Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,899
- 944
UZINDUZI WA MRADI WA UMEME VIJIJINI JIMBO LA PERAMIHO
Mbunge wa Jimbo la Peramiho ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. JENISTA J. MHAGAMA ameendelea na Ziara Katika Kata ya Parangu Kijiji Cha Litowa.
Mhe. Jenista Mhagama Katika Ziara Jimboni Peramiho ameambatana na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi ngazi ya Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea pamoja na Wakuu wa Idara.
Pia, Mhe. Jenista Mhagama ameshiriki Misa ya Kumuombea Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. SAMIA SULUHU HASSAN, Mhe: Mbunge wa Jimbo la Peramiho na Waheshimiwa Madiwani.
Mhe. Jenista Mhagama Amezindua Mradi wa Umeme na Kuweka Nguzo Katika Msikiti wa Litowa, Ametoa Misahafu Sana (7) na Kanzu kwa Shekhe wa Msikiti wa Litowa, Amegawa Wheel Chairs Saba (7) na Mashuka, Mablanketi, Vifaa vya Kujifungulia Akina Mama pamoja na Nguo za Watoto Wachanga, Amegawa Vifaa vya Michezo (Jezi na Mipira) Kwa Timu Za Mpira Tatu za Kijiji Cha Litowa.
Jimbo la Peramiho lipo Imara na Kazi Inaendelea,,
Mama Yupo Kazini
Attachments
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.56.jpeg103.1 KB · Views: 4
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.55.jpeg105.1 KB · Views: 5
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.54(1).jpeg88 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.50(2).jpeg68.8 KB · Views: 4
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.50(1).jpeg109.2 KB · Views: 5
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.43.jpeg112.8 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.44.jpeg97.4 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-07-12 at 07.49.52(1).jpeg109.5 KB · Views: 2