Vibanda vya machinga kando ya barabara Dar jifanyeni hamvioni

Vibanda vya machinga kando ya barabara Dar jifanyeni hamvioni

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,341
Reaction score
15,842
Mara ya pili leo nimeona gari limeacha njia hapa mlimani city nakuingia mtaroni. Kabla ya mtaro wamejipanga machinga na mabanda yao ambayo siku zote jiji wanajifanya hawavioni wanaacha kila siku wanavamia na kujenga mabanda. Mara ya kwanza kama miezi miwili lori la mafuta liliacha njia na kuingia mtaroni hapahapa mlimani city na likaua. Subirini lije janga kubwa mtumbuliwe ndo mtakua proactive sababu daily mnapita humu na mnaona.
 
Mkuu ukiondoa vibanda unataka watu waishi vipi ?

Nchi hii ina watu karbu milioni 60 lakini serikali imeajiri watu laki 5 tu na wengi wao serikali imeshindwa kuwahudumia, wana maisha magumu.

So hapo unategemea nini ?
 
Mkuu ukiondoa vibanda unataka watu waishi vipi ?

Nchi hii ina watu karbu milioni 60 lakini serikali imeajiri watu laki 5 tu na wengi wao serikali imeshindwa kuwahudumia, wana maisha magumu.

So hapo unategemea nini ?
Ni hatari kurisk maisha yao maana we mwenyewe unajua jinsi dar magari yanavyokimbia utasema mtu anaenda mkoani kumbe anaenda kubeba zigo sinza
 
Mkuu ukiondoa vibanda unataka watu waishi vipi ?

Nchi hii ina watu karbu milioni 60 lakini serikali imeajiri watu laki 5 tu na wengi wao serikali imeshindwa kuwahudumia, wana maisha magumu.

So hapo unategemea nini ?
Haya majibu ya watu wataishi vipi yatapatikana siku yakitokea madhara.
Wenzetu wameweka sheria ili kuzuia maafa sisi maafa yakitokea ni mpango wa Mungu kumbe tulikuwa na uwezo kuyazuia
 
Hao machinga ni mtaji wetu kwenye kura..subiri kidogo uchaguzi umalizike.

Tutawashukia kama hatuwafahamu vile..!
 
Kwani si waliruhusiwa? Na aliye waruhusu siku janga likitokea yeye atakuwa nyumba nyeupe, itabakia mchuma janga hula na wakwao!
 
Nje ya mada hivi kwanini wasiweke pia njia ya lugalo vibanda si wameruhusiwa na mkuu wafanyie popote wangefanya kupanua huduma.
 
Serikali makini ya CCM katika kuhakikisha kuwa inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wananchi wanyonge ili nao waweze kufanya biashara zao bila usumbufu imeliona hilo na lipo tayari kwenye ilani yetu ya uchaguzi ukurasa wa 22. Mchague Magufuli ili ayo unayoyapigia kelele na mengine mengi na mazuri zaidi yapate kufanyiwa kazi.
20200910_161918.jpg
 
Haya majibu ya watu wataishi vipi yatapatikana siku yakitokea madhara.
Wenzetu wameweka sheria ili kuzuia maafa sisi maafa yakitokea ni mpango wa Mungu kumbe tulikuwa na uwezo kuyazuia
Basi bodaboda zote zipigwe marufuku, wachibaji wadogowadogo migodini wapigwe marufuku, mama-ntilie water wapigwe marufuku. Au sio Mkuu?!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom