Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,499
Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa imeonesha kushangazwa na kitendo cha Baraza la Wanawake wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) kutokutoa kauli yoyote baada ya Katibu Mwenezi wa BAWACHA Taifa, Sigrada Mligo (34), kushambuliwa kimwili.
Ikumbukwe kuwa, tarehe 25 Machi 2025, Mjini Njombe, iliripotiwa kuwa Mwenezi Mligo alifanyiwa shambulio la kudhuru mwili na mmoja wa walinzi wa chama hicho wakati wa kikao cha ndani kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akitoa tamko la jumuiya hiyo leo, Ijumaa, tarehe 28 Machi 2025, Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda, ameilaani vikali hali hiyo na kutoa wito kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe kuendelea kumsaka mtuhumiwa na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.
UWT imesema kuwa inashangazwa na kitendo cha BAWACHA kutokutoa kauli yoyote, na inasisitiza kuwa vitendo vya vurugu havipaswi kuvumiliwa na vinapaswa kupigiwa vita kwa nguvu zote.
Ikumbukwe kuwa, tarehe 25 Machi 2025, Mjini Njombe, iliripotiwa kuwa Mwenezi Mligo alifanyiwa shambulio la kudhuru mwili na mmoja wa walinzi wa chama hicho wakati wa kikao cha ndani kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akitoa tamko la jumuiya hiyo leo, Ijumaa, tarehe 28 Machi 2025, Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda, ameilaani vikali hali hiyo na kutoa wito kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe kuendelea kumsaka mtuhumiwa na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.
UWT imesema kuwa inashangazwa na kitendo cha BAWACHA kutokutoa kauli yoyote, na inasisitiza kuwa vitendo vya vurugu havipaswi kuvumiliwa na vinapaswa kupigiwa vita kwa nguvu zote.