Vibali vipi vinahitajika ili kufungua biashara?

Vibali vipi vinahitajika ili kufungua biashara?

Forgotten

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
3,630
Reaction score
11,096
Habari, wana-JF naomba kueleweshwa kuhusu vibali vinavyohitajika kabla sijafungua biashara mpya, maana kuna kauli za kisiasa na sheria zilizopo vinanichanganya.

Ikumbukwe, mwaka 2023 ilitoka kauli kutoka kwenye serikali ya Samia kuwa wafanya-biashara wapya watapewa muda kufanya biashara kwa kipindi cha miezi 6 mpaka mwaka 1 bila kutozwa kodi.

Sasa, kuna mtu nafahamiana naye yupo Maisapaa nilimtafuta ili kumuuliza taratibu na gharama za kupata leseni ya biashara ninayotaka kufungua, akaniambia niende miezi 3 baada ya kufungua biashara.

Maana yake, baada ya miezi mitatu niende TRA nikiwa na TIN, mkataba wa pango na barua ya utambulisho, ili nipate Tax Clearance, ndiyo niende Manispaa/Tausi Portal kwaajili ya leseni.

Sasa, wasiwasi wangu ni kwamba ndani ya hii miezi mitatu wazee wa tai mbele wanaweza kuvamia ofisini na wakikuta sina vibali inaweza kuleta shida japokuwa tayari kuna matamko ya kisiasa na sheria ambazo hazipo wazi kwa wafanya-biashara.

Naomba ushauri wenu wazoefu au ambao mna taarifa zaidi ya hizi nilizonazo mimi.
 
Habari, wana-JF naomba kueleweshwa kuhusu vibali vinavyohitajika kabla sijafungua biashara mpya, maana kuna kauli za kisiasa na sheria zilizopo vinanichanganya.

Ikumbukwe, mwaka 2023 ilitoka kauli kutoka kwenye serikali ya Samia kuwa wafanya-biashara wapya watapewa muda kufanya biashara kwa kipindi cha miezi 6 mpaka mwaka 1 bila kutozwa kodi.

Sasa, kuna mtu nafahamiana naye yupo Maisapaa nilimtafuta ili kumuuliza taratibu na gharama za kupata leseni ya biashara ninayotaka kufungua, akaniambia niende miezi 3 baada ya kufungua biashara.

Maana yake, baada ya miezi mitatu niende TRA nikiwa na TIN, mkataba wa pango na barua ya utambulisho, ili nipate Tax Clearance, ndiyo niende Manispaa/Tausi Portal kwaajili ya leseni.

Sasa, wasiwasi wangu ni kwamba ndani ya hii miezi mitatu wazee wa tai mbele wanaweza kuvamia ofisini na wakikuta sina vibali inaweza kuleta shida japokuwa tayari kuna matamko ya kisiasa na sheria ambazo hazipo wazi kwa wafanya-biashara.

Naomba ushauri wenu wazoefu au ambao mna taarifa zaidi ya hizi nilizonazo mimi.
Miezi mitatu kwanini? Kama una uwezo bora ulipie tu mwenyewe tausi, tena gharama haitazidi laki2 kutegemea aina ya biashara na biashara ilipo.

Otherwise wakikuotea jiandae kulipa faini kubwa zaidi
 
Unataka kufungua biashara wapi. Mbona just simple Nenda TRA Upate Tin ya biashara than wakupe clearence than uende Manispaa au jaza mwenyewe kwenye mfumo wao Tausi. Than the rest is history
 
Miezi mitatu kwanini? Kama una uwezo bora ulipie tu mwenyewe tausi, tena gharama haitazidi laki2 kutegemea aina ya biashara na biashara ilipo.

Otherwise wakikuotea jiandae kulipa faini kubwa zaidi
OK! Na TRA kwenye Tax Clearance kuna makato yoyote yanafanyika na baada ya makadirio kodi inaanza kutozwa baada ya kipindi gani?

Asante kwa maoni yako!
 
Unataka kufungua biashara wapi. Mbona just simple Nenda TRA Upate Tin ya biashara than wakupe clearence than uende Manispaa au jaza mwenyewe kwenye mfumo wao Tausi. Than the rest is history
Nataka ku-apply TIN online. Je, niende nikafanye process zote za TIN na Tax Clearance kwenye ofisi zao?

Asante kwa maoni yako!
 
Nataka ku-apply TIN online. Je, niende nikafanye process zote za TIN na Tax Clearance kwenye ofisi zao?

Asante kwa maoni yako!
Ukiwa na Nida unaweza kufanya mwenyewe kwenye mfumo wao taxpayerportal.tra.go.tz than ingia sehemu ya log up au sin up. Clearence lazima uende ofisini
 
Mkuu upo wapi..
Naweza kukusaidia A to Z kwa njia rahisi kabisa ambayo takupa hapa hapa jf
 
Back
Top Bottom