DOKEZO Vibanda Holela Ubungo/Kijazi interchange

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Trubarg

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2020
Posts
4,398
Reaction score
7,252
Ni ajabu kuona zile juhudi zilizofanyika kusafisha jiji miaka ya nyuma zinapuuziwa kutokana na watendaji kutokufanya majukumu yako ipasavyo.

Nachojiuliza hivi vibanda vinavyochipukia kama uyoga chini na pembezoni mwa daraja na Songas hamvioni. Au mnasubiria mpaka maduka yawe makubwa ndo mje tena mtumie nguvu za ziada kuvunja.
 
Chukulia mfano wewe ndio hao wenye hivyo vibanda na unahitaji fedha kupata mahitaji yako, je utatumia njia zipi?
 
kweli hakuna unafuu
Nilikua nikionaga bei za china na bongo huwa nasema wafanyabiashara wetu wanatupiga sana. Nilivyoingia kwenye biashara mimi mwenyewe nikaelewa vizuri.

Picha linaanza kodi 600k/month. Halmashauri, tra, ulinzi, ku-import mzigo, gharama zingine za uendeshaji. Nchii ni kama mamlaka zina bifu na wananchi. Kila mwananchi unavyopambana kuinuka jukumu la mamlaka ni kukupiga nyundo ya utosi urudi chini
 
Na ndiyo maana wafanyabiashara wanaletaga vitu fake toka china ili tu abalance kwenye faida,sio kwamba vitu original havipo hapana ni namna biashara imekua ngumu sana na serikali inachukua tu pasipo kumpa unafaa mfanyabiashara ili aendelee kwenye biashara
 
Mbezi Mwisho pale Stand ya Daladala vinakaribia kuingia ndani kabisa.
 
Nchi hii unahitaji viongozi wenye akili za ziada. Haiwezekani vibanda kila mahali alafu viongozi wanasinzia usingizi WA pono.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…