Uzi maalum wa kuishauri serikali

Uzi maalum wa kuishauri serikali

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
361,071
Reaction score
831,695
Wanajamvi tumekuwa na nyuzi mbalimbali maalum, ambazo zimekuwa msaada mkubwa sana kwetu
Jamiiforums ni mtandao unaoheshimika sana, ni sehemu ya jamii(wapiga kura) ikiwa na mchanganyiko wa watu wa kaliba zote
Jamiiforums imekuwa chanzo muhimu cha habari kwa mitandao mingine na hata vyombo vya habari... Ni mtandao wenye mchango wa aina yake... Tunapaswa kuutumia vyema
Tumekuwa na mada zinazoibuka na kupotea zikiwa na lengo la kuishauri serikali kwenye mambo mbalimbali... Tuna wataalam wa kila aina humu na kuna wanajamvi walishawahi kuishauri serikali kupitia JF na ushauri wao ukafanyiwa kazi
Ndani ya Jamiiforums tuna watumishi wa serikali, wanasiasa na viongozi mbalimbali ambao haipiti siku bila kuperuzi JF ili kuona kuna kipi kipya ama jamii inasema nini kwenye jambo fulani
Kwa kuzingatia hayo yote ni muhimu sasa kuwa na huu UZI MAALUM wa kuishauri serikali yetu... Ushauri wako wowote hata kama hautafanyiwa kazi lakini utakuwa umetimiza jukumu lako kupitia maandishi kama Mtanzania mzalendo na mpiga kura, Kwahiyo usione uvivu wala kuvunjika moyo! Andika, maandishi hayafutiki na WANASOMA!

TIMIZA WAJIBU WAKO SASA....!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna kipindi barafu alitoa ushauri fulani kuhusiana na ndege na mambo ya anga! Ulikuwa ushauri wa kitaalam na uliojaa weledi! Ushauri ule ulifanyiwa kazi
Lakini kwa nyakati mbalimbali hapa JF kuna wajuzi wa ambo walishawahi kuishauri serikali kwenye sekta za madini kodi bandari elimu afya na hata uchawi na ushirikina na kwa sehemu ushauri wao ukazingatiwa na kufanyiwa kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja.
Naanza na hii serikali ianze kutatua changamoto za msingi za watanzania,vipaumbele vya watanzania ni kwanza mazingira mazuri ya biashara/ ajira ,afya,Elimu, bombadier muhimu lakini sio kwa sasa tutatue kwanza hizo changamoto.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tukiwa makini na weledi hii mada itakuwa jicho kionambali la serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie ushauri kwa serikali nauchukulia kama KUPANGIANA...mpaka kauli ya TUSIPANGIANE itakapofutwa nitatoa ushauri wangu.

Na kama hauamini nisemayo basi naanza na ushauri huu mwepesi tuu..SERIKALI IRUHUSU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA KAMA WAKATI WA JK NA MKUU AKUBALI KUWAITA WAPINZANI IKULU WANYWE NAYE CHAI AONE MAMBO YATAKAVYONYOOKA.

haipendezi laisi kuweka beef na watu wake hasa wanaotakiwa kumsaidia kuona nchi inapoenda mrama...UPINZANI SIO UADUI.

WAANZE NA HILO LISILOGHARIMU HATA MIA YA SERIKALI...MENGINE YAJA.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
Naomba serikali iweze tena kuangalia vyama vya ushirika ikiwemo Kilimanjaro Native Cooperative Union(KNCU) kwani vyama hivi vinaelekea kupotea kama siyo kufa.


Chama kinaendeshwa na wajanja. Mkulima hanufaiki, bei ya miche na dawa za kahawa hamna ruzuku na kama ipo inatolewa kibaguzi.


Wakulima wamekata tamaa hawaoni tena umuhimu wa kulima kahawa tena maana hata bei wajanja wanawanyonya sana wakulima huku wao wakinufaika kwa bei ya juu ukiangalia kahawa wanauza nje ya nchi kwa bei nzuri tuu.


Tafadhali Serikali naomba iweze kusikia kilio hiki, kuna wapuuzi wachache kwa tamaa zao wanataka kuona KNCU inakufa kabisa.
 
Ni kweli, maadam ni serikali sikivu na ya wanyonge, watu wote kwa mimi, ushauri wangu ningependa vitu vyote vinavyouzwa viwekewe bei elekezi kama ni kiberiti kiandikwe code zake na bei yake kama vocha,
Ili hata hao wanaopandisha vitu tupate kuwajoji..... Imekuwaje
Na kwa njia hii itakuwa rahisi kujua kitu harisi na bandia.
Mf. Mzuri bidhaa za nje huwekwa code na bei yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali hii sikivu kwa sasa iwaone watumishi, watumishi wamekuwa hawana amani kwa sasa maana hawajui nini hatma yao hasa wale waliostahili kupanda madaraja toka mwaka jana!!

Ukizungumzia haki za watumishi unaonekana mpiga kelele hasa walioko sekta binfsi au wafanyabiashara lakini ukweli ni kwamba athari ya mwaka mmoja inaweza kumuathiri mtumishi kwa muda wake wote wa ajira. Mfano mtu alistahili kupanda daraja toka mwaka jana na mkulu akasitisha, mbaya zaidi hata barua basi wakasitisha kuzitoa so hana barua ya kupanda daraja mkononi.

Je, watakapoanza kutoa hizo barua nae itadate mwaka jana au mwaka huu?? Tayari ile trend ya upandaji madaraja ishaathiriwa, kumbuka na mafao yanayoingia mfuko wa jamii kwa mwaka mzima sasa si stahiki yake. Vipi wakati wa kustaafu??

Hiyo moja, pili kuna wazee wamechanganyikiwa hata kazi hazifanyiki!! Mtu alikuwa apande daraja mwaka jana, mwaka huu anastaafu!! Au alijiendeleza akamaliza mwaka juzi ili mwaka jana aanze kutumikia cheti chake na mwaka huu anastaafu!! Kasitishiwa kupanda daraja kwa level ya elimu yake ya sasa na ndiyo anastaafu hivyoo, usumbufu wanaowaletea hawa watu jamani.

Sheria inasema utalipwa kwa mafao mapya ikiwa umekitumikia cheti chako cha kujiendeleza kwa muda usiopungua miezi sita. Ana mwaka sasa, anakwenda kustaafu mwezi wa tisa, mafao yake mfuko wa jamii kwa mwaka mzima yameathiriwa pia!! Anastaafu vipi huyu mtu!!

Nadhani wawaondolee watumishi matatizo yasiyo ya lazima sasa, hasa wanaposema serikali ya sasa haitaki madeni na wameshtengeneza madeni lukuki toka mwaka jana yaani nashindwa kuwaelewa!! Watalipa au ndo vile tena, ubabe ubabe
 
Nasahauri serikali ilime bangi ikauze marekani ama jamaica vijana itaongeza pato nchini na ajira lkn iwe chini ya ulinzi mkali.. hii ni fursa tuliyoifumbia macho
 
Mnajisumbua kwa uongozi huu ..ni sawa na kumpigia mbuzi gitaar mkitarajia amwage mauno bora Bata ....Rais mwenyewe anakuambia
..Sishauriki na ukijaribu ndo unaharibu kabisaaaa...vipi kwa vibaraka wake ..?
Ama kwel saul tumemtaka wenyewe acha ajitawale atakavyo...
"Kusikia kwa kenge hadi...."
 
Hivi hadi sasa maamuzi ya kukurupuka yamelitia taifa hasara kiasi gani vile...vile viwanda zaidi ya 1000 vimeajiri vijana kiasi gani vile ....hiv wale waliosema Rais aongezewe muda wa kuwa madarakani ni watz au wasomalia..? mbona twaweza wako kimya wapi tafiti au ile 1/4 imeongezeka..?
Hapa upepo tu kazi muulize punda....
 
Wanajamvi tumekuwa na nyuzi mbalimbali maalum, ambazo zimekuwa msaada mkubwa sana kwetu
Jamiiforums ni mtandao unaoheshimika sana, ni sehemu ya jamii(wapiga kura) ikiwa na mchanganyiko wa watu wa kaliba zote
Jamiiforums imekuwa chanzo muhimu cha habari kwa mitandao mingine na hata vyombo vya habari... Ni mtandao wenye mchango wa aina yake... Tunapaswa kuutumia vyema
Tumekuwa na mada zinazoibuka na kupotea zikiwa na lengo la kuishauri serikali kwenye mambo mbalimbali... Tuna wataalam wa kila aina humu na kuna wanajamvi walishawahi kuishauri serikali kupitia JF na ushauri wao ukafanyiwa kazi
Ndani ya Jamiiforums tuna watumishi wa serikali, wanasiasa na viongozi mbalimbali ambao haipiti siku bila kuperuzi JF ili kuona kuna kipi kipya ama jamii inasema nini kwenye jambo fulani
Kwa kuzingatia hayo yote ni muhimu sasa kuwa na huu UZI MAALUM wa kuishauri serikali yetu... Ushauri wako wowote hata kama hautafanyiwa kazi lakini utakuwa umetimiza jukumu lako kupitia maandishi kama Mtanzania mzalendo na mpiga kura, Kwahiyo usione uvivu wala kuvunjika moyo! Andika, maandishi hayafutiki na WANASOMA!

TIMIZA WAJIBU WAKO SASA....!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hakiki JF ni zaidi ya chanzo cha habari nchini.
 
Back
Top Bottom