Uwezekano wa kuhama Mfuko wa Hifadhi ya Jamii

Inawezekana na sheria inayosimami haki ya mwajiriwa kujichagulia mfuko ipo , ongea na mwajiri wako yy ndo anapeleka data za member wote ktk mfuko husika, hvyo unaongea nae ili apeleke barua kuwa unataka hama mfuko! Then taratibu nyngne zinafwata.
 
Wadau,

Naombeni msaada juu ya hili,mm ni mtumishi wa Umma ni mtumishi mpya,kwa bahati mbaya sikupata maelezo ya kutosha juu ya mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii nimejikuta nimejiunga na mfuko ambao hauna mafao bora hivyo nataka kuhama kuhamia mfuko mwingine,swali langu je inawezekana kwa mtumishi wa umma kufanya hivyo,kama inaezekana taratibu zikoje?

nimejiunga na mfuko ambao hauna mafao bora hivyo nataka kuhama kuhamia
 
Kwanza Mkuu hujasema upo ktk mfuko gani?

Isije ukaruka mkojo ukakanyanga mavi (I'm sorry, ila najaribu kukusisitizia)

Pamoja na hayo ipo sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii inaendelea kutungwa ili kufanya kanuni za kutoa mafao ziwe sawa kwa mifuko yote & tofaut iwe ktk michango ya wabachama & miaka waliyofanya kazi

Pia ni vyema ukajua kuwa kubadili mfuko wa jamii km umefanya kazi na mwajiri mmoja kwa muda mrefu ni ngumu, labda km umebadili mwajiri
 
Inawezekana. Wasiliana na afisa utumishi wako na/au viongozi wako wa chama chako cha wafanyakazi wakusaidie kwani ni haki yako kuchagua mfuko uupendao
 
Wadau naombeni kujuzwa kama kuna impact yoyote kama ukihama mfuko mmoja wa hifadhi ya jamii kwenda mwingine, provided that kule umehama kwa kujitoa kabisa
 
wana jamvi, naombeni kujua kama kuna impact yoyote kama ukihama kutoka mfuko mmoja wa hifadhi ya jamii na kujiunga na mwingine, provided ule mwingine umejitoa, msaada tafadhali
 
we tulia tu huko huko, hakuna haja ya kuhama mambo yatakua mazuri tu. ameeni
 
Kuna taarifa kuwa kuna sheria za mifuko ya jamii zinazokusudiwa kanzishwa lengo ikiwa ni kumbana mteja- mwanachama wa mifuko hiyo. Nijuavyo mimi mifuko hii ilianzishwa ili kumuudumia mteja aliyejisajili, na mifuko hii inawajibika moja kwa moja kwa wateja wake. Swali ni je ikiwa kuna sheria zinakusudia kumbana mteja kiasi kwamba akisha jiunga na mfuko mmoja wapo kati ya hiyo mifuko hataruhusiwa kuhama,au kusitisha mkataba mpaka kwa kiwango cha mda flani na kwa kutimiza kiwango fulani cha mchango wake....mimi naona si sawa..Je sheria hizi ni kwa manufaa ya nani na zinakusudia nini?

WATANZANIA TUSIKUBALI..

Rafiki sasa hivi huwezi kuhama mfuko moja kwenda mwingine, SSRA inasimamia mifuko yote na kuna sheria ya kumukataza mwajiriwa kuhama mfuko. Mimi binafsi nilikuwa nafanya kazi kampuni binafsi na nikajiunga na mfuko mojawapo, nilipopata kazi serikalini nikajiunga na mfuko mwingine ila baada ya mwezi nikapigiwa na utumishi kuwa huruhusiwi kuhama mfuko,hatimaye nikaenda kujitetea kwa mwajiri nilichokuta ni fomu zangu nilizojaza nikiwa kampuni binafsi na wakaambanisha kifungu cha SSRA kinachomkataza kuhama mfuko.
 
mi nina miezi sita sasa toka nimejitoa kwenye mfuko flani. na sasa nimepata kazi serikalini naweza kuhamia mfuko mwingine? na ni mfuko gani mzuri kiuchangiaji na mafao naomba ushauri wenu wadau
 
mi nina miezi sita sasa toka nimejitoa kwenye mfuko flani. na sasa nimepata kazi serikalini naweza kuhamia mfuko mwingine? na ni mfuko gani mzuri kiuchangiaji na mafao naomba ushauri wenu wadau



Yeah unaweza, mfuko mzuri ni PSPF na LAPF
 
Teh teh sasa unajisfia kuhama mfuko badala uendeleze uanachama wako utaweza kuqualifie huko kuwa pensionable? Maranyingine u vulnerability tunautafuta wenyewe
 
Back
Top Bottom