Uwanja wa ndege Dar waingia 10 bora Afrika

Uwanja wa ndege Dar waingia 10 bora Afrika

esther mashiker

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
616
Reaction score
555
1564758922911.png



Zaidi ya abiria milioni nane watahudumiwa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) baada ya kukamilika kwa jengo la tatu la abiria (Terminal III), huku jengo hilo jipya likiwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka.

Uwezo wa kuhudumia abiria hao kwa mwaka unaufanya Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kuingia katika viwanja kumi Afrika vyenye uwezo wa kuchukua abiria wengi. Jengo la kwanza la abiria (Terminal 1) lina uwezo wa kuhudumia abiria 500,000 kwa mwaka wakati jengo la pili (Terminal 2) likiwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni 1.5 kwa mwaka.

Hata hivyo, jengo la Terminal 2 ambalo ndilo linatumika kwa sasa limekuwa likilemewa na wingi wa abiria mpaka kufikia milioni 2.6 kwa mwaka. Kukamilika kwa jengo la tatu la abiria kutapunguza msongamano wa abiria kwenye jengo la pili na kurahisisha shughuli za usafiri wa ndani na nje ya nchi.

Akizungumzia mradi huo jana Alhamisi Agosti Mosi, 2019 wakati wa hafla ya uzinduzi uliofanywa na Rais John Magufuli, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale alisema wazo la kujenga uwanja huo lilikuja baada ya jengo la pili kuelemewa na wingi wa abiria.
 
Hivi kilichoingia kumi bora ni jengo la huduma au uwanja wa ndege? Kwa uandishi huu ndiyo maana wakiibuka waandishi wachache wenye weledi wa kuchambua mambo wanaitwa "Raia haramu"
 
Enzi zile pesa ipo nilikuwa napenda kula pizza na kuwatongoza wahudumu wa Flamingo 😛... Sasa nitahamia terminal 3 mambo yakikaa sawa...
 
View attachment 1170535


Zaidi ya abiria milioni nane watahudumiwa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) baada ya kukamilika kwa jengo la tatu la abiria (Terminal III), huku jengo hilo jipya likiwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka.

Uwezo wa kuhudumia abiria hao kwa mwaka unaufanya Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kuingia katika viwanja kumi Afrika vyenye uwezo wa kuchukua abiria wengi. Jengo la kwanza la abiria (Terminal 1) lina uwezo wa kuhudumia abiria 500,000 kwa mwaka wakati jengo la pili (Terminal 2) likiwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni 1.5 kwa mwaka.

Hata hivyo, jengo la Terminal 2 ambalo ndilo linatumika kwa sasa limekuwa likilemewa na wingi wa abiria mpaka kufikia milioni 2.6 kwa mwaka. Kukamilika kwa jengo la tatu la abiria kutapunguza msongamano wa abiria kwenye jengo la pili na kurahisisha shughuli za usafiri wa ndani na nje ya nchi.

Akizungumzia mradi huo jana Alhamisi Agosti Mosi, 2019 wakati wa hafla ya uzinduzi uliofanywa na Rais John Magufuli, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale alisema wazo la kujenga uwanja huo lilikuja baada ya jengo la pili kuelemewa na wingi wa abiria.
Asante Rais mstaafu Kikwete kwa kutujengea terminal three ya kisasa kabisa
 
aidi ya abiria milioni nane watahudumiwa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) baada ya kukamilika kwa jengo la tatu la abiria (Terminal III), huku jengo hilo jipya likiwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka.


Tatizo letu ni matunzo, utakuta hata taa zinaharibika replacement hakuna
 
Mheshimiwa tuwekee na uwanja wa KIA Jet Bridge.
 
View attachment 1170535


Zaidi ya abiria milioni nane watahudumiwa katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) baada ya kukamilika kwa jengo la tatu la abiria (Terminal III), huku jengo hilo jipya likiwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka.

Uwezo wa kuhudumia abiria hao kwa mwaka unaufanya Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kuingia katika viwanja kumi Afrika vyenye uwezo wa kuchukua abiria wengi. Jengo la kwanza la abiria (Terminal 1) lina uwezo wa kuhudumia abiria 500,000 kwa mwaka wakati jengo la pili (Terminal 2) likiwa na uwezo wa kuhudumia abiria milioni 1.5 kwa mwaka.

Hata hivyo, jengo la Terminal 2 ambalo ndilo linatumika kwa sasa limekuwa likilemewa na wingi wa abiria mpaka kufikia milioni 2.6 kwa mwaka. Kukamilika kwa jengo la tatu la abiria kutapunguza msongamano wa abiria kwenye jengo la pili na kurahisisha shughuli za usafiri wa ndani na nje ya nchi.

Akizungumzia mradi huo jana Alhamisi Agosti Mosi, 2019 wakati wa hafla ya uzinduzi uliofanywa na Rais John Magufuli, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale alisema wazo la kujenga uwanja huo lilikuja baada ya jengo la pili kuelemewa na wingi wa abiria.
Kwa statistics zipi, huduma? mapato, aircraft traffic, idadi ya passengers au uzuri wa jengo, kwa sababu ni jana tu umefunguliwa.
 
Haina maana kama wasiojulikana wanafanya ujinga na vyombo vya dola vipo inachafua taswaira ya taifa
 
Back
Top Bottom