Makoye Matale
JF-Expert Member
- May 2, 2011
- 6,491
- 2,104
Tangu mwaka 2006 Watanzania na viongozi wetu tumekuwa tunajidai kuwa tunao uwanja wa michezo wa kisasa kabisa huku tukisahau kuwa tunahitajika kujenga viwanja vingine zaidi katika miji kama Arusha, Tanga, Mbeya, Mwanza na Dodoma angalau tupate sifa ya kuandaa mashindano ya Cup of African Nations (CAN) au hata hiyo CHAN.
Hapo juu ni uwanja wa Soccer City katika Jiji la Johannesburg huko Afrika ya Kusini. Kwa kulinganisha uwanja wetu na uwanja huu wa wenzetu haitufundishi kwamba safari yetu ni ndefu katika ujenzi wa viwanja vya Michezo?
Tubadilike badala ya kujisifu kila kukicha huku tumelala usingizi mnono!