figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Uzinduzi wa Kitabu cha Dkt.Reginald Abraham Mengi unafanyika katika hoteli ya Serena Dar es Salaam.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli ndiye mgeni rasmi.
Je, atachomeka sababu za kufanya mabadiliko madogo?
====
UPDATES:
=> Tayari rais ameshawasili na inaoneshwa live ITV.
=> Kwa sasa aliyekuwa anaongea ni Prof. Mkandala. Wapo watu wengi wanaongelea review za kitabu hiki. Akiwemo Makonda, Mwapachu. Etc.
=> Paul Makonda anasema alimfahamu Mengi alipokuwa anasoma chuo cha Ushiriki Moshi. Mzee mengi ndo amenisaidia kimasomo hadi hapa nlipo.
Mwapachu anasema:
=> Tumekuwa marafiki mimi na Mengi tangu miaka ya 80, hiki kitabu cha Ican, I must, I will kinanikumbusha mbali sana kipindi tulipoonana. Huu uamuzi wake wa kuandika kitabu. Ameaandika historia ya mafanikio yake, ameandika kuhusu kutumia utajiri kuwasaidia wenzetu.
Rais Mstaafu Mwinyi sasa ndiye anaongea.
=> Anaanza kwa mumshukuru Mengi kwa kumualika kwenye uzinduzi. Anasema hakualikwa kuongea lakini anayo hamu kubwa ya kusema machache ya pongezi.
Kwa kuandika kitabu kuhusu Maisha yake na kufika kilele, amefanya jambo ambalo si Waafrika wengi wanaoamua kiandika. Ipo fikra kwamba watu wenye uwezo wa uwaandishi ni watu wa taaluma na wasomi. Dr. Mengi kavunja mwiko huo, tumpongeze kwa hayo.
Hata rais kukubali kuzindua hiki kitabu ni kudhihilisha anathamini uandishi wa dr. Mengi.
Matumaini yangu ni kwamba kitabu kitakachozinduliwa leo itakuwa ni chachu na msukumo kwa watu wenye mafanikio kuandika vitabi vyao. Asia, Ulaya na Marekani watu Maarufu wameandika vitabu na vinatumika katika vyuo. Kwa kuzungumzia uongozi wao..
Nashukuru tena kwa kualikwa. Kamaliza.
Sasa Dr. Mengi anaongea
Anatoa zawadi kwa washindi wazo/ ubunifu mzuri la biashara alililiendesha twitter. Washindi ni Wakota Kapunda kutoka Tanzania na Bryan Mwenda kutoka kenya. Kila mmoja amepewa zawadi ya Dola elfu 20.
Huyu mtoto wa Konta, anaandika kwa ulimi. Anaandika kwa kutumia ulimi na ameweza.
Watu wananiuliza kwanini naandika kitabu?
Mimi nlikuwa na mtoto wangu, kabla ya kufariki aliniomba uandike kitabu. Hivyo nmetimiza ahadi yangu kwa Mwanangu.
Aliniomba pia niende mazoezi kila siku, kuanzia leo nitatimiza.
Watu wanauliza nini kilikusukuma?
Mimi nlizaliwa familia masikini. Nyumba ya nyasi na Udongo. Nlipokuwa nikasema naweza kuondoka kwenye umasikini na nimeweza kweli. Wengi wamezaliwa kwenye umasikini kama mimi. Ukisema unaweza unaweza kweli.
Mtu wa kwanza kunifundisha ongezeko la thamani ni mama. Alikuwa anauza ulezi. Alikuwa akinunua ulezi na kuuloweka unaongezeka uzito.
Baba alikua ananunua mbuzi waliokonda akifika nyumbani anawaosha na kuwapa maji matumbo yanakuwa makubwa ndo anawauza. Mtasema sijui nini alkini hayo mambo ya kisasa hayakuwepo
Kaka yangu alikuwa anasafisha viatu vya wanajeshi. Akapata hela akafungua duka likajua akanunua gati na kuwa anaenda Mombasa.
Kwenye biashara unatakiwa uwe muaminifu. Ukisema nakupa pesa yako kesho iwe kesho kweli. Huyu kaka alinifundisha makubwa.
Watu wanauliza. Mengi unawasaidia watu hutafilisika?
Nawajibu hata nikiishi miaka mia sitafilisika. Sababu kila kitu napewa na mwenyezi Mungu. Siogopi. Mama ndo alinofindisha kutoa. Zamani masikini walikuwa wanachemsha mawe ili watoto wakija wadhani kuna chakula. Mama alikuwa anatowa chakula kwa watoto masikini kuliko sisi.
Rais Magufuli aliniambia nifanye lolote la kibiashara kwa kifuata sheria. Sasa najenga. Mwinyi alinipa nishani hadi leo sijajua ni ya nini. Ila ntamuuliza siku nyingine. Wapo watu wengi wamenisaidia katika maisha yangu. Nawashukuru wote
Yote haya ni kuwatia moyo vijana kwamba wanaweza. Asante
Rais John Magufuli anaongea.
Anaanza kwa kutoa salamu na itifaki imezingatiwa.
Napenda niungane na wote kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyefanikisha mkusanyiko huu, pia nashukuru Mzee Mengi kwa kunialika
Nmekuja pamoja na mambo mengine wewe ni mlipa kodi mzuri. Asante sana.
Nmefurahi kuona watu kutoka kada mbalimbali akiwemo mzee mwinyi. Hii inaonesha kuwa mzee mengi ni mtu wa watu mwenye upendo.
Kama tujuavyo, tupo hapa kuzinfua kutabu kilichoandikwa na Mengi. Sote tunamfahamu ni msomi mzuri wa uhasibu na ni mzalendo. Kupitia biashara zake ametoa mchango kwa taifa letu. Ikiwemo ajira na ameshika nafasi mbalimbali.
Msukumo wa maisha yake, ulimfanya aandike kitabu. Sijapata fursa ya kukisoma lakini kama tulivyosikia, ameelizea kuhusu mama, baba. Nlianza kuwaza lazima ulezinuuzwe siku hiyo, ungekaa siku tatu ungeota..
Ameeleza mahangaiko aliyoyapitia na jitihada ilizozifanya. Ni historia ya kusisimua.
Mafunzo nliyoyapata kwenye hiki kitabu;
1. Sisi watanzania tukiamua tunaweza. Mzee Mengi aliukataa umasikini akfanikiwa. Na sisi Watanzania tukikataa umasikini tutafanikiwa. Huwa nawaambia tukijiamini tunaweza, tuache kukatishana tamaa. Nafahamu, Wapo watu walipata kuzungumza kwamba watanzania hawawezi kufanya biashara ya gesi, madini nk. Hii ni kukatishana tamaa. Watanzania tujiamini
Kabla sijaingia madarakani, nlijua kabisa ukishakuwa rais huwezi katishwa tamaa na mtu yoyote kwakuwa wewe ni rais. Haikuwa hivyo, nlivyoingia tu nliyaona.
Tulipotaka kutoa elimu bure tuliambiwa hili haliwezekani. Eti hadi ulaya elimu ni ya kulipia, lakini tulipojaribi kwa kutoa bil 23 kila mwezi tumefanikiwa. Wanafunzi waliongezeka.
Tukasema tuanze kujenga reli ili kufanya biashara na bandari ya dar itumike vizuri. Reli ya sasa inabeba tani 7 tukataka yenye kubeba hadi tani 38. Wakasema siwezi reli imewashinda wengi. Imejengwa miaka 112 iliyopita kwahiyo ni kitu hakiwezekani. Wenye mikopo kutukopesha wakakataa. Sisi tukaamua kujenga. Lakini kukatisha tamaa kupo na hao tunao wajengea ndo walianza kukatisha tamaa. Hela zipo za kujenga hata wakandarasi wakimaliza leo tunawalipa. We can.
Sisi tunazungumzia watalii mil1, misri wanazungumzia mil 10.
Shirika la ndege lilikuwa limepotea angani. Sifahamu rais Mwinyi alikuta ndege ngapi. Mimi nliingia hakuna ndege. Tanzania tuna vivutio vya utalii, watu watavifikiaje bila kuwa na ndege?
Kwa hili namshukuru sana rais Kagame, aliniambia fanya, sisi Rwanda tumeshaanza. Ukitaka kununua kwa bei ya chini waite mashirika ya ndege kwa wakati mmoja. Sasa tumenunua ndege saba.
2. Nmejifunza ili ufanikiwe lazima uchape kazi kwa bidii.
Mzee mengi baada ya kusoma hukuishia hapo, ukichapa kazi kwa bidii. Nawasihi watanzania wqchape kazi kwa bidii. Ndo maana huwa nawambia watanzania hapa kazi tu. Ukishasema I MUST lazima ufanye.
3. Tumejifunza changamoto hazikosekani.
Mzee mengi umeelezea changamoto ulizokutana nazo. Wapo waliokuunga mkono na wapo waliokukatisha tamaa wapo. Ukitaka kujenga bwawa la umeme kuongeza umeme nchi wapo wanaozungumza tunakata moti tunaharibu mazingira. Sisi tunachukua sehemu ndogo ya asilimia 3 ya eneo lote la stiegler's gorge.
Unakuta mtanzania ambaye hajui anataka kutukwamisha. Unakuta anasema tumuenzi nyerere. Nyerere na stiegler's gorge vinaenda pamoja.
Nakupongeza Mengi. Na kitabu chako kiwe fundisho kwa watanzania wote.
Haya nliyoyataja ni mambo machache kati ya mengi yaliyomo humu.
Nashukuru mzee Mengi kwa kuweza kuandika kitabu hiki.
Nakuomba mzee mengi uangalie uwezekano wa kuandika kitabu hiki kwa kiswahili ili watanzania wengi waweze kukisoma. Kitawasaidia sna.
Nawasihi sana watanzania kununua kitabu hiki cha mzee mengi. Tujenge utamaduni wa kununua na kusoma vitabu. Kuna hazina kubwa kwenye usomaji wa kitabu.
Naomba wanasiasa wachumi wafanyabiashara kuiga mfano wa mzee Mengi katika kuandika viatbu.
Nimemuona hapa Prof. Akizungumzia hiki kitabu cha Mengi. Huyu prof. Mkandala sina uhakika kama ameandika kitabu chake pamoja na nafasi aliyokuwa nayo. Sijakiona.
Mengi alinipigia simu wakati tupo kwenye uchaguzi wakati nmeshateuliwa na chama changu kugombea. Akanambia mheshimiwa nataka nikuone. Nikamwambia nipo mbali tulikuwa tunatoka Iringa tunaenda Dodoma. Akasema nataka nikupe mchango wangu kwani huna chochote. Nikakataa. Akaniuliza kwanini? Nikasema sitaki nije nlipishwe. Aliponipigia alinipigia tena nikamwambia nitakuja nikija dar. Lakini sijamuona hadi leo. Yupo hapa. Nataka kusema mzee Mengi ana huruma. Nakushukuru kwa moyo wako wa upendo. Unaendelea kuuonesha hadi kwa walemavu. Jina lako litakumbukwa daima kwa watanzania.
Huyu binti aliyepata zawadi mimi nlimsoma kwenye historia. Aligongwa. Hanauwezo wa kuandika lakini aliweza kuandika hicho anachokifikiria kwa kutumia ulimi. Mimi pia ntamchangia kidogo angalau mil 10 iweze kumsaidia.
Kitabu cha mzee mengi kiwe fundisho kwetu sote.
Natoa wito kwa jumuia ya wafanya biashara. Msisikilize maneno ya watu wanaowakatisha tamaa. Hakuna serikali inaweza kuendelea bila kutegemea tasisi binafsi. Jukumu la Serikali ni kukusanya kodi basi. Ukiwa na taasisi nyingi utakusanya kodi nyingi nakutengeneza ajira. Fanyankazi zako usikwepe kodi.
Nataka wafanya biashara wafanyebkazi zao free.
Nawaomba waheshimiwa mabalozi walete wawekezaji kutoka nchi zenu. Tanzania ni tajiri. Tuna madini na kila kitu
Serikali ninahoiongoza itaendelea kushirikiana na wafanyabiashara kama Mengi.
Amemaliza. Sasa anazindua kitabu na kupiga picha za kumbukumbu.
=======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 02 Juni 2018, amezindua kitabu chenye historia ya maisha ya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Abraham Mengi kinachoitwa I CAN, I MUST I WILL jijini Dar es salaam.
Mhe. Rais Dkt. Magufuli amewataka wafanyabiashara nchini kuiga mfano wa Dkt Mengi na kupuuza maneno ya baadhi ya watu wanaowakatisha tamaa kwani hakuna serikali yoyote duniani iliyopata maendeleo bila ya kushirikiana na sekta binafsi.
Amesema hata Serikali imekuwa ikikatishwa tamaa katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kama vile ujenzi wa Reli ya Kisasa, Utoaji elimu bila malipo, Ununuzi wa ndege mpya saba na ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa Stiglers Gorge na mingine mingi.
Pamoja na kukatishwa tamaa huko na baadhi ya watu wasioitakia nchi maendeleo Serikali haikukata tamaa na imekuwa ikiendelea na utekelezaji wa miradi yake kwa lengo la kuwaletea watanzania maendeleo.
‘’Ninachotaka kuwaambia Wafanyabiashara wa Tanzania na watanzania kwa ujumla ni kuwa kitabu cha Mzee Mengi kiwe fundisho kwetu sote tunaweza kwelikweli,na mimi napenda nitoe wito kwa wafanyabiashara wote nchini ninarudia wito wangu msisikilize maneno ya watu wanaowakatisha tamaa fanyeni biashara zenu kwelikweli, wekeni uwekezaji wenu wote hakuna serikali inayoweza kuendelea bila kutegemea sekta binafsi’’ amesema Rais Magufuli.
Rais Magufuli amsema watanzania wakiamua wanaweza kwani Dkt. Mengi alizaliwa katika familia masikini lakini kwa kuwa aliukataa umasikini ameweza kufikia maendeleo aliyonayo hivi sasa na hivyo kuwataka watanzania wote kujiamini na kuukataa umasikini kwani tunaweza.
Aidha Rais Magufuli amewataka Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini kuwahamasisha wafanyabiashara katika nchi zao kuja kuwekeza hapa nchini kwani Tanzania ni sehemu salama kwa uwekezaji.
Amesema katika historia ya mzee Mengi yapo mengi amekutana nayo ya kumkatisha tamaa lakini yeye hakukata tamaa bali aliamini anaweza na akaamua kufanya na akaweza hivyo watanzania tuache kukatishana tamaa ili tuweze kufikia mafanikio ya kweli.
Dkt. Magufuli amesema Dkt. Reginald Mengi ni mfanyabiashara wa kuigwa hapa nchini kutokana na jitihada zake mbalimbali katika mchango wa Taifa kwa kuwa chanzo cha ajira kwa watanzania na kulipa kodi kwa serikali inayokwenda kutoa huduma mbalimbali kwa watanzania wote.
Kwa upande wake Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi amempongeza Dkt. Mengi kwa uamuzi wa kuandika historia ya maisha yake na kuonyesha hatua mbalimbali alizopitia hadi kufikia mafanikio aliyonayo kwani ni watu wachache wanaoweza kufanya kitu kama hicho hasa kwa Afrika.
Amesema ipo fikra kwamba watu wenye uwezo wa uandishi ni wale wenye taaluma na wasomi katika vyuo mbalimbali lakini Dkt. Mengi amevunja dhana hiyo na kuweza kuandika kitabu hicho.
Nae Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi amemshukuru Rais Dkt. John Pombne Magufuli kwa kukubali kumzindulia kitabu hicho na kuwataka watanzania kutokata tamaa katika kufikia hatua ya maendeleo kwani alichoandika yeye ni uhalisia wa maisha yake tangu akiwa masikini hadi kufikia mafanikio aliyonayo.
Dkt. Mengi amepata msukumo wa kuandika kitabu hicho cha historia ya maisha yake ili kutimiza azma ya marehemu mtoto wake Rodney Mutie Mengi aliyemtaka kuandika kitabu hicho na mambo mengine ambayo atayatimiza kadri awezavyo.
Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
02 Julai, 2018