UVCCM mmekosa adabu kwa Mzee Moyo

UVCCM mmekosa adabu kwa Mzee Moyo

Mitoto ya CCM imevimbiwa ........wataweza je kujua wanakoelekea bilakujua walipotoka ?
 
CCM watafukuza fukuza sn na jambo hili kitawaathiri sn mana hawa wengine wanaowafukuza wana makundi yao ya wafuasi sasa vita ya panzi ni amani ya kunguu., ndivyo ccm inavyomaliza kufa., mansour kama kawaida 2015 anagombania jimbo kwa ticket ya cuf
 
Kuna siku niliomba CV ya shaka Naibu katibu UVCCM zanzibar sikueleweka, yule kijana ni hatari sana kwa usalama wa taifa hasa kauli zake ni zaidi ya nape yeye likija neno ni analitoa live bila chenga na kuangalia hadhira kuu

Ni shidah sanaaaa.
 
Nimesikitishwa sana na kitendo cha UVCCM wa Zanzibar kutishia kumnyang’anya na kumfuta uanachama wa CCM kada wake mkongwe mzee Nassoro Moyo eti kwa sababu tu anatetea na kusimamia wananchi wanyonge!Vitoto hivi, tena vinavyonuka mkojo na maziwa, vinapata wapi ujasiri wa kumdhalilisha mzee wetu. Mnatishia kumfukuza mzee wa watu kutoka CCM kana kwamba akitoka kwenye chama atakufa? Mnadhani ni ndani ya CCM tu ndipo kwenye uhai? Msijaribu kufananisha CCM na wanachama kama maji na samaki. Samaki ukimtoa ndani ya maji atakufa. Ingekuwa CCM ni maji na wanachama ni samaki, hilo tishio la kumtoa ndani ya chama lingekuwa na mashiko. Ni wanachama wangapi wamejitoa CCM na bado wanaendelea kuwatetea wananchi wakiwa nje ya chama hicho? Kwani akina Maalim Seif walitoka wapi? Acheni kuwa na akili mgando.

Tukumbuke kwamba huyu mzee ni mwanamapinduzi aliyepigania uhuru wa Zanzibar hadi akamung’oa sultani. Moyo amepigania uhuru wa Zanzibar tangu zamani sana, hata kabla wazazi wa hayo makinda (ya kunguru) yanayopanua midomo kumdhihaki mzee wetu, hawajaliona jua. Sasa iweje watoto wadogo hawa wamdhihaki huyu mwanamapinduzi huku viongozi wa juu wa CCM wamekaa kimya? Au ndio tuseme kwamba ‘ukiona kifaranga juu ya kichuguu, mama yake yupo chini ya kichuguu hicho’?

Ni lini hasa wanaCCM wataanza kuthamini uhuru wa mawazo miongoni mwa makada wake? Tumekuwa tukisikia makada wengi wa CCM wakienda kinyume na mawazo ya kikandamizaji ya chama chao lakini hatukuwahi kusikia wakitishiwa kunyang’anywa kadi au kufutwa uanachama. Mifano halisi ni Mohamed Raza na mzee Sabodo. Raza amekuwa akienda kinyume na ukandamizaji wa CCM mara nyingi sana. Lakini kwa kuwa anazo fedha za kukifadhili chama, hatukuwahi kusikia akitishiwa kufutiwa uanachama. Aidha, mzee Sabodo, kada maarufu wa CCM, ameenda mbali zaidi hadi kufikia hatua ya kukifadhili Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Na huyu mzee kwa kuwa huwafadhili CCM pia hatukuwahi kusikia vitisho vyovyote dhidi yake.

Hata mtu uende kinyume na maagizo ya CCM, ilmradi tu unawafadhili fedha, hawana taabu nawe. Shida iliyopo ni kama mwanacham ataenda kinyume na mawazo yao halafu ukawa hana ufadhili wowote kwenye chama. Hata mfadhili angekuwa fisadi, mchafu au mnyonyaji, hawezi kufukuzwa uanachama. Kwa maana hiyo CCM ni chama kisichokuwa na ubaguzi wa aina ya wanachama—ni kama dodoki—huzoa kila aina ya uchafu ilmradi tu huo uchafu uwe na manufaa kwa chama. Kamwe tusitarajie kwamba mafisadi wataisha ndani ya CCM. Hilo haliwezekani hata kidogo.

TANGANYIKA KWANZA
:yield:

Wanaokoteza sasa hawana dira.ccm imefikia mwisho.
 
Watu na waseme CCM siyo Mama Yao! Ukifukuzwa tambua kuna vyama kibao, tafakari na jiunge na chama kingine kinacho vumilia uhuru wa MAWAZO.

Huyu aliyesema CCM SIO MAMA YAKE ndiye alitakiwa awe wa kwanza kufutwa uanachama na kama angekuwa hai hadi leo angekwishajitoa CCM kwa hiari yake. CCM ni janga la kitaifa.
 
Ninachokiona na kuhakikisha,vijana wengi hawajui,Katiba ya CCM,imeanzia wapi,na kilianza kipi.Wale wengi wetu tunaojua TANU,ASP na CCM ndiyo wenye uchungu wa kuona katiba ya CCM siyo ile iliyotengenezwa na waasisi.Na ndiyo maana wengi hukimbilia kutukana,kukashfu,kukejeli bila kujua mtu huyu anaifahamu vipi CCM,pale anapohoji mambo yanayofanywa na viongozi wa CCM leo.
 
Nimesikitishwa sana na kitendo cha UVCCM wa Zanzibar kutishia kumnyang'anya na kumfuta uanachama wa CCM kada wake mkongwe mzee Nassoro Moyo eti kwa sababu tu anatetea na kusimamia wananchi wanyonge!Vitoto hivi, tena vinavyonuka mkojo na maziwa, vinapata wapi ujasiri wa kumdhalilisha mzee wetu. Mnatishia kumfukuza mzee wa watu kutoka CCM kana kwamba akitoka kwenye chama atakufa? Mnadhani ni ndani ya CCM tu ndipo kwenye uhai? Msijaribu kufananisha CCM na wanachama kama maji na samaki. Samaki ukimtoa ndani ya maji atakufa. Ingekuwa CCM ni maji na wanachama ni samaki, hilo tishio la kumtoa ndani ya chama lingekuwa na mashiko. Ni wanachama wangapi wamejitoa CCM na bado wanaendelea kuwatetea wananchi wakiwa nje ya chama hicho? Kwani akina Maalim Seif walitoka wapi? Acheni kuwa na akili mgando.

Tukumbuke kwamba huyu mzee ni mwanamapinduzi aliyepigania uhuru wa Zanzibar hadi akamung'oa sultani. Moyo amepigania uhuru wa Zanzibar tangu zamani sana, hata kabla wazazi wa hayo makinda (ya kunguru) yanayopanua midomo kumdhihaki mzee wetu, hawajaliona jua. Sasa iweje watoto wadogo hawa wamdhihaki huyu mwanamapinduzi huku viongozi wa juu wa CCM wamekaa kimya? Au ndio tuseme kwamba ‘ukiona kifaranga juu ya kichuguu, mama yake yupo chini ya kichuguu hicho'?

Ni lini hasa wanaCCM wataanza kuthamini uhuru wa mawazo miongoni mwa makada wake? Tumekuwa tukisikia makada wengi wa CCM wakienda kinyume na mawazo ya kikandamizaji ya chama chao lakini hatukuwahi kusikia wakitishiwa kunyang'anywa kadi au kufutwa uanachama. Mifano halisi ni Mohamed Raza na mzee Sabodo. Raza amekuwa akienda kinyume na ukandamizaji wa CCM mara nyingi sana. Lakini kwa kuwa anazo fedha za kukifadhili chama, hatukuwahi kusikia akitishiwa kufutiwa uanachama. Aidha, mzee Sabodo, kada maarufu wa CCM, ameenda mbali zaidi hadi kufikia hatua ya kukifadhili Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Na huyu mzee kwa kuwa huwafadhili CCM pia hatukuwahi kusikia vitisho vyovyote dhidi yake.

Hata mtu uende kinyume na maagizo ya CCM, ilmradi tu unawafadhili fedha, hawana taabu nawe. Shida iliyopo ni kama mwanacham ataenda kinyume na mawazo yao halafu ukawa hana ufadhili wowote kwenye chama. Hata mfadhili angekuwa fisadi, mchafu au mnyonyaji, hawezi kufukuzwa uanachama. Kwa maana hiyo CCM ni chama kisichokuwa na ubaguzi wa aina ya wanachama-ni kama dodoki-huzoa kila aina ya uchafu ilmradi tu huo uchafu uwe na manufaa kwa chama. Kamwe tusitarajie kwamba mafisadi wataisha ndani ya CCM. Hilo haliwezekani hata kidogo.

TANGANYIKA KWANZA
:yield:


Waliposema sikio la kufa halisikii dawa, hawakumaanisha masikio ya kichwani. Walimaanisha kila kinachoenda kufa huwa hakuna namna ya kukiponya. ndiyo maana utakuta mtu alikuwa hana safari yoyote, mara katoka na kung'ang'ania kupana gari litakaloenda kupinduka.

Hicho ndicho kinachoitokea CCM. Kwa sasa kimechoka sana. Na ni kweli kuwa raia wa Mungu wanateseka mno na kilio hiki kilishamfikia Mungu. Kinachotokea sasa ni kutimia kwa mpango wa Mungu tu. Inabidi haya manguruwe yafanye kufuru aina aina ili ambaye atakuwa hajakerw na hili basi akerwe na lile. Au ambaye hajadhulumiwa hiki adhulumiwe kile. Baada ya hapo wote wataamka na kuikataa CCM. Na hivyo ndivyo CCM itakavyozikwa.

Kwa asiyeelewa ni kwa nini nasema hivi, atafikiri nafanya porojo. Ila kwa wanaoelewa wanajua ni kwa nini nimesema hivi na ni kwa nini haya si ya utani, yatatokea. Waacheni wajaze kikombe cha dhulma zao, ili wakati ukifika hata shetani awakatae.
 
Hahahaaa yuko wapi jiongooo mb..w.a kasoro mkia mwambie mzee moyo katukanwa vp atalia
 
na wewe jeuri ya kuwasemea wazanzibar amekupa nani. unacheza ngoma usiyoijua.
 
Shekh hawezi kumlilia Nyerere huyo ni mlilia Tumbo.na ukweli kabisa shekh hawezi toka BAKWATA.

BAKWATA=CCM B. Ndio maana wale waislamu safi na wasiopenda dhuluma, ufisadi na wizi hawataki kuisikia hiyo BAKWATA. Na yule shehe aliyeigiza kulia anatakea hukohuko. CCM inapokaribia kufa inajishikiza kila mahali--inahaha. Chezea kifo wewe!
 
na wewe jeuri ya kuwasemea wazanzibar amekupa nani. unacheza ngoma usiyoijua.

kwani msemaji wa wazanzibar uliyemteua wewe ni nani? na wewe jeuri ya kuwasemea watukanaji amekupa nani au unacheza ngoma usoijua?
 
Moyo ccm sio baba yake, kushiriki mapinduzi sio hoja ya yeye kutofukuzwa kwenye chama. Kwani unawajua washiriki wa mapinduzi wote walifia ccm?
 
wana jamvi vijana wa ccm wanapendaga kutoa matamko juu ya mambo mbali mbali hususani yanayofanywa na wapinzani kupitia ukawa,juzi juzi wameandamana nchi nzima wakijinadi kulinda muungano wa serikali 2,wametoa matamko kuwa waasisi wametukanwa,huko zanzibar wametoa tamko mzee nassoro moyo afukuzwe ccm,kwa ufupi vijana hawa wameonekana kupitia vituo vingi vya radio na tv wakitoa matamko mengi kusisitiza uzalendo wa taifa tena wakijinasibu kuwa wao ni wazalendo;leo nataka kuwauliza mbona wapo kinyaa hatusikii matamko yao kama wazalendo wanao linda mali za nchi hii zinatafunwa?ripoti ya cag imeanika ubadhirifu mkubwa,tembo wana kwisha mwituni,bot bil 200 zimekwapuliwa,madawa feki arvs tumeona kiongozi mmoja akipandishwa kizimbani,bara bara zimejengwa hata mwaka hazina zinabomoka,hospital hazina madawa ya kutosha,mil 80 zimetengwa kununua rav 4 moja tu,wakulima wapamba hawataki kilimo cha mkataba lakini wanalazimishwa tu nk je uzalendo wa uvccm kama wanavyo jinasibu uko wapi?naomba kuwasilisha ongezeni mengine
 
UVCCM wapuuzwe. Hawa UVCCM ni watoto wa Mafisadi, wametumwa kuwalaghai watanzania.

Ewe Mtanzania, amka na sumbua akili yako kidogo na tafakari haya Maswali hapa chini:

A - Shule za kata hazina waalimu, hazina maabara.
B- Kama waalimu wapo wachache, hata hao wachache wanakosa mshahara na wanakosa moyo wa kufundisha hivyo kuleta Division zero nyiingi sana. Wanaoathirika ni watoto wa walalahoi- hawa watoto wa UVCCM wanasoma International schools na ni watoto wa vigogo.

C- Ajira ni shida kwa vijana. Wengi waliomaliza form 4 na kupata div 0, wanakuwa wamachinga na wanapigwa mabomu na serikali ya CCM, baba zao UVCCM.

D - Mikopo Chuo kikuu ni shida, watoto wa masikini hawapati.

Sasa naomba muwaulize UVCCM haya maswali. Mbona matamko kuhusu haya masuala hapo juu hawatoi???? Watanzania amkeni, kataeni propaganda za mwaka 47'.
 
Back
Top Bottom