Vazi la Rais Uhuru Kenyatta

Vazi la Rais Uhuru Kenyatta

Mtani Nyani Ngabu, mbona hata Rais Magufuli alitinga 'gwanda za kijeshi' kule Arusha? Rais aweza kuvaa atakavyo, kikubwa ni kuwa mavazi ya heshima na staha

Hoja yangu ni kwamba, akivaa Magufuli tunaaminishwa kuwa kavaa hivyo kwa sababu ni dikteta.

Uhuru tunaaminishwa kwamba ndo mmoja wa vinara wa demokrasia.

Sasa Uhuru akivaa kijeshi bado anakuwa kinara wa demokrasia au anakuwa dikteta?
 
Mtani Nyani Ngabu, mbona hata Rais Magufuli alitinga 'gwanda za kijeshi' kule Arusha? Rais aweza kuvaa atakavyo, kikubwa ni kuwa mavazi ya heshima na staha
Mara nyingi aina ya mavazi huonesha tabia ya ndani ya mtu hasa mtu huyu akiwa na uchimi au uwezo wa kuvaa atakavyo!
 
Ni Jamhuri Day huko Kenya na Rais Kenyatta kavaa kijeshi!

Angekuwa ndo Rais Magufuli kafanya hivyo majuzi kwenye sikukuu ya Uhuru pasingekalika humu.


Hivi unajua kuwa Rais wa Kenya ana vazi maalum la kijeshi ndani ya jeshi? Huyu wa kwetu hata haelewi taratibu za mavazi ya kijeshi. Yan anadandia dandia tu!
 
Unaaminishwa na nani?? akili zingine bhn so kesho ukiaminishwa na hao unaowaita wanakuaminisha kwamba Magufuli ni malaika then kesho ukaona vinginevyo utasema mbona tuliaminishwa kuwa yeye ni malaika!! ulishaona/kusikia wapi udikteta unapimwa kwa mavazi? hata avae vazi la kitenge daily kama matendo yake hayasadifu hataonekana mwema.

Magu is not yet a dictator japo tu ana mapungufu yake ya kiuongozi na hamna kiongozi ambae atakuwa perfect lakini pamoja na hivyo hatakama mtu uko on his side haimaanishi ndio uwe kipofu wa ku-rise hoja dhaifu.
 
Hivi unajua kuwa Rais wa Kenya ana vazi maalum la kijeshi ndani ya jeshi? Huyu wa kwetu hata haelewi taratibu za mavazi ya kijeshi. Yan anadandia dandia tu!
Sidhani kama unalolisema linaukweli ,hata kama kuna chuki zingine Ila kwa hili si kweli
 
Hivi unajua kuwa Rais wa Kenya ana vazi maalum la kijeshi ndani ya jeshi? Huyu wa kwetu hata haelewi taratibu za mavazi ya kijeshi. Yan anadandia dandia tu!

Wewe ni mwanajeshi? Una uhakika rais wetu hana vazi lake maalumu jeshini kama jemedari mkuu wa majeshi?
 
Ni Jamhuri Day huko Kenya na Rais Kenyatta kavaa kijeshi!

Angekuwa ndo Rais Magufuli kafanya hivyo majuzi kwenye sikukuu ya Uhuru pasingekalika humu.


Magufuli alishavaa hivyo ila sikumbuki kama aliitwa dictator
 
Back
Top Bottom