Breki za mbele za kigari changu ziliisha nikaenda mjini kwa madealer pair inarange kati ya elfu 40 hadi laki. Ukienda Toyota Tanzania breki similar ni 270,000 aisee ukiifunga unaona tofauti. Hakuna mkwaruzo kama imepakwa mafuta! Bidhaa substandard ni majanga.Mamlaka ivunjwe.
Tuunde mamlaka moja kwa EAC. Itakuwa rahisi kugharamia mafunzo yao na kupata vifaa na miundombinu inayohitajika katika kupima na kutambua ubora wa bidhaa.
Teh teh[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Yote tisa,
Kumi hujauziwa kadet nzuri ya kung'aa alafu ukiweka kwenye maji tu inageuka rangi, kama ilikuwa ya kijivu inakuwa nyeupe au njano
Ha ha ha! Hakuna tairi ya maana ya gari ndogo ndogo inauzwa chini ya TZS 350,000.145,000 kila tairi, ndo unanicheka sasa we mmama!!
Kwenye nguo kuna majanga zaidi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Yote tisa,
Kumi hujauziwa kadet nzuri ya kung'aa alafu ukiweka kwenye maji tu inageuka rangi, kama ilikuwa ya kijivu inakuwa nyeupe au njano
Acha upotoshaji,Ha ha ha! Hakuna tairi ya maana ya gari ndogo ndogo inauzwa chini ya TZS 350,000.
Mara elfu mtumba wa Canada kuliko brand new ya mchina.Kwenye nguo kuna majanga zaidi
... Yokohama ex Japan; Michelin; and the like.Acha upotoshaji,
Hizo bei kwa gari ndogo (rimsize 15-17) labda kwa Bf Goodrich.
Ila hizi za kina Linglong ,Goodride n.k nyingi zinacheza humo humo kwenye 140,000-160,000
Exactly [emoji106]... Yokohama ex Japan; Michelin; and the like.
Wazo zuri Mimi naona kuimarisha ya kwetu ni vizuri zaidi kwasababu bidha nyingi zinagusa maisha yetu,mfano simu nyingi ni feki na vipuri vyakeMamlaka ivunjwe.
Tuunde mamlaka moja kwa EAC. Itakuwa rahisi kugharamia mafunzo yao na kupata vifaa na miundombinu inayohitajika katika kupima na kutambua ubora wa bidhaa.
Umenena vema, tiles za goodwill ni takataka kabisa,tiles zimepishana size madhalani tiles ya 40cmx40cm zimepishana zingine 40.2cm mpaka 40.3cm zingine ni 39.8cm.Leo hii Tanzania imejaa bidhaa nyingi zenye ubora duni zilizotengenezwa China na ndani ya Tanzania, na kwa kiasi kidogo toka India na Thailand.
Leo hii, ni rahisi sana kuikunja nondo ya 16mm iliyotengenezwa Tanzania kuliko nondo ya 12mm iliyotengenezwa Kenya. Mathalani, ukienda dukani kutaka kununua nondo ya 6mm, utaulizwa unataka 6mm nene (imetengenezwa Kenya) au nyembamba (imetengenezwa Tanzania). Unajiuliza, hivi unene wa 6mm unawezaje kuwa na unene wa aina mbili? Ni sawa na mtu akuulize kama unataka kilo moja nyepesi na kilo moja nzito!!
Leo hii, siyo ajabu ukaingia dukani kununua kiatu kilichotengenezwa China, ukavaa asubuhi, jioni kikawa kimechanika.
Kwenye vifaa vya umeme na machinery, huko nako ni balaa. Kila duka zimejaa bidhaa za China, na kwa kukadiria, zaidi ya 70%, zina ubora hafifu kabisa. Mwaka 2017 nilinunua safety boot nchini Australia iliyotengenezwa China (made in China Australian standard) kwa Australian dola 100 (sawa kama U$80 au shilingi 170,000). Mwakajana nilinunua safety boot Dar iliyotengenezwa nchini China kwa shilingi 120,000. Ile ya Australia, mpaka leo, hakuna kilichobadilika, ni kama mpya, LAKINI ile ikiyotengenezwa China hukohuko lakini nikanunulia Dar, nilivaa miezi 4 tu, sole ilibanduka, na haikufaa tena. Huu ni mfano mdogo.
Kilicho dhahiri ni kuwa China inafahamika kwa kutengeneza bidhaa nyingi zenye ubora duni, na chache zenye ubora mzuri ambazo zinapelekwa kwenye mataifa ya watu wanaojitambua, na ambayo yana taasisi zenye uwezo mkubwa wa kupima na kudhibiti ubora.
Kilicho dhahiri hapa kwetu, TBS ni taasisi yenye ubora duni, itawezaji kudhibiti bidhaa zenye ubora duni? TBS ni duni kuanzia uwezo wa wataalam wake, vifaa na hata kimaadili. Wao wanachojali ni kulipwa pesa, ja siyo ubora.
Leo tuna mpaka bidhaa ndogo kama misumari ambayo ni ya kiwango duni kabisa. Misumari ambayo ukipiga kwenye ubao, kama ni hard wood, una uhakika wa zaidi ya 90% lazima utapinda au utashindwa kuingia kabisa.
Pendekezo:
Kwa kuwa taasisi yetu ya viwango haina kiwango, EAC iwe na taasisi moja tu ya kudhibiti viwango, ambayo itakuwa na wataalam wenye uwezo, nyenzo na maadili. Kwa bidhaa ambazo uwezo wa EAC kutambua ubora, ni mdogo, tuyaombe mataifa yenye uwezo kama Australia, tutumie viwango vyao. Mathalani bidhaa zitakazoruhusiwa kuingia nchini zilizotengenezwa China ziwe ni zile zenye label "Made in China Austrakia and EAC standards".
Taifa na watu wake tunapoteza pesa nyingi, tunapata hasara kubwa kwa kuingiza nchini bidhaa zenye ubora duni. Unaweza kununua bidhaa ya kiwango kizuri kwa shilingi 100,000 ikadumu kwa miaka 5, lakini unaweza kununua bidhaa yenye ubora duni kwa shilingi 50,000 halafu ikadumu kwa miezi 3 tu, ni bidhaa ipi inaendana na tjamani ya fedha yako? Watanzania tunaibiwa sana, na mataifa kama China kwa kuwa dampo la bidhaa duni, zisizofaa kuwafikia wateja. Hasara kubwa tuliyo nayo ni kuwa na shirika la viwango kama TBS lisilokuwa na viwango.
Hapa unadhani EAC Partner states wote wana nia nzuri baina yao za kiuchumi? Acha inferiority complex TBS inafanya majukumu yake vizuri mno, tatizo pia inawezekana uelewa wako juu ya mambo ya ubora na usalama upo chini. kuna bidhaa bora inatengenezwa kwa ajili ya kuishi mwezi pia kuna bidhaa bora kama hiyo hiyo na yenye usalama huo huo inatengenezwa kwa ajili ya kuishi mwaka. Wewe unapoingia sokoni kichwa kichwa na kulanguliwa bidhaa ya bei rahisi na ya muda mfupi TBS inahusikaje? Jiongeze; TBS inafanya kazi kwa mujibu wa sheria za kitaifa na kimataifaMamlaka ivunjwe.
Tuunde mamlaka moja kwa EAC. Itakuwa rahisi kugharamia mafunzo yao na kupata vifaa na miundombinu inayohitajika katika kupima na kutambua ubora wa bidhaa.
TBS wanatakiwa wapime ubora wa kiwango cha bidhaa iliyoko dukani na siyo wanayopelekewa na mtengenezaji. Tanzania ni mwanachama wa IBS (Shirika la Viwango la Kimataifa) hata hivyo bidhaa zetu hazikidhi viwango, TBS inapoweka alama yake kwenye vibiriti na mikate ambayo haina ubora hata kidogo ndipo utajua TBS haina manufaa kwetu kwani imekuwa ikipitisha ubora wa viwango kisiasa.Leo hii Tanzania imejaa bidhaa nyingi zenye ubora duni zilizotengenezwa China na ndani ya Tanzania, na kwa kiasi kidogo toka India na Thailand.
Leo hii, ni rahisi sana kuikunja nondo ya 16mm iliyotengenezwa Tanzania kuliko nondo ya 12mm iliyotengenezwa Kenya. Mathalani, ukienda dukani kutaka kununua nondo ya 6mm, utaulizwa unataka 6mm nene (imetengenezwa Kenya) au nyembamba (imetengenezwa Tanzania). Unajiuliza, hivi unene wa 6mm unawezaje kuwa na unene wa aina mbili? Ni sawa na mtu akuulize kama unataka kilo moja nyepesi na kilo moja nzito!!
Leo hii, siyo ajabu ukaingia dukani kununua kiatu kilichotengenezwa China, ukavaa asubuhi, jioni kikawa kimechanika.
Kwenye vifaa vya umeme na machinery, huko nako ni balaa. Kila duka zimejaa bidhaa za China, na kwa kukadiria, zaidi ya 70%, zina ubora hafifu kabisa. Mwaka 2017 nilinunua safety boot nchini Australia iliyotengenezwa China (made in China Australian standard) kwa Australian dola 100 (sawa kama U$80 au shilingi 170,000). Mwakajana nilinunua safety boot Dar iliyotengenezwa nchini China kwa shilingi 120,000. Ile ya Australia, mpaka leo, hakuna kilichobadilika, ni kama mpya, LAKINI ile ikiyotengenezwa China hukohuko lakini nikanunulia Dar, nilivaa miezi 4 tu, sole ilibanduka, na haikufaa tena. Huu ni mfano mdogo.
Kilicho dhahiri ni kuwa China inafahamika kwa kutengeneza bidhaa nyingi zenye ubora duni, na chache zenye ubora mzuri ambazo zinapelekwa kwenye mataifa ya watu wanaojitambua, na ambayo yana taasisi zenye uwezo mkubwa wa kupima na kudhibiti ubora.
Kilicho dhahiri hapa kwetu, TBS ni taasisi yenye ubora duni, itawezaji kudhibiti bidhaa zenye ubora duni? TBS ni duni kuanzia uwezo wa wataalam wake, vifaa na hata kimaadili. Wao wanachojali ni kulipwa pesa, ja siyo ubora.
Leo tuna mpaka bidhaa ndogo kama misumari ambayo ni ya kiwango duni kabisa. Misumari ambayo ukipiga kwenye ubao, kama ni hard wood, una uhakika wa zaidi ya 90% lazima utapinda au utashindwa kuingia kabisa.
Pendekezo:
Kwa kuwa taasisi yetu ya viwango haina kiwango, EAC iwe na taasisi moja tu ya kudhibiti viwango, ambayo itakuwa na wataalam wenye uwezo, nyenzo na maadili. Kwa bidhaa ambazo uwezo wa EAC kutambua ubora, ni mdogo, tuyaombe mataifa yenye uwezo kama Australia, tutumie viwango vyao. Mathalani bidhaa zitakazoruhusiwa kuingia nchini zilizotengenezwa China ziwe ni zile zenye label "Made in China Austrakia and EAC standards".
Taifa na watu wake tunapoteza pesa nyingi, tunapata hasara kubwa kwa kuingiza nchini bidhaa zenye ubora duni. Unaweza kununua bidhaa ya kiwango kizuri kwa shilingi 100,000 ikadumu kwa miaka 5, lakini unaweza kununua bidhaa yenye ubora duni kwa shilingi 50,000 halafu ikadumu kwa miezi 3 tu, ni bidhaa ipi inaendana na tjamani ya fedha yako? Watanzania tunaibiwa sana, na mataifa kama China kwa kuwa dampo la bidhaa duni, zisizofaa kuwafikia wateja. Hasara kubwa tuliyo nayo ni kuwa na shirika la viwango kama TBS lisilokuwa na viwango.
Wazo hili wataalam wetu wa UDSM wanahofia wataalam wetu watamezwa.Mamlaka ivunjwe.
Tuunde mamlaka moja kwa EAC. Itakuwa rahisi kugharamia mafunzo yao na kupata vifaa na miundombinu inayohitajika katika kupima na kutambua ubora wa bidhaa.
Nilichokielewa kwa mleta mada nikuwa:Uchumi bora utokomeza bidhaa duni
Mtu akiwa na uchumi mzuri atanunua bidhaa bora
umaskini ndio zao la bidhaa duni Mchina anakutengezea kutokana na bei yako
mfano bila Mchina kuwepo hata simu za mkononi hapa 80% tusingekua nazo
tbs inapaswa uwe wewe mwenyewe mkuu si ajabu wewe ndio mnunuzi wa feki
IBS kweli ni shirika la viwango la kimataifa? watanzania wenzangu tujenge utamaduni wa kujisomea na kujenga uelewa kwa mambo ya msingi yanayotuzunguka. Tunayotabia mbaya ya kumtafuta wa kumtupia lawama baada ya sisi wenyewe kufanya uzembe.TBS wanatakiwa wapime ubora wa kiwango cha bidhaa iliyoko dukani na siyo wanayopelekewa na mtengenezaji. Tanania ni mwanachama wa IBS (Shirika la Viwango la Kimataifa) hata hivyo bidhaa zetu hazikidhi viwango, TBS inapoweka alama yake kwenye vibiriti na mikate ambayo haina ubora hata kidogo ndipo utajua TBS haina manufaa kwetu.
Shika unachokielewa lakini ni hivyo au unaijua B I S ndiyo hiyohiyo.IBS kweli ni shirika la viwango la kimataifa? watanzania wenzangu tujenge utamaduni wa kujisomea na kujenga uelewa kwa mambo ya msingi yanayotuzunguka. Tunayotabia mbaya ya kumtafuta wa kumtupia lawama baada ya sisi wenyewe kufanya uzembe.