PreGE2025 UVCCM yalaani wanaovuruga amani kutoka nje

PreGE2025 UVCCM yalaani wanaovuruga amani kutoka nje

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Viongozi wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wakiwemo Wenyeviti wa Mikoa wameungana kwa sauti moja kulaani vikali kile walichokiita vitendo vya baadhi ya wanaharakati na watu wengine kutoka nchi jirani wanaojaribu kuvuruga amani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Msimamo huo umetolewa siku ya Jumamosi katika Jiji la Dodoma mbele ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohamed Ali Kawaida, wakati wa uzinduzi wa matembezi ya amani ya Kijani First Time Voters, yaliyoandaliwa na UVCCM kwa ajili ya kuwahamasisha vijana wapiga kura wa mara ya kwanza kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Wenyeviti hao wa UVCCM kutoka mikoa mbalimbali wameeleza kuwa amani ya nchi ni tunu isiyopaswa kuchezewa na kwamba vijana wa Tanzania hawawezi kukubali kuona taifa lao likivurugwa kwa hila au ushawishi wa watu kutoka nje.

Wamesisitiza kuwa vijana wa CCM watasimama imara kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa kisiwa cha amani, na kwamba wataendeleza juhudi za kuelimisha wenzao kuhusu umuhimu wa kuilinda nchi dhidi ya ushawishi wenye misingi ya kuchochea fujo au uchochezi wa kisiasa.

Source: Jambo TV
 
..okay.

..kwa hiyo uvccm hawana tatizo na genge la watekaji wanaovuruga amani kutoka ndani!!
 
Viongozi wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wakiwemo Wenyeviti wa Mikoa wameungana kwa sauti moja kulaani vikali kile walichokiita vitendo vya baadhi ya wanaharakati na watu wengine kutoka nchi jirani wanaojaribu kuvuruga amani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Msimamo huo umetolewa siku ya Jumamosi katika Jiji la Dodoma mbele ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohamed Ali Kawaida, wakati wa uzinduzi wa matembezi ya amani ya Kijani First Time Voters, yaliyoandaliwa na UVCCM kwa ajili ya kuwahamasisha vijana wapiga kura wa mara ya kwanza kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Wenyeviti hao wa UVCCM kutoka mikoa mbalimbali wameeleza kuwa amani ya nchi ni tunu isiyopaswa kuchezewa na kwamba vijana wa Tanzania hawawezi kukubali kuona taifa lao likivurugwa kwa hila au ushawishi wa watu kutoka nje.

Wamesisitiza kuwa vijana wa CCM watasimama imara kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa kisiwa cha amani, na kwamba wataendeleza juhudi za kuelimisha wenzao kuhusu umuhimu wa kuilinda nchi dhidi ya ushawishi wenye misingi ya kuchochea fujo au uchochezi wa kisiasa.
Screenshot_20250525_141152_Chrome.jpg
 
Viongozi wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wakiwemo Wenyeviti wa Mikoa wameungana kwa sauti moja kulaani vikali kile walichokiita vitendo vya baadhi ya wanaharakati na watu wengine kutoka nchi jirani wanaojaribu kuvuruga amani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Msimamo huo umetolewa siku ya Jumamosi katika Jiji la Dodoma mbele ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mohamed Ali Kawaida, wakati wa uzinduzi wa matembezi ya amani ya Kijani First Time Voters, yaliyoandaliwa na UVCCM kwa ajili ya kuwahamasisha vijana wapiga kura wa mara ya kwanza kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Wenyeviti hao wa UVCCM kutoka mikoa mbalimbali wameeleza kuwa amani ya nchi ni tunu isiyopaswa kuchezewa na kwamba vijana wa Tanzania hawawezi kukubali kuona taifa lao likivurugwa kwa hila au ushawishi wa watu kutoka nje.

Wamesisitiza kuwa vijana wa CCM watasimama imara kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa kisiwa cha amani, na kwamba wataendeleza juhudi za kuelimisha wenzao kuhusu umuhimu wa kuilinda nchi dhidi ya ushawishi wenye misingi ya kuchochea fujo au uchochezi wa kisiasa.

Source: Jambo TV



Hivi hawa jamaa hawana msamiati wa wezi na watekaji?
 
Back
Top Bottom