Utumishi Moshi Manispaa kwafukuta

Utumishi Moshi Manispaa kwafukuta

mtumishihuru

Member
Joined
Jan 8, 2020
Posts
8
Reaction score
11
Baada ya kuweka habari hii (Rushwa yatumika kupandisha watumishi madaraja Manispaa ya Moshi) sasa ofisi ya utumishi Manispaa ya Moshi kunafukuta. Tangu habari hii isomwe na maafisa wa ofisi ya utumishi Grace na Mary sasa wanahaha. Ili kujiokoa:

1) Ndani ya wiki moja wamewashusha madaraja watumishi wote waliopandishwa daraja hivi karibuni (evidence ya nakala za barua za kushushwa madaraja zipo ila naomba leo nisiziweke kuwahifadhi). Maswali yanayozuka ni kwamba kama kweli hawakuwapandisha kwa Rushwa kwa nini wawashushe baada ya makala hii?

2) Sasa Grace na Mary wamekuwa wakiwatishia walimu wanaohisi kuwa ndio wameandika habari hizi. Tayari wamewatishia waalimu kadhaa. Wamesahau kuwa habari za madudu ya Mary kwa mfano tumeanza kuyaandika toka zamani. Mfano harakati za Mary tuliziandika miaka mingi nyuma sana. Mfano Marrystela afisa utumishi moshi(manispaa) na ombwe la uongozi.

3) Siku mojawapo ndani ya wiki moja iliyopita nimefika ofisi ya utumishi na Grace akawa anawatuhumu walimu kadhaa huku akijiapiza kuwakomoa. Audio ya maneno yake ipo na kwa sasa namstahi ila akiendelea nitaiweka.

Ushauri wangu kwa Grace na Marry ni kwamba tulieni dozi iwaingie. Tupo hapa kumuunga mkono mheshimiwa Rais wetu John Pombe Magufuli anayehimiza uchapa kazi bila kuonea wananchi ama watumishi. Ni vema wajirekebishe na watende haki. Vinginevyo tutaendelea kuanika vitendo vyao vya rushwa na upendeleo.

Ndimi mtumishi wenu huru.
 
naturally hawa wenye majina ya akina Merisela na Grace ni waadilifu na wanyenyekevu..

hao wachunguze zaidi...huenda ni zao LA vyeti feki ama zilikuwa sketi za ma- lecturer

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maafisa utumishi ni shida sana, katibu mkuu utumishi amewasema lakini hawasikii, pia mkurugenzi wenu huko moshi ni kiazi, anaachache mambo ya kijingajinga yaendelee? au hao maafisa utumishi ni chakula chake?
 
Kuna mmoja pale ofisi ya mamlaka ya mkonge na yeye kazi yake ni kumtetea yule mwenzie anaesali naye kanisa la efata yan huyo dada s mfanyaj kaz na huyo afisa utumishi anamkingia kifua sana
 
Nyie ndo 'Zombie Citizens'. Kwani kushushwa watumishi madaraja ndani ya wiki moja baada ya habari hii si ushahidi? Habari hizi zinajulikana Moshi nzima usisubiri utafutiwe kila kitu
Nijuavyo kwasasa mtumishi hupandishwa cheo au vinginevyo kupitia mfumo rasmi (lowson); si vyepesi kupandisha na kushusha kama unavyoeleza wewe, otherwise hapo moshi bado mko zama za kalamazoo bin analogs. Kama umachosema kinaukweli basi kuna tatizo kubwa zaidi kuliko uwezo wako wa kuelewa
 
Kazi ya ualimu imekushida, tafuta kazi nyingine.

Pili kusoma sio kupandishwa daraja mjomba au shangazi, tumikia ualimu upata kupanda daraja.

Unaonyesha una chuki binafsi na Idara ya utumishi, na mikopo ya mabank kupitia mshahara ukiunganisha na mkopo wa bodi ya elimu kwenye ATM unakutanaga na 52,000 kila mwezi Sasa unatafuta kupandishwa daraja kabla ya wakati ili uweze kufukia mapengo ya mikopo,imekula kwako.

Kitakachofuta ni kuhamishiwa kufundisha shule za msingi Tena darasa la pili na la tatu akili yako ndipo itatulia.
Idadi ya walimu shule za sekondari Moshi manispaa haswa wa masomo ya Sanaa wamezidi kwa wingi na idadi kulingana na idadi ya wanafunzi mwisho wamekosa vipindi vya kufundisha Sasa wanahangaika na majungu mjini.tunaomba wapunguziwe shule za msingi zilizoko wilaya za same,rombo ,siha na mwanga penye upungufu wa walimu wa msingi.

Ova
 
Kazi ya ualimu imekushida, tafuta kazi nyingine.

Pili kusoma sio kupandishwa daraja mjomba au shangazi, tumikia ualimu upata kupanda daraja.

Unaonyesha una chuki binafsi na Idara ya utumishi, na mikopo ya mabank kupitia mshahara ukiunganisha na mkopo wa bodi ya elimu kwenye ATM unakutanaga na 52,000 kila mwezi Sasa unatafuta kupandishwa daraja kabla ya wakati ili uweze kufukia mapengo ya mikopo,imekula kwako.

Kitakachofuta ni kuhamishiwa kufundisha shule za msingi Tena darasa la pili na la tatu akili yako ndipo itatulia.
Idadi ya walimu shule za sekondari Moshi manispaa haswa wa masomo ya Sanaa wamezidi kwa wingi na idadi kulingana na idadi ya wanafunzi mwisho wamekosa vipindi vya kufundisha Sasa wanahangaika na majungu mjini.tunaomba wapunguziwe shule za msingi zilizoko wilaya za same,rombo ,siha na mwanga penye upungufu wa walimu wa msingi.

Ova
Nimekuwa nikifika ofisi ya utumishi kila mara kuona kama kuna mabadiliko yoyote.Jana nilifika na nikaongea na Grace bila kunitambua. Alianza kujitapa kwamba hakuna anayemweza na atawakomesha wanaojifanya kumharibia kibarua. Bahati nzuri nilimrekodi na audio yake nitai-upload soon akiendelea na huo ujinga. Na weweunayetetea tunakufahamu na utaumbuka soon. Niwakumbushe tu kwamba wahenga walisema kikulacho kinguoni mwako!
 
Nimekuwa nikifika ofisi ya utumishi kila mara kuona kama kuna mabadiliko yoyote.Jana nilifika na nikaongea na Grace bila kunitambua. Alianza kujitapa kwamba hakuna anayemweza na atawakomesha wanaojifanya kumharibia kibarua. Bahati nzuri nilimrekodi na audio yake nitai-upload soon akiendelea na huo ujinga. Na weweunayetetea tunakufahamu na utaumbuka soon. Niwakumbushe tu kwamba wahenga walisema kikulacho kinguoni mwako!
Wewe una chuki binafsi na Idara ya utumishi.ninakushauri kuwa unapoteza muda,na mapema hata kibarua ulichonacho kitaisha utakwenda kulima maboga na hujui utayauza soko lipi .
 
Nimekuwa nikifika ofisi ya utumishi kila mara kuona kama kuna mabadiliko yoyote.Jana nilifika na nikaongea na Grace bila kunitambua. Alianza kujitapa kwamba hakuna anayemweza na atawakomesha wanaojifanya kumharibia kibarua. Bahati nzuri nilimrekodi na audio yake nitai-upload soon akiendelea na huo ujinga. Na weweunayetetea tunakufahamu na utaumbuka soon. Niwakumbushe tu kwamba wahenga walisema kikulacho kinguoni mwako!
Lakini kupanda cheo lazima uwe umekidhi vigezo siyo kuwa mbabaishaji alafu unakuja huku kulalama
 
Baada ya kuweka habari hii (Rushwa yatumika kupandisha watumishi madaraja Manispaa ya Moshi) sasa ofisi ya utumishi Manispaa ya Moshi kunafukuta. Tangu habari hii isomwe na maafisa wa ofisi ya utumishi Grace na Mary sasa wanahaha. Ili kujiokoa:

1) Ndani ya wiki moja wamewashusha madaraja watumishi wote waliopandishwa daraja hivi karibuni (evidence ya nakala za barua za kushushwa madaraja zipo ila naomba leo nisiziweke kuwahifadhi). Maswali yanayozuka ni kwamba kama kweli hawakuwapandisha kwa Rushwa kwa nini wawashushe baada ya makala hii?

2) Sasa Grace na Mary wamekuwa wakiwatishia walimu wanaohisi kuwa ndio wameandika habari hizi. Tayari wamewatishia waalimu kadhaa. Wamesahau kuwa habari za madudu ya Mary kwa mfano tumeanza kuyaandika toka zamani. Mfano harakati za Mary tuliziandika miaka mingi nyuma sana. Mfano Marrystela afisa utumishi moshi(manispaa) na ombwe la uongozi.

3) Siku mojawapo ndani ya wiki moja iliyopita nimefika ofisi ya utumishi na Grace akawa anawatuhumu walimu kadhaa huku akijiapiza kuwakomoa. Audio ya maneno yake ipo na kwa sasa namstahi ila akiendelea nitaiweka.

Ushauri wangu kwa Grace na Marry ni kwamba tulieni dozi iwaingie. Tupo hapa kumuunga mkono mheshimiwa Rais wetu John Pombe Magufuli anayehimiza uchapa kazi bila kuonea wananchi ama watumishi. Ni vema wajirekebishe na watende haki. Vinginevyo tutaendelea kuanika vitendo vyao vya rushwa na upendeleo.

Ndimi mtumishi wenu huru.
Unajua utaratibu wa kupandisha madaraja/vyeo kwa watumishi wa umma?

Ni hv Afisa utumishi hana Room ya kumpandisha/Kumshusha mtu hasa kikundi kama unavyozungumzia wewe, maana Action yyt kwenye HRMIS au Lawson kama wengi wanavyoiita ili iwe Geniune na effective ni lazima iambatane na valid documents (signed and stamped) Na Action haiwi complete hadi iwe approved kwa level ya Katibu mkuu Utumishi.

Sitaki kubisha ila si kila kitu kinachoandikwa hapa kina ukweli. Tujaribu ku reason mambo mengine tusijazwe chuki kwa maslahi binafsi na mmoja mmoja!!

Simfahamu yeyote hapo Moshi but i stand not to be bias!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom