Uzi wa kutoa pongezi na kutambua mchango wa wafanyakazi wa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kwenye kutoa huduma nzuri

HS CODE

JF-Expert Member
Jul 5, 2019
1,779
4,330
Iwe ni serikalini au taasisi binafsi wapo wafanyakazi wanaotekeleza majukumu yao kwa ufanisi wa hali ya juu sana. Ukikutana nao, watakuhudumia vizuri mpaka utamani wengine wote wangekuwa kama wao. Hawa watu wanahitaji kufahamishwa kwamba ubora wa wanachokifanya tunautambua, ili wapate nguvu ya kututumikia kwa wema zaidi. Soma hii mifano miwili:

Wakwanza
Siku moja nilikuta mzozo mkubwa maeneo ya kivukoni kutoka upande wa Kigamboni, kwenda Magogoni. Kusikiliza kwa makini, nikabaini kuna jamaa aliahidiana na mwenzake kuvuka pamoja, hivyo alipofika eneo la kukata tiketi akakata mbili, yakwake na ya mwenzie. Bahati mbaya huyo mwingine akapata dharura iliyopelekea kutokuvuka.

Ikabidi aliyekata tiketi atafute mtu atakayeinunua moja ili na yeye abaki na nyingine. Shida ni abiria hawakuonyesha kumuamini na wakawa wanakata zakwao mpya dirishani. Jamaa akaona isiwe kesi, akaenda sehemu ya kuskani, akapitisha moja kisha ile isiyoskaniwa akaitia mfukoni huku anakimbia kuingia kwenye pantoni lisimuache. Ghafla wasimamizi wakamuita kwa makelele sana, kufika mahojiano yao yalikuwa hivi:

Msimamizi: Sasa kwanini unatia tiketi mfukoni badala ya kupitisha zote kwenye mashine? (Aliuliza kwa ukali sana).

Abiria: Ni kweli nimeskani moja kwa kuwa navuka mimi mtu mmoja, nyingine bado haijatumika, japo sina mpango wa kurudi kuitumia sijaona ulazima wa kuiskani (Alijibu kwa upole).

Msimamizi: Kuskani tiketi sio maamuzi binafsi, ni sehemu ya utaratibu. Tiketi zote zinazotolewa ni lazima ziskaniwe na sio vinginevyo (Jamaa ndio kwanza akazidi kupandisha sauti).

Abiria: Inawezekana ni kweli uko sahihi, lakini humu kwenye hii tiketi kuna hela yangu ambayo ni haki yangu itakayoisha endapo tu nikiitumia. Hata hivyo pamoja na kuwepo mashine, mbona kuna baadhi yenu mnapokea tiketi mkononi na kuzichana badala ya kulazimisha ziskaniwe? Utofauti uko wapi kati ya hii ninayopita nayo na hizo mnazozichana bila ya kupitishwa kwenye mashine. Au kama itafaa naomba mnirudishie pesa yangu niwaachie tiketi yenu (Abiria akaona unyonge utamkosti, nayeye akawaka, japo hakufikia kwa wasimamizi waliokuwa wanamchangia).

Msimamizi: Maafandeeeeee huyu abiria analeta vurugu njooni mumchukue, akafundishwe adabu.

Basi jamaa wa Suma JKT wakamiminika kwa kasi ya ajabu, hawakutaka kuuliza kitu, hawa jamaa huwa wanajiona ni makomandoo wenye mafunzo ya hali ya juu sana, kumbe hamna kitu. Wakampiga mikwara mingi abiria huku wameshaanza kumkanda makofi ya hapa na pale kadiri walivyoona ina swihi.

Ndipo ghafla akatokea kamanda mmoja wa FFU huwa anamikwara mingi ya kimuonekano, anavaaga kama yuko vitani huku amepiga miwani nyeusi, umri wake umesogea kidogo. Nadhani wengi wanaotumia ile njia wanamfahamu. Ndugu zangu, ule usemi wa sura sio roho ni wa kweli, yule afande alipoelezewa ile shida, akawaambia wale JKT, nyie ni wapumbavu sana. Mnamchelewesha raia kwenye majukumu yake kwa sababu ya hovyo kabisa. Kisha akaingiza mkono mfukoni na kutoa Tzs 200/= akamuamsha jamaa chini alipokuwa amekalishwa kwa mabavu, na kumuomba amuuzie hiyo tiketi.

Kama hiyo haitoshi pantoni lilikuwa limeshaanza kuondoka akamuombea kwa nahodha kupitia zile redio zao asubiriwe, na kweli jamaa akaliwahi na kuvuka upande wa pili. Nadhani unaweza kuona namna kuna watu wana ubinadamu wa hali ya juu.

Wapili
Miaka ya nyuma nilikuwa nafanya kazi ya mkataba wa muda mfupi na NGO fulani ya kimataifa. Ilitokea jukumu linalohitaji kufanya tafiti fulani fulani. Nikapewa maelekezo ya kwenda Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) nikakutane na Dkt. Godwin Kaganda ambaye kwa sasa nilisikia yuko Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMU).

Basi kufika ofisini kwake nikapokelewa na sekretari wake, ni mdada fulani anavaa kiheshima, lugha na muonekano vyote vizuri. Alinikaribisha kwa ukarimu na uchangamfu wa hali ya juu. Nilipomuelezea shida yangu, akanijibu kwa upole kwamba kwa sasa Dokta ametoka kidogo, kama muda unaniruhusu nimsubiri. Yule dada akaniuliza kama natumia kahawa, nikamjibu ndio, akaniwekea huku tunabadilishana mawazo kusogeza muda. Kwa kuwa hana uhakika atarudi muda gani, na nimeshakaa muda mrefu akashauri nimuachie mawasiliano yangu na baadhi ya nyaraka chache kisha nivute subira, atanipigia kunijulisha ni kipi kitawezekana.

Kweli, mchana akanipigia niende, nikakutana na Dokta tukamalizana, nilipokuwa natoka, akaniambia ameona kwenye fomu zangu kuna wengine natakiwa kuonana nao, kwa hao kuwapata watanizungusha sana. Aisee, huwezi amini, alitoa simu na kumpigia mmoja baada ya mwingine, kuwauliza kama wako ofisini kisha akanitambulisha kwamba mimi ni ndugu yake nina suala langu anawaomba wanisaidie lifanikiwe mapema. Dah, wakuu hii kitu ilinigusa sana, mpaka nikajiapiza na mimi popote nitakapokuwa na nafasi ya kuhudumia watu, nitakuwa mwema hata kwa nisiowajua. Na ni kweli, hiyo imekuwa ni moja ya sera zangu za maisha.

Hao ni wachache miongoni mwa wengi waliopewa dhamana ya kutoa huduma na wanafanya kazi zao vizuri sana. Tuwapeni moyo hawa watu. Wewe ni nani ulikutana naye akakuvutia namna ya utekelezaji wake wa majukumu?

Kwa upande wa mazuri kama unamfahamu kwa jina mtaje na ofisi yake, hata kama jina hulikumbuki vizuri au hutaki kulitaja, muelezee kwa namna watu wamtambue, iwe ni tukio lilitokea kipindi kilichopita au hata siku za karibuni, usiache kutupa kisa angalau kwa ufupi tupate cha kujifunza.

Endapo pia kuna mahala hukuhudumiwa vizuri sio vibaya ukaizungumzia kwa maelezo yenye stara bila kulenga kumchafua mtu wala kumdhalilisha, itakayotosha kumfanya muhusika kujijua na kujirekebisha, upande huu naomba tusitaje majina moja kwa moja.

Asante.
 
Kuna ka dada keupe Kasulu -Polisi kalikuwa na nyota moja mwaka 2018 aise kanaongea kwa ukarimu utadhani unaulizia huduma kwenye hoteli ya kitalii.
 
Miezi kadhaa iliyopita nilienda polisi kuchukua loss report nilipoteza ID yangu ya NSSF. Kufika nikaambiwa mhasibu hajafika, nikasubiri karibia masaa mawili ndio akaja, ni kadada fulani keupe.

Kuingia ofisini akaniambia toka nje subiri nitakuita, nikasubiri naona muda unaenda haniiti nikaingia kibabe. Nakuta anachat nikamwambia sista mwajiri anahitaji nipeleke copy ya kitambulisho kuna uhakiki wa wanachama naomba nisaidie. Akaniandikia pale akaniambia nikalipie nimeenda nikalipia kwa wakala, kurudi ananipa form nikatoe copy, nikatukana kimoyo moyo. Ina maana angenipa hiyo form niende wakati wakulipa ingekuwaje? Halafu copy tu jeshi letu la police linashindwa kutupa wateja wao?

Nimerudi pale yule dada kujaza ile form hajazi akanipark tena nje, nikamfata nikamchana dada leo upo ofisini kwako ila hujui utakuja kunikuta wapi. Dada akawaka akaanza niambia nimelewa wakati sikuwa nimekunywa. Nikamwambia wewe ni mtumishi wa umma nihudumie sijaja kuomba msaada. Akaijaza haraka akanipa nikaondoka pale nimewaacha wananishangaa nilivyokuwa najiamini.

Yule dada siku nikija kukutana nae kitaa nitamtongoza halafu nitakuja kumkumbusha.
 
Vp mtandao, umeme una nunulika leo


Ova
Picha linaanza tu umeme umekatika..

PXL_20220912_184851698.NIGHT.jpg
 
Miezi kadhaa iliyopita nilienda polisi kuchukua loss report nilipoteza ID yangu ya NSSF. Kufika nikaambiwa mhasibu hajafika, nikasubiri karibia masaa mawili ndio akaja, ni kadada fulani keupe.

Kuingia ofisini akaniambia toka nje subiri nitakuita, nikasubiri naona muda unaenda haniiti nikaingia kibabe. Nakuta anachat nikamwambia sista mwajiri anahitaji nipeleke copy ya kitambulisho kuna uhakiki wa wanachama naomba nisaidie. Akaniandikia pale akaniambia nikalipie nimeenda nikalipia kwa wakala, kurudi ananipa form nikatoe copy, nikatukana kimoyo moyo. Ina maana angenipa hiyo form niende wakati wakulipa ingekuwaje? Halafu copy tu jeshi letu la police linashindwa kutupa wateja wao?

Nimerudi pale yule dada kujaza ile form hajazi akanipark tena nje, nikamfata nikamchana dada leo upo ofisini kwako ila hujui utakuja kunikuta wapi. Dada akawaka akaanza niambia nimelewa wakati sikuwa nimekunywa. Nikamwambia wewe ni mtumishi wa umma nihudumie sijaja kuomba msaada. Akaijaza haraka akanipa nikaondoka pale nimewaacha wananishangaa nilivyokuwa najiamini.

Yule dada siku nikija kukutana nae kitaa nitamtongoza halafu nitakuja kumkumbusha.
Huko ndio zero kabisa..
 
costomer care wa tume ya utumish wale n moja ya watumish wa hovyo sana hawana kaul nzur hata kidogo utapga cm utafkir unawadai hwapokei hata cku mbil sku wakipokea unasikia eeh mghh ndio karbu badoo tunashughulikia anakata cm
 
Kipindi fulani nilifiwa na mama mzazi, wakati wa kufatilia mirathi nikaenda alipokuwa ameajiriwa ili kuanza mchakato.
Nikafika ofisi za masijala, asee alikuja dada mmoja kunisikiliza aliichukua ishu yangu kama yake. Alipambana huku na huko mpaka alijua faili lilipo. Imagine lilikuwa linatembezwa ofisi kadhaa lakini alienda akiuilizia mpaka akalipata.
Baada ya hapo akanipa namba ili nisiwe na haja ya kwenda pale mara kwa mara niwe napiga simu tu.
Ni kweli nikawa nikipiga simu anapokea na anaenda kufatilia kwa niaba yangu.
Mpaka nikapata na haki nyingine za mama ambazo sikuwa najua kuwa anatakiwa kuzipata.
Dada yule wa kihaya MUNGU ambariki sana pale Manispaa ya Ilala.

Mpana leo na nimejifunza kumuhudumia yeyote kwenye jambo lililo ndani ya uwezo wangu.
 
Kuna ka dada keupe Kasulu -Polisi kalikuwa na nyota moja mwaka 2018 aise kanaongea kwa ukarimu utadhani unaulizia huduma kwenye hoteli ya kitalii.

Watu wa aina hii ni adimu sana, hongera kwake. Naamini na kuna wengine humu wanamjua huyo dada.
 
Miezi kadhaa iliyopita nilienda polisi kuchukua loss report nilipoteza ID yangu ya NSSF. Kufika nikaambiwa mhasibu hajafika, nikasubiri karibia masaa mawili ndio akaja, ni kadada fulani keupe.

Kuingia ofisini akaniambia toka nje subiri nitakuita, nikasubiri naona muda unaenda haniiti nikaingia kibabe. Nakuta anachat nikamwambia sista mwajiri anahitaji nipeleke copy ya kitambulisho kuna uhakiki wa wanachama naomba nisaidie. Akaniandikia pale akaniambia nikalipie nimeenda nikalipia kwa wakala, kurudi ananipa form nikatoe copy, nikatukana kimoyo moyo. Ina maana angenipa hiyo form niende wakati wakulipa ingekuwaje? Halafu copy tu jeshi letu la police linashindwa kutupa wateja wao?

Nimerudi pale yule dada kujaza ile form hajazi akanipark tena nje, nikamfata nikamchana dada leo upo ofisini kwako ila hujui utakuja kunikuta wapi. Dada akawaka akaanza niambia nimelewa wakati sikuwa nimekunywa. Nikamwambia wewe ni mtumishi wa umma nihudumie sijaja kuomba msaada. Akaijaza haraka akanipa nikaondoka pale nimewaacha wananishangaa nilivyokuwa najiamini.

Yule dada siku nikija kukutana nae kitaa nitamtongoza halafu nitakuja kumkumbusha.

Duh! Mkuu, hii hali inaumiza sana. Mbaya zaidi unaweza jihisi kama vile unapewa msaada kumbe ni haki yako, na mara nyingine ni maeneo tunayolipia huduma ila ubora ni dhaifu sana.
 
costomer care wa tume ya utumish wale n moja ya watumish wa hovyo sana hawana kaul nzur hata kidogo utapga cm utafkir unawadai hwapokei hata cku mbil sku wakipokea unasikia eeh mghh ndio karbu badoo tunashughulikia anakata cm

Hahaha, dah Mkuu nimecheka sana ulivyomalizia. Umefanya niimalize siku vizuri sana.
 
Kipindi fulani nilifiwa na mama mzazi, wakati wa kufatilia mirathi nikaenda alipokuwa ameajiriwa ili kuanza mchakato.
Nikafika ofisi za masijala, asee alikuja dada mmoja kunisikiliza aliichukua ishu yangu kama yake. Alipambana huku na huko mpaka alijua faili lilipo. Imagine lilikuwa linatembezwa ofisi kadhaa lakini alienda akiuilizia mpaka akalipata.
Baada ya hapo akanipa namba ili nisiwe na haja ya kwenda pale mara kwa mara niwe napiga simu tu.
Ni kweli nikawa nikipiga simu anapokea na anaenda kufatilia kwa niaba yangu.
Mpaka nikapata na haki nyingine za mama ambazo sikuwa najua kuwa anatakiwa kuzipata.
Dada yule wa kihaya MUNGU ambariki sana pale Manispaa ya Ilala.

Mpana leo na nimejifunza kumuhudumia yeyote kwenye jambo lililo ndani ya uwezo wangu.

Dah! Mkuu japo muda umepita lakini pole kwa kuondokewa na Mama mzazi.

Ni kweli kabisa, kuna watu bila kujua huwa wanatufundisha kuwa wema kupitia matendo yao kwetu.
 
Duh! Mkuu, hii hali inaumiza sana. Mbaya zaidi unaweza jihisi kama vile unapewa msaada kumbe ni haki yako, na mara nyingine ni maeneo tunayolipia huduma ila ubora ni dhaifu sana.

Hahaha! Mkuu, naona umeamua uweke mambo kwa msisitizo wenye maneno machache sana.
 
Back
Top Bottom