UVCCM mmekosa adabu kwa Mzee Moyo

UVCCM mmekosa adabu kwa Mzee Moyo

hapo ni sawa na kuisema serikali ndani ya bunge la zima utapambana na wabunge wa ccm,hao ni watu waliopoteza dira hawajui waendako wala watokapo
 
hawana uzalendo mkuu ile ni njaa kama kweli wazalendo mbona wako kimya kwa taabu wanazopata watanzania wenzetu wa kusini na ubovu wa bara bara yao kuonekana imesahaulika huku bomba la gesi likijengwa kwa kasi? hawana lolote
 
UVCCM wapuuzwe. Hawa UVCCM ni watoto wa Mafisadi, wametumwa kuwalaghai watanzania.

Ewe Mtanzania, amka na sumbua akili yako kidogo na tafakari haya Maswali hapa chini:

A - Shule za kata hazina waalimu, hazina maabara.
B- Kama waalimu wapo wachache, hata hao wachache wanakosa mshahara na wanakosa moyo wa kufundisha hivyo kuleta Division zero nyiingi sana. Wanaoathirika ni watoto wa walalahoi- hawa watoto wa UVCCM wanasoma International schools na ni watoto wa vigogo.

C- Ajira ni shida kwa vijana. Wengi waliomaliza form 4 na kupata div 0, wanakuwa wamachinga na wanapigwa mabomu na serikali ya CCM, baba zao UVCCM.

D - Mikopo Chuo kikuu ni shida, watoto wa masikini hawapati.

Sasa naomba muwaulize UVCCM haya maswali. Mbona matamko kuhusu haya masuala hapo juu hawatoi???? Watanzania amkeni, kataeni propaganda za mwaka 47'.

Kama nilivyokwisa sema, nitaendelea kusema kuwa sisi wananchi wa Tanganyika na Zanzibar ndiyo tumewapa CCM na UVCCM haki ya kufanya wanayofanya. Vinginevyo haiwezekani kudi dogo la watawala wasiofika hata milioni mbili wawatweze wananchi milioni 45 na hao 45 eti wako kimya!

Kila mtu aanza kutimiza wajibu wake. Kila mtu anayestahili akajiandikishe kupiga kura. Siku ya kupiga kura kila mtu aliyejiandikisha akapige kura. Haiwezekani katika nchi yenye watu milioni45 waliojiandikisha kupiga kura hawajafika milioni kumi. Halafu tunakaa tunalalamika tunaonewa. Mara machinga na mgambo mara Bodaboda na jiji. Mara kodi za PAYE zimepanda mara gharama za maisha juu!

Jamani uwezo wa kuamua viongozi waweje tunao sisi. Tuanze kuutumia kwa kujichagulia serikali tunayoitaka. Tuache unafiki wa kujifunga khanga na vitenge vya vyama visivyo na tija kwetu. Vinginevyo tuache kulalamikia maisha kama kubadilisha system hatutaki.

Ukweli ni kwamba tutaendelea kuonewa mpaka tutakapoamka ujingani!
 
Elly B, umesema vyema. Watanzania tumekuwa waoga, na hiyo ndo inawapa nguvu hawa mafisadi. Tuendelee kuelimishana. Mbali na kuandika hata JF, huko site (mitaani na nyumbani) napiga soga na kumwaga sera za kutosha, mifano ya kutosha ili watu waamke na wafanye mabadiliko.
 
Back
Top Bottom