Shayu
Platinum Member
- May 24, 2011
- 608
- 1,657
Muda unakimbia. Maisha yetu hapa duniani yanaishia taratibu. Nashangaa nilikuwa mtoto sasa ni kijana. Natambua ujana huu ambao ni mzuri hautaendelea kukaa na mimi. Nina nguvu na sura nzuri lakini vitu vyote hivi vitapita. Wakati uzee utakapo nijia. Siwezi kuukimbia uzee utanichukua tu. Wakati huo miguu yangu haitofanya kazi vizuri. macho yangu hayataona. Mikono yangu ikitetemeka. Viungo vyote vya mwili wa binadamu vilivyokuwa vikifanya kazi havitafanya kazi tena katika nguvu ileile. Na simama na kufikiria ni nini maana ya maisha haya yanayopita kama upepo?
Natembea mitaani mjini posta naona wasichana wenye maumbo na sura nzuri. Kama maua uzuri wa mwanamke hautakaa milele ndani yake. Ni kitu kinachopita kama upepo. Utafika wakati wasichana vijana wote watakuwa wazee kitu kitachobaki ndani yao tu ni kumbukumbu ya uzuri waliokuwa nao.
Ujana ni mzuri lakini tuwe makini usitupoteze. Ukiutumia ujana vizuri uzee utaukumbuka kwa kumbukumbu ni za ujana.
Basi moyo wako usijawe na uovu. Jaza moyo wako kwa wema na uzuri wa mungu yeye apambaye maua na ndege wanaovutia. Kumbukeni maisha yanapita kwa kasi mno. Na huko tuendako hatukujui na wala tulikotoka hatu fahamu wote tumejikuta hapa duniani na tuwe na amani basi na tupendane.
Binadamu alipoumbwa na mungu alitafuta kiumbe kitakachoendana na mwanaume lakini alikosa miongoni mwa wanyama wote wa duniani. Ndipo mungu akampa usingizi mzito mwanadamu akamtoa ubavu wake na kumuumba mwanamke ili awe mwambata wake. Mtu ambaye atakaye ambatana nae na kuendana nae. Ndio maana katika dunia yote tuna watu wa aina mbili mwanamke na mwanaume. Watu hawa lazima waendane na wapendane na ni lazima kuwe na utaratibu ndio maana kukawa na ndoa sio tu kuparamiana kama mbuzi. Basi msichana atamuacha baba yake na mama yake na kumfuta mume wake hawa wawili watakuwa mwili mmoja. Ni lazima kuwe na muunganiko wa kihisia, kiakili, kiroho na kimwili. Love is more than lust. Love live longer, love endure and penetrate all things. But Lust destroy the hearts of men.
Natembea mitaani mjini posta naona wasichana wenye maumbo na sura nzuri. Kama maua uzuri wa mwanamke hautakaa milele ndani yake. Ni kitu kinachopita kama upepo. Utafika wakati wasichana vijana wote watakuwa wazee kitu kitachobaki ndani yao tu ni kumbukumbu ya uzuri waliokuwa nao.
Ujana ni mzuri lakini tuwe makini usitupoteze. Ukiutumia ujana vizuri uzee utaukumbuka kwa kumbukumbu ni za ujana.
Basi moyo wako usijawe na uovu. Jaza moyo wako kwa wema na uzuri wa mungu yeye apambaye maua na ndege wanaovutia. Kumbukeni maisha yanapita kwa kasi mno. Na huko tuendako hatukujui na wala tulikotoka hatu fahamu wote tumejikuta hapa duniani na tuwe na amani basi na tupendane.
Binadamu alipoumbwa na mungu alitafuta kiumbe kitakachoendana na mwanaume lakini alikosa miongoni mwa wanyama wote wa duniani. Ndipo mungu akampa usingizi mzito mwanadamu akamtoa ubavu wake na kumuumba mwanamke ili awe mwambata wake. Mtu ambaye atakaye ambatana nae na kuendana nae. Ndio maana katika dunia yote tuna watu wa aina mbili mwanamke na mwanaume. Watu hawa lazima waendane na wapendane na ni lazima kuwe na utaratibu ndio maana kukawa na ndoa sio tu kuparamiana kama mbuzi. Basi msichana atamuacha baba yake na mama yake na kumfuta mume wake hawa wawili watakuwa mwili mmoja. Ni lazima kuwe na muunganiko wa kihisia, kiakili, kiroho na kimwili. Love is more than lust. Love live longer, love endure and penetrate all things. But Lust destroy the hearts of men.