Umati ni mkubwa sana. Kijani na Njano kila mahali mpaka wasanii na wao wamevaa. Vuvuzela kwa fujo.
Ndiyo ni mkubwa sana. Lakini kazi kubwa imefanyika kuwapeleka pale. Majira ya saa 4 asubuhi nilikuwa natoka Magomeni kwenda Chang'ombe, nilikutana na zaidi ya mabasi 8 hivi yakiwa yamejaza wafuasi wa CCM wakielekea kule. Sasa hapo sijui barabara zingine kuu kama vile Morogoro Rd etc.
Unavyoona wewe ni bendi gani ya mziki itashinda.Banana Zoro / B band amemaliza kutumbuiza. Amemodify kidogo wimbo wake wa Zomba kuinadi CCM