Uvunaji mkaa una athari gani kwenye kilimo na mazingira yetu?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,628
46,273
Mkaa unauzwa bei rahisi sana nchi hii, huwa nashangaa kama kweli tunayo miti mingi ya kuiteketeza kiasi hicho! Je, Serikali inafanya utafiti wowote kuhusu athari za kukata miti ya asili na biashara ya mkaa inavyoleta athari kubwa katika mazingira na kilimo chetu kwa ujumla?

Serikali inajua ni miti kiasi gani inayokatwa kutengeneza gunia moja la mkaa linalouzwa elfu 20,000?

Serikali inajua inachukua muda gani kupanda mti utakaokua na kufaa kukatwa tena kwa ajili ya mkaa?

Serikali inafahamu ni kiasia gani cha miti inakatwa kila siku kwa ajili ya kutengeneza mkaa?

Serikali inafahamu ni kiasi gani cha ardhi inayobaki wazi kila siku kutokana na kufyekwa kwa miti ili kutengeneza mkaa?

Serikali inafahamu ni lini nchi hii itafikia ukomo wa kuwa na miti ya kukata kutengeneza mkaa?? Ukweli ni kwamba ipo siku tu miti yote ya kutengenezea mkaa itaisha kama ilivyoisha sehemu nyingine duniani.
Je, tunajiandaje ?
 
Wamekuja na mkaa mbadala (Rafiki coal briquettes) kama watafanya kadiri walivyosema itasaidia kwa kiwango kikubwa kuokoa misitu.

Mimi binafsi niliwapigia simu Stamico kujua namna ya upatikanaji wa huo mkaa, wakanambia wanatafuta agents wa kuusambaza, nikawaambia nipo tayari kuwa agent, wakaniambia andika barua ya maombi na ueleze unataka kuwa agent ktk mkoa gani, basi tangu nimeandika ni mwezi sasa! Hamna jibu lolote.
 
20220917_080929.jpg
 
Wamekuja na mkaa mbadala (Rafiki coal briquettes) kama watafanya kadiri walivyosema itasaidia kwa kiwango kikubwa kuokoa misitu.

Mimi binafsi niliwapigia simu Stamico kujua namna ya upatikanaji wa huo mkaa, wakanambia wanatafuta agents wa kuusambaza, nikawaambia nipo tayari kuwa agent, wakaniambia andika barua ya maombi na ueleze unataka kuwa agent ktk mkoa gani, basi tangu nimeandika ni mwezi sasa! Hamna jibu lolote.
Walikuondoa njiani tu
 
Back
Top Bottom