Uuwiii! Baba yetu RC Mwanza tuokoe na udadisi HBS Mwanza

Misungwi Yetu

Senior Member
Oct 7, 2017
103
39
NBS walitangaza nafasi za kazi kada ya Udadisi katika Utafiti wa Mapato na Matumizi ya Kaya Binafsi (Household Budget Survey - HBS), jumla ya nafasi 450 kwa nchi nzima.

Utaratibu kwa waombaji, pamoja na mambo mengine, sifa za msingi alipaswa kuwa na Elimu ya kuanzia kidato cha IV na pia awe mkazi kutoka katika eneo husika (mkazi ama mzaliwa wa kijiji au mtaa husika).
Kwa uthibitisho wa barua ya mtendaji wa kijiji au mtaa ambapo utafiti utafanyika.

Sisi katika kijiji chetu hapa Misungwi, waombaji tulikuwa NANE (8) TU, hadi siku ya mwisho kutuma maombi (12/ 08/2017). Nakala za Barua zetu hadi leo Mtendaji wetu wa Kijiji anazo.

Cha ajabu kati yetu hao waombaji nane, HAKUNA HATA MMOJA ambaye amewahi kutumiwa MESEJI wala KUPIGIWA SIMU kuitwa kwenye usaili unaosemekana kuwa ULIKWISHAFANYIKA.

Tumejaribu kufuatilia kwa Mtendaji wa Kijiji HAKUNA TAARIFA YEYOTE, hata yeye anashangaa tu. Tumeenda kuuliza kwenye Ofisi za TAKWIMU Mwanza, wanasema TUSUBIRI MATANGAZO YATATOKA TU, simu wakipigiwa HAWAPOKEI (0282502500).

Tetetsi mitaani inasemekana Watu walishapigiwa simu siku nyingi, inamaana Kijiji chetu WAMEKIRUKA? Au kuna WATU WATAPELEKWA TU?

Baba yetu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, tunakuomba ufuatilie hili jambo ili mchakato wake uwe kama wa Dar es salaam. Majina ya waombaji wote waliofaulu usaili yabandikwe, katika Mkoa wa Mwanza tumeomba wengi sana, ni kama Dsm tu.

Tunaomba mchakato uwe wa wazi ili turidhike na matokeo. Haya mambo ya kufanyia gizani yataleta malalamiko mengi na pia kuna harufu ya RUSHWA NA KUJUANA.

Karibuni Misungwi.
 
Teh tehe teh, mimi Mtendaji wa Kijiji (V.E.O) huku Mwanza. Kwenye kijiji changu wakiniletea majina ambayo sikuyaandikia Barua za Utambulishi, NITAWAKIMBIKIZA KWA VIBOKO! Ni lazima tuwe serious na mambo ya kitaifa.
 
Endeleeni kupambana watawasikia tu, sisi Dar tumefanya bidii mno ya kupiga kelele hadi wakatoa majina ya waombaji hadharani. Tatizo watu wengine hawajitambui
 
Teh tehe teh, mimi Mtendaji wa Kijiji (V.E.O) huku Mwanza. Kwenye kijiji changu wakiniletea majina ambayo sikuyaandikia Barua za Utambulishi, NITAWAKIMBIKIZA KWA VIBOKO! Ni lazima tuwe serious na mambo ya kitaifa.
haaaaaaa umenichekesha kweli, utafikiri mazuri. watendaji wetu wa vijiji mtusaidie jamani
 
angalau watuoneshe namna wanavyoita wasailiwa, usaili unavyofanyika n.k yaani kama walivyofanya dar es salaam, hadi raha
Kazi za muda hizo hazihitaji nguvu kama ile ya Dar unaweza ukapitia maombi yao tu na wakikuridhisha ni kuita vijana waje semina na kuanza kazi.
 
Kazi za muda hizo hazihitaji nguvu kama ile ya Dar unaweza ukapitia maombi yao tu na imarishika na kuita vijana wake semina na kuanza kazi.
kumbe hata huelewi kama hii kazi tunayopigia kelele ndiyo hiyo hiyo kama ya dar es salaam? inafanyika nchi nzima sio dar pekee
 
Zoezi wilayani halitafanyika kama Dar
kaka mbona wewe mgumu kuelewa? hapa tunamuomba baba yetu RC Mwanza, ajaribu kuingilia ili mchakato kwa mkoa wa mwanza ufanyike kwa uwazi. hata huku mwanza waombaji wa hii kazi ni wengi sana, hapo juu nimetoa mfano tu wa kijiji chetu kilichopo wilaya ya misungwi.
lakini kuna wilaya za ukerewe, kwimba, sengerema, ilemela, nyamagana n.k
 
Teh tehe teh, mimi Mtendaji wa Kijiji (V.E.O) huku Mwanza. Kwenye kijiji changu wakiniletea majina ambayo sikuyaandikia Barua za Utambulishi, NITAWAKIMBIKIZA KWA VIBOKO! Ni lazima tuwe serious na mambo ya kitaifa.
Kazi ya VEO ni ya kijinga kabisa,kwa hiyo wewe ni Executive Officer kama walivyo wakurugenzi? Usijidanganye,wewe ni mla vumbi
 
kaka mbona wewe mgumu kuelewa? hapa tunamuomba baba yetu RC Mwanza, ajaribu kuingilia ili mchakato kwa mkoa wa mwanza ufanyike kwa uwazi. hata huku mwanza waombaji wa hii kazi ni wengi sana, hapo juu nimetoa mfano tu wa kijiji chetu kilichopo wilaya ya misungwi.
lakini kuna wilaya za ukerewe, kwimba, sengerema, ilemela, nyamagana n.k
Kazi ya kijinga ndio unaanzishia Uzi hapa JF
 
kaka mbona wewe mgumu kuelewa? hapa tunamuomba baba yetu RC Mwanza, ajaribu kuingilia ili mchakato kwa mkoa wa mwanza ufanyike kwa uwazi. hata huku mwanza waombaji wa hii kazi ni wengi sana, hapo juu nimetoa mfano tu wa kijiji chetu kilichopo wilaya ya misungwi.
lakini kuna wilaya za ukerewe, kwimba, sengerema, ilemela, nyamagana n.k
Tafuta kazi nyingine achana na hizo
 
Back
Top Bottom