Viapo vya ndoa havitekelezeki

Viapo vya ndoa havitekelezeki

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,686
"Harusi na viapo visivyotekelezeka".

Ahadi ya kuwa pamoja maishani katika shida na raha,taabu na shida viapo hivi ama ahadi hizi zinaonekana kuchukuliwa kirahisi mno na wanandoa wapya, lakini kwa muujibu wa utafiti mpya uliotolewa hivi karibuni unathibitisha kuwa ni rahisi mno kutamka kuliko utekelezaji wa viapo vyenyewe .

Utafiti uliofanywa kwa wanandoa wenye bahati 2,700 waliooana umegundua kwamba, ikiwa mwanamke katika ndoa hiyo ataugua kwa muda mrefu asilimia sita hukaribia kupewa talaka kuliko wale ambao wana afya njema .

Ukilinganaisha na wanaume ambao huugua wakiwa kwenye ndoa, hatari ya kuvunjika kwa ndoa ni ndogo mno, hatahivyo upendo huendelea hadi hapo mmoja wao atakapo baki kuwa mgane ama mjane.

Utafiti ulioongozwa na wanazuoni wa chuo kikuu nchini Marekani, kinapendekeza kwamba kwa asili, wanawake wao wameumbwa kutoa huduma katika familia zao na hii inamaanisha kwamba wanaume wao huwa hawana uvumilivu kwa wake zao pindi wanapokumbwa na maradhi ya muda mrefu, ambayo pia yanaweza kuwa hayatabiriki kuyakabili.

Walifanyiwa utafiti wanandoa nchini Marekani, ambao wote walikuwa na umri wa miaka 50, mnamo mwaka 1990 ambao waliulizwa juu ya afya zao kuhusiana na maisha yao wakichunguzwa kwa muda wa miaka miwili, miwili ndani ya utafiti uliofanywa kwa miaka ishirini.

Asilimia thelathini na mbili ya ndoa ziliishia kwa kuachana na asilimia ishirini na nne zilivunjika kutokana na vifo vya mmoja wa wanandoa.

Kikosi cha utafiti kiliongozwa na Amelia Karraker, ambaye ni profesa msaidizi juu ya masuala ya maendeleo ya binaadamu na utafiti juu ya familia kutoka katika chuo cha Iowa State University, analinganisha matukio ya namna nne: kansa, magonjwa ya moyo, kiharusi na magonjwa ya njia ya hewa kwa wanawake na wanaume na matokeo ya ndoa.


Tamu na chungu ya ndoa

Utafiti huo umebainisha kwamba , kuna tofauti ya kujisikia mgonjwa sana na huwezi kupika chakula cha jioni, ama unahitaji mtu hasa wa kukulisha masuala haya yanaweza kubadili upepo ndani ya ndoa .

Katika hali hiyo, utafiti huo hauonyeshi dhahiri kuwa mume ama mke anadai talaka, takwimu kamili zinaonyesha kwamba wanawake ni wepesi zaidi kuomba talaka kuliko wenza wao.

Bi Karraker anasema amegundua kwamba inawezekana baadhi ya wanawake ambao huachwa kwasababu ya huduma zao ama kushindwa kuhudumia.

Tafakari juu ya Uhai ama kifo husababisha watu wajitafiti wenyewe na kujiuliza maswali muhimu kuwa ni nini muhimu maishani mwao? Anaeleza mtafiti huyo.
Wanawake wakati mwingine huibuka kwa kusema kuwa waume zao hawawajali, na hawafurahishwi na suala hilo ama husema sikufurahishwa na mwanzo wa mahusiano yao, na wanasema kwamba wako radhi kubaki peke yao kuliko kujitosa katika ndoa isiyofaa.


Chanzo: bbc
 
Back
Top Bottom