wingi wa damu au kwa lugha ya kitabibu ni Haemoglobin(Hb)!
Kipimo chak huwa katika SI Units za gm/dl i.e grams per deciliter
Kazi ya Haemoglobin ni kubeba Oxygen kwenda sehemu mbali mbali za mwili na kiungo muhimu kinachoitaji Glucose na Oxygen nyingi ni Ubongo ila hata misuli huitaji oxygen ili kuunguza glucose ili uweze kupata Nguvu e.g Hata gari uitaji air/oxygen kuunguza Mafuta ili gari lipate nguvu ya kutembea.
Ndo maana ukiwa na damu chache/Hb ndogo unakua mchovu unasikia kizunguzungu na wakati mwingine hata kuzimia.
Normal Hb level utegemeana sana sana na jinsia e.g kwa mwanamke Normal level yao iko chini zaidi ukilinganisha na wanaume.
Pia normal levels utegemeana na teknolojia inayotumika mahabara moja na nyingine!
Ili si kuchanganye sana chukua kwamba normal Hb level ni 12-16.5gm/dl
Damu yako inaweza kupungua iwapo unaumwa kwa mda mrefu,Kupoteza damu sana e.g ajali au kwa wamama wakati wa kujifungua au wanawake wanaoingia period zilizopitiliza kawaida,tatizo la kutokula vyakula vyenye madini chuma kama mboga za majani na maini.
Damu chini ya 12g/dl kwa wanaume au 11g/dl kwa wanawake hili ni tatizo huitwa Anaemia
Damu ikiwa chini 6g/dl utaitaji kuongezewa damu au wakati mwingine ukipoteza damu nyingi ambayo imepunguza 2g/dl kutoka kwenye normal yako itakubidi kuongezewa damu.
Damu juu ya 6gm/dl---11gm/dll kama haikupi shida yoyote inaweza kutibiwa kwa kula vyakula vyenye madini chuma(Iron) kama mboga za majani,maini n.k au ukatumia dawa za kisasa zenye madini chuma ndani.
Damu nyingi ambayo inatishia afya yako kwa kitaalamu Polycythemia ni pale unapokua na Hb juu ya 16.5gm/dl kwa mwanamke au 18gm/dl kwa mwanaume.
Damu hii inakua nzito kiasi kwamba inakua sluggish kwenye mishipa na inaweza kuganda na kuenda kuziba mirija kama ya ubongo na inaweza kukupa stroke. Unaweza kulinganisha hii na maji na Oil kipi ukimwaga kitakua kinatembea kwa urahisi.
Ngoja niishie hapo nsikujaze na mambo ambayo hayatakusaidia!
kwa sasa nakaribisha maswali!