Troll JF
JF-Expert Member
- Feb 6, 2015
- 7,804
- 12,224
Wakuu mimi binafsi natumia colget Advanced whitening kina ujazo wa 75mil si nyingi ila bei yake ni Tsh. 4,500 hii nzuri sana watoto wa Arusha utawakamata sana si unajua yale meno yao.
Je wewe unatumia Dawa gani? ili niweze ku shift kama ni nzuri zaidi! kuna hizi wanaziita sensodine naona zipo za aina nyingi na sijazikubali ni vigumu kugundua feki.
========
Dawa ya kusugulia meno ni kemikali inayotumika pamoja na mswaki wa kisasa kusafishia meno yazidi kupendeza na kuwa na afya.
Inasaidia kuondoa harufu mbaya, utambo wa meno na mabaki ya chakula katikati yake, pamoja na kuacha aina ya kinga (hasa ya floridi, kwa Kiingereza "Flouride") dhidi ya maradhi ya meno na ya ufizi (nyama inayoambatana nayo) (kwa Kiingereza "gingivitis").
Hata hivyo kwa kiasi kikubwa ufanisi wa usafi unategemea zaidi matumizi ya mswaki wenyewe kuliko ya dawa hiyo.
Badala ya dawa ya meno vinaweza kutumika chumvi na magadi.
Dawa ya meno hayatakiwi kumezwa kutokana na floridi iliyomo. Ikimezwa kidogo si hatari sana, lakini kama ni kiasi kikubwa ni lazima kuomba msaada wa daktari.
Dawa ya meno iliyotengenezwa kwa kusaga mifupa au chaza ilianza kutumika katika Ugiriki wa Kale na Roma ya Kale.
Matumizi yake yalienezwa hasa katika karne ya 19.
Nchi mbalimbali zimekataza aina kadhaa za dawa ya meno kutoka China kwa sababu zina sumu aina ya diethylene glycol (kifupi diglycol au DEG).
Michango ya wadau
Je wewe unatumia Dawa gani? ili niweze ku shift kama ni nzuri zaidi! kuna hizi wanaziita sensodine naona zipo za aina nyingi na sijazikubali ni vigumu kugundua feki.
========
Dawa ya kusugulia meno ni kemikali inayotumika pamoja na mswaki wa kisasa kusafishia meno yazidi kupendeza na kuwa na afya.
Inasaidia kuondoa harufu mbaya, utambo wa meno na mabaki ya chakula katikati yake, pamoja na kuacha aina ya kinga (hasa ya floridi, kwa Kiingereza "Flouride") dhidi ya maradhi ya meno na ya ufizi (nyama inayoambatana nayo) (kwa Kiingereza "gingivitis").
Hata hivyo kwa kiasi kikubwa ufanisi wa usafi unategemea zaidi matumizi ya mswaki wenyewe kuliko ya dawa hiyo.
Badala ya dawa ya meno vinaweza kutumika chumvi na magadi.
Dawa ya meno hayatakiwi kumezwa kutokana na floridi iliyomo. Ikimezwa kidogo si hatari sana, lakini kama ni kiasi kikubwa ni lazima kuomba msaada wa daktari.
Dawa ya meno iliyotengenezwa kwa kusaga mifupa au chaza ilianza kutumika katika Ugiriki wa Kale na Roma ya Kale.
Matumizi yake yalienezwa hasa katika karne ya 19.
Nchi mbalimbali zimekataza aina kadhaa za dawa ya meno kutoka China kwa sababu zina sumu aina ya diethylene glycol (kifupi diglycol au DEG).
Michango ya wadau
----World Dentists Association wamekubaliana kwamba dawa za meno ziko kwa ubora kama ifuatavyo:
1. Sensodyne
2. Crest
3. Colgate
Pamoja na ku list hizo dawa hapo kulingana na ubora wake lakini mambo yafuatayo ni lazima kuyatilia maanani
1. Jinsi ya kuutumia mswaki, wengi wetu huwa tuna maarifa haba ya kuutumia mswaki na mara nyingi hulifanya zoezi hilo kwa haraka sana kuliko inavyohitajika
2. Uhalisia wa Bidhaa
Nimeishawahi kutana na Sensodyne zinazotembezwa na Wamachinga zilikiuzwa bei rahisi sana nilipokuja kuzitumia niligundua zimechakachuliwa hivyo hazikuwa na ubora. Dawa ambayo sijaona kuchakachuliwa ni Crest labda kwa sababu siyo maarufu sana sokoni
3. Jina Moja Malengo Anuwai
Unaweza ukalalamika dawa haijakusaidia lakini Sensodyne au Colgate uliyochukua haiko sawa na mahitaji yako. Kuna Sensodyne kwa ajili ya kuripea, kungarisha au kuondosha kutu hivyo ni muhimu kusoma kasha la dawa kabla hujanunua au pata ushauri toka kwa dentists
----Me natumia colgate maxfresh ambayo ina box kama la redbrown (kuna zenye box la blue)hivii au ukisema maximum spiced unapatiwa iwe dukani kwa mangi au supermarkets zinapatikana 3500-4000 ,hizo sensodyne ,ile aloe hamna kitu japo dr wanashauri
----Mimi mwanzo nilipata sensodyne kwa 6500 nimetumia imesaidia kidogo ila mara ya pili nikanunua kwa 12000 hii ilikuwa kiboko.
Kuna jino langu limetoboka sasa ikifika usiku linauma balaa,nikawa natumia hii ya 12K basi jino likiuma napaka sensoydne mswaki napiga aisee baada ya dakika maumivu yote yanapotea kama sio jino lile.
Sasa hivi imeisha ni kama wiki hivi natumia mswaki tupu huwezi amini jino haliumi tena kama zamani na hakuna jino linalouma japokuwa limetoboka,nafanya mpango nifumbe macho nikanunue tena duka lilelile nina imani nikitumia kwa mwaka mmoja tu tatizo la meno litaondoka
Kuna Colgate ya Maji inaweza kukufaa. Ila Tumia Mouth Wash imeandikwa Lasterine kuna yenye rangi ya kijani na Gold (Nakushauri tumia ya rangi ya Gold ni nzuri zaidi unaweza kusukutua na kupigia mswaki) Then baada ya hapo tumia Colgate Herbal ni poa sana isipokuwa shida fake ni nyingi. Colgate Origanal ni ya Thailand au Brazil.
NB: Kwa meno yaliyotoba kitu kinachosaidia zaidi ni usafi wa meno kupiga mswaki mara tatu/kila baada ya kula nje ya hapo yatakuzingua tu maana mabaki ya chakula yakikaa siku kama tatu yanatengeneza uchafu/usaa unaoleta maumivu na uharibifu zaidi