Mtumsafi
Member
- Jun 1, 2012
- 92
- 68
Mfuko wa uwekezaji wa pamoja UTT punguzeni ubabaifu katika kuhudumia watu,mnafanya clerical errors na badala ya kuzishughulikia mnampa mzigo mteja.Mkiwa watoa huduma tena mnaoshika vitu muhimu kama pesa hakikisheni mnafanya kazi zenu kwa weledi.Dunia iko kidijitali lakini mnafanya makosa yanayowagharimu wateja halafu mnajizima data.
Mathalani wimbi la kukosea na kuunganisha mifuko ya wazazi na wategemezi na kumkosesha mteja (mzazi) kupata huduma anapohitaji ni wazimu na tatizo sugu ambalo kila wakati linatokea na mkipigiwa huduma kwa wateja mnavimba na maswali mengi kwa makosa mliyofanya nyie wakati wa kuhifadhi taarifa za wateja. Mnaposema mteja aje ofisini na huduma ziko kiganjani kwa makosa yenu mnakuwa mnataka nini?
Mathalani wimbi la kukosea na kuunganisha mifuko ya wazazi na wategemezi na kumkosesha mteja (mzazi) kupata huduma anapohitaji ni wazimu na tatizo sugu ambalo kila wakati linatokea na mkipigiwa huduma kwa wateja mnavimba na maswali mengi kwa makosa mliyofanya nyie wakati wa kuhifadhi taarifa za wateja. Mnaposema mteja aje ofisini na huduma ziko kiganjani kwa makosa yenu mnakuwa mnataka nini?