VENEZUELA builds its first Drone( pilotless) and riffle with IRAN's help

VENEZUELA builds its first Drone( pilotless) and riffle with IRAN's help

BINARY NO

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2011
Posts
2,155
Reaction score
2,171
president Hugo Chavez said in a televised speech " They are made in our country with military engineers who went to do course in the sister Republic of IRAN,This has shocked US much since Venezuela is also anti US and its said IRAN has built military bases in venezuela which Stock its missile capable of reaching US....
 
president Hugo Chavez said in a televised speech " They are made in our country with military engineers who went to do course in the sister Republic of IRAN,This has shocked US much since Venezuela is also anti US and its said IRAN has built military bases in venezuela which Stock its missile capable of reaching US....

Unawaita "the sister republic of Iran"? Hawa jamaa wamesoma na sasa ni miongoni mwa nchi zinazosifika kwa technology.Sisi tutaendelea na ushabiki na kusota ktk vumbi kwenye vikao vya CCM,CDM na CUF huku tukijua tunadanganywa na sisi tupo tu kama majuha.
 
chaves ni rais mwenye maamuzi magumu kwa manufaa ya nchi yake!us anataka auze silaha yeye peke yake dunia nzima
 
Chezea israel wewe kumbuka vta ya siku sita kapiga nchi saba
 
Dunia ingekuwa na marais 5 kama Hugo ingekuwa safi sana. USA wamefika hatua ambayo na wao wanatakiwa wadhibitiwe na imperialism yao. Lazima kuwe na world power balance, lakini si kama ilivyo sasa...
 
Ile cancer ni original au ya kutengenezwa maana haya majamaa ya west utata mtupu.
 
huwezi mkabizi kichaa bunduki au kisu
Ni nani kichaa?

Marekani ambaye aliipiga miji ya Hiroshima na Nagasati huku akijua anauwa maelfu ya raia wasio na silaha, amewaunga mkono madikteta na wauaji wengi wa Afrika, ameuwa malaki ya wa Iraq wasio na hatia, ameendelea kuua maelfu ya raia wasio na hatia Afghanistan, ameibadilisha Libya kutoka nchi ya asali na maziwa kuwa nchi ya mauaji, majuto na laana zote huku akiiba mafuta.

Israel Imekuwa na silaha za nyuklia peke yake mashariki ya kati, imepora ardhi ya wapelestina wasio na silaha, imekuwa ikiwauwa waPalestina wasio na silaha kwa kutumia mabomu ya sumu ambayo hayakubaliki duniani, imewahi kuzishambulia nchi kama Syria, Sudan na Iraq kwa kuhisi tu wanatengeza silaha kali, na hivyo yaweza shambulia nchi yoyote duniani kwa kuhisi tu.

Iran haijawahi ivamia nchi yoyote duniani wala kuua watu ovyo. Je kwa kutengeneza nishati ya nuklia tu ni tishio?
,
 
Ni nani kichaa?

Marekani ambaye aliipiga miji ya Hiroshima na Nagasati huku akijua anauwa maelfu ya raia wasio na silaha, amewaunga mkono madikteta na wauaji wengi wa Afrika, ameuwa malaki ya wa Iraq wasio na hatia, ameendelea kuua maelfu ya raia wasio na hatia Afghanistan, ameibadilisha Libya kutoka nchi ya asali na maziwa kuwa nchi ya mauaji, majuto na laana zote huku akiiba mafuta.

Israel Imekuwa na silaha za nyuklia peke yake mashariki ya kati, imepora ardhi ya wapelestina wasio na silaha, imekuwa ikiwauwa waPalestina wasio na silaha kwa kutumia mabomu ya sumu ambayo hayakubaliki duniani, imewahi kuzishambulia nchi kama Syria, Sudan na Iraq kwa kuhisi tu wanatengeza silaha kali, na hivyo yaweza shambulia nchi yoyote duniani kwa kuhisi tu.

Iran haijawahi ivamia nchi yoyote duniani wala kuua watu ovyo. Je kwa kutengeneza nishati ya nuklia tu ni tishio?
,

unasema Iran haijawahi kushambulia nchi yoyote?!, unakumbuka vita ya Iraq na iran?!, ilichukua miaka mingapi?!
 
oh my gudness it seems history inakupita pembeni.. Iran haijawahi kuishambulia nchi yoyote ila ilipigana na Irak kwa miaka 8 baada ya Sadam kuivamia IRAN na ikumbukwe kipindi chote cha vita Sadam alikua anapatiwa silaha nzito na US,UK ila aweze kuipiga IRAN mpaka akadiriki kutumia chemical weapon agains iranians na apa kuna visa na ushahidi mwingi kua US alikua bega kwa bega na IRAK

Kwani ata baadhi ya meli mbili za kivita za IRAN zilizamishwa na US japo na US alipoteza meli na hiyo yote ni mapinduzi ya 1979 yaliouondoa utawala wa kifalme IRAN ambao ulikua rafiki wa US mpaka leo hawana ubalozi IRAN.....

Lakini mwisho IRAN ilishinda na tokea 1980 ndo akawekewa vikwazo vya uchumi na silaha ndo mwanzo wa kusomesha wanafunzi mpaka leo hii IRAN ina export silaha
 
unasema Iran haijawahi kushambulia nchi yoyote?! unakumbuka vita ya Iraq na iran?!, ilichukua miaka mingapi?!

Utakuwa unapoteza kumbukumbu kwa haraka mno. Ni Iraq ikisaidiwa na Marekani ndio iliivamia Iran. Wakati huo wamerekani walilisaidia jeshi la Iraq likawa kubwa zaidi ya mara tatu na silaha nyingi zikiwemo za sumu.

Huku Iran wakiwekewa vikwazo vya kupata silaha. Hata hivyo wairan walipigana kiume hawakushindwa mpaka vita vilipoisha 1998.

Cha ajabu Marekani walimgeuka swahiba wao Sadam na kupelekea kunyongwa!
 
Back
Top Bottom