Siri ya sifuri
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 2,014
- 1,498
Umzaniae ndie kumbe siye, Ameumbika kwelikweli, mrefu wa wastani ana mwili mkubwa lakini sio tinginya,mweusi tii anameremeta akipaka mafuta, ana kifua kipana na manyonyo yaliyojazia, analo pia kalio linalotingishika akitembea. Niseme ule ukweli nilimtamani na baadae nikampenda kwa dhati.
Sikua na jinsi zaidi ya kujipendekeza, kwa haraka tukawa marafiki ila hakuwa tayari tuwe mwili mmoja, kwanini!?hakunambia na sikuweza kufikiri wala kuhisi kwamba anatat, nilidhani ni mbwembwe tu za usistaduu mpaka siku mmoja wa shoga zake alipotambua nyendo zangu kwamba namsarandia rafikie ndipo aliponitonya kwamba mwenzie anaugua.(ameathirika)ana ukimwi anatumia dozi kikamilifu. Sikuamini maskio yangu na bado siamini macho yangu, mdada alivyoumbika hakika kakamilika, iweje aishi na mdudu?
Bado najiuliza ila ndio hivyo tena "anao, anao, anao" Jamani nawasihi wanaume wenzangu tunapokwenda kwenye miji ya watu ama tunapokutana na watu tusiowajua na kuwahitaji kwa kufanya nao mapenzi tujipe muda kwanza ili kuwachunguza vinginevyo tuwe tayari kufa kimas'hara. (Muwe na usiku mwema wakuu)
Sikua na jinsi zaidi ya kujipendekeza, kwa haraka tukawa marafiki ila hakuwa tayari tuwe mwili mmoja, kwanini!?hakunambia na sikuweza kufikiri wala kuhisi kwamba anatat, nilidhani ni mbwembwe tu za usistaduu mpaka siku mmoja wa shoga zake alipotambua nyendo zangu kwamba namsarandia rafikie ndipo aliponitonya kwamba mwenzie anaugua.(ameathirika)ana ukimwi anatumia dozi kikamilifu. Sikuamini maskio yangu na bado siamini macho yangu, mdada alivyoumbika hakika kakamilika, iweje aishi na mdudu?
Bado najiuliza ila ndio hivyo tena "anao, anao, anao" Jamani nawasihi wanaume wenzangu tunapokwenda kwenye miji ya watu ama tunapokutana na watu tusiowajua na kuwahitaji kwa kufanya nao mapenzi tujipe muda kwanza ili kuwachunguza vinginevyo tuwe tayari kufa kimas'hara. (Muwe na usiku mwema wakuu)