinidhamu kuchukuliwa, baadhi ya watumishi wa umma wamefikishwa mahakamani na wengine mbele ya Baraza la Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.


BAK

Kwa hiyo gazeti la Rai ndio source yako?
 
BAK Mkuu mbona hukubali hizo source ambazo una-base your argument ili twende vizuri maana naona una paste tu habari, we need to argue this topic as learned people, sio ku-argue tu for the sake of it?
 
haya wanayoyasema yako kilometer millioni mia moja na tunayoyaona .mbona kwenye mambo ya uchaguzi hawalisemei hilo .hata umeya tu ni shida
 
Unataka kuargue na mtu anayeandika ngojera, lakini wewe huandiki ngonjera pamoja na kuwa huna hata evidence yoyote ile ya kusupport ulichoandika!? Unataka kuargue nini tena wakati wewe umeshatoa hitimisho lako, ,"JPM ana sifa kem kem hivi sasa sio Bongo tu worldwide." wakati hujatuambia sifa hizo zinatokana na kipi alichokifanya Tanzania au duniani mpaka amwagiwe sifa hizo!? Hizo sifa kem kem World wide ni kutoka kwa akina nani wa nchi zipi?

BAK Mkuu mbona hukubali hizo source ambazo una-base your argument ili twende vizuri maana naona una paste tu habari, we need to argue this topic as learned people, sio ku-argue tu for the sake of it?
 
Unataka kuargue na mtu anayeandika ngojera, lakini wewe huandiki ngonjera pamoja na kuwa huna hata evidence yoyote ile ya kusupport ulichoandika!? Unataka kuargue nini tena wakati wewe umeshatoa hitimisho lako, ,"JPM ana sifa kem kem hivi sasa sio Bongo tu worldwide." wakati hujatuambia sifa hizo zinatokana na kipi alichokifanya Tanzania au duniani mpaka amwagiwe sifa hizo!? Hizo sifa kem kem World wide ni kutoka kwa akina nani wa nchi zipi?

Mkuu huwezi kutoa source then unakataa kukubali kwamba argument yako ipo-based na hizo source/s, kubishana ki-JF mpya without facts is a waste of time. Based on the sources you have provided there is no need for me to continue; that is why I told you, what you know is not enough to understand the process of government workings etc. You need to know more than what Rai has provided or whoever has given you those false information before you make an informed decision. Based on that, I am quite confident that you do not know what transpired and hence your emotions has taken over.
 
Stop your nonsense please! Who told you that my emotions has taken over!? Any evidence!? Kama huna cha maana cha kuandika kaa kimya badala ya kuja na kauli hewa ambazo huna uthibitisho hata chembe zaidi ya kukurupuka na kuandika pumba zako. Niliuliza maswali hata moja umeshindwa kulijibu.

Nayarudia tena hapa maswali hayo. "JPM ana sifa kem kem hivi sasa sio Bongo tu worldwide." wakati hujatuambia sifa hizo zinatokana na kipi alichokifanya Tanzania au duniani mpaka amwagiwe sifa hizo!? Hizo sifa kem kem World wide ni kutoka kwa akina nani wa nchi zipi?

Kama huna majibu sema sina majibu badala ya kumsifia mtu ambaye katika miezi michache tu uongozi wa nchi umeshamshinda. Kaangusha uchumi kwa kukurupuka kwake na vitu ambavyo hana ufahamu navyo. Kapaisha deni la Taifa kwa 55.8% sawa na 24 Trillioni toka 43 Trilioni hadi 67 Trillioni. Haliheshimu Bunge kwa kutumia pesa bila idhini ya Bunge. Haiheshimu katiba ya nchi pamoja na kula kiapo mbele ya mamilioni ya Watanzania na kuahidi kulinda na kuiheshimu katiba ya nchi. Hawajali Watanzania, kule Kagera ni mwezi wa nne sasa unaingia tangu tetemeko la ardhi litokee lakini hataki kwenda kuwapa pole na kawapora bilioni 16 zilizochangwa ndani na nje ya nchi. Pumba unazoandika humu peleka lumumba kule watakuelewa sana.

Mkuu huwezi kutoa source then unakataa kukubali kwamba argument yako ipo-based na hizo source/s, kubishana ki-JF mpya without facts is a waste of time. Based on the sources you have provided there is no need for me to continue; that is why I told you, what you know is not enough to understand the process of government workings etc. You need to know more than what Rai has provided or whoever has given you those false information before you make an informed decision. Based on that, I am quite confident that you do not know what transpired and hence your emotions has taken over.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom