Utoaji wa Mimba na gharama ya mapenzi

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Mara binti kapata mimba. Alikuwa anapendwa kweli na licha ya kuwa mara kwa mara walikuwa wanatumia kinga wakati fulani walikuwa hawatumii. Ahadi ilikuwa hata "ukipata mimba tutamtunza mtoto". Sasa binti kapata mimba. Hawako tayari kuwa na mtoto, hawana uwezo wa kulea mtoto kwa wakati huu. Mahali halipo kumtoa mtoto alelewe (adoption) ni kama halipo kabisa.

Binti anapewa pressure kubwa kwamba ni bora atoe mimba ili maisha yao yarudi kama zamani. Na pressure inaongezwa kuwa kama "kweli unanipenda"... binti anapiga mahesabu na kujiona hana "ujanja". Wanaenda kliniki na mimba inachopolewa japo kwa huzuni. Binti moyoni alitamani awe na mtoto wake lakini alijua ingekuwa vigumu sana kuweza kumlea mtoto huyo. Na mimba ilotolewa ilikuwa ni ya pacha.

Ndio mwanzo wa huzuni ulipoanza. Na machozi. Na aibu, na uchungu...

Miezi michache yule binti akashindwa kuendelea na kijana akaamua waachane. Upweke.

Miaka imepita binti kaolewa na yupo na mume wake kwa miaka. Hawajajaliwa kupata mtoto. Na hajawahi kumuambia kuwa amewahi kuwa na ujauzito... na Siri ikaongezeka.

Maskini, miaka inavyokwenda anatamani arudi siku ile .. siku ile.. ile siku ya machozi. Aombe msamaha.

Akasikia niliko.. kaomba ushauri.. amwambie mumewe ili awe na amani..? au aendelee kuombea wajaliwe..

Yakaanza kunilenga machozi... maskini rafiki yangu wa utotoni....
 
mkuu MM hiii ni true story au ni ubunifu wako wa utunzi wa kila siku???
yaweza kuwa true au ubunifu lakini nami nina true story ya my best frend inafanana kabisa na hii ya MM bint huyo sasa yuko kwenye ndoa 5yrs na hajafanikiwa kupata mtoto na hajui aanzeje kumweleza mumewe kuwa aliabort!
 
Mpe pole sana duniani kuna mambo mengi ya kuhuzunisha, hata akimwambia mmewe mambo yatabakia kuwa yale yale ..atubu dhambi zake kwa mwenyezi mungu aombe kwa imani Sara alipata mtoto wa uzeeni.
Lakini kama hayuko Confotable na anateseka moyoni kwa dhambi aliyoifanya amwambie tu mmewe ili angalau awe free na huo mzigo alioutunza moyoni mwake .
Ama wakachukue mtoto yatima wamtunze kama wa kwao
 
Mpe pole sana duniani kuna mambo mengi ya kuhuzunisha, hata akimwambia mmewe mambo yatabakia kuwa yale yale ..atubu dhambi zake kwa mwenyezi mungu aombe kwa imani Sara alipata mtoto wa uzeeni.
Lakini kama hayuko Confotable na anateseka moyoni kwa dhambi aliyoifanya amwambie tu mmewe ili angalau awe free na huo mzigo alioutunza moyoni mwake .
Ama wakachukue mtoto yatima wamtunze kama wa kwao

Ni wanaume wachache watakaoweza kustahimili taarifa ya aina hiyo. Binafsi nadhani the moment najua hilo, naweza kucolapse au ndo kwanza naivunja ndoa. Huwa tunajitahidi kuvumilia pale tunapokosa mtoto kwa kuamini kwamba ni majaliwa ya mwenyezi Mungu lakini si rahisi kuvumilia kwa kujua kwamba mwenzangu aliharibu kizazi kwa makusudi. Otherwise huyo binti ataingia kwenye mateso mengine makubwa na magumu. Achunguze kwanza busara ya huyo mwanaume. Kama si mstaarabu atatafuta mke wa pembeni na kuanza kumtangazia mbovu.
Bora afe nayo siri yake maana kuisema au kutokusema hakutasaidia kumaliza tatizo alilonalo.
 
Duh, hii noma sasa. Solution ni kutooa mpaka uhakikishe kitu kimetinga nyavuni, bila hivo UWIZI mtupu..siku hizi kila mtu mjasiriamali, unatakiwe uwe dakika mbili mbele au sivo imekula kwako.
 
na ndio maana ndoa za siku, almost zinfungiwa leba......
Back to ushauri....kweli itakuweka huru......sema kweli halafu ukabiliane na madhara ya ukweli wenyewe..
Asisema kweli, baada ya muda fulani (kutegemea na uvumilivu wa mme), hamu ya mume kuwa na mtoto itazidi uwezo wake wa kuhimili. Kitakachofuata ni ama ufarakano au migogoro ya kudumu katika ndoa yenyewe.
 
Akasikia niliko.. kaomba ushauri.. amwambie mumewe ili awe na amani..? au aendelee kuombea wajaliwe..

Mimi nadhani busara ingekuwa kwa yeye/wao kutafuta sababu hasa ya kutopata mtoto. Kama ni tatizo ni mwanamke na sababu ni ile mimba iliyotolewa, then ni vema isiindelee kuwa siri tena. Si haki kuendelea kumsubirisha mwanaume 'kujaaliwa' kwa vitu ambavyo kamwe havitatokea. Ukweli ni lazima uwekwe wazi ili kama wanaamua kuendelea yawe ni maamuzi ambayo msingi wake ni ukweli (informed decision).
 
mkuu MM hiii ni true story au ni ubunifu wako wa utunzi wa kila siku???

Ni true story hata kama haimhusu yeye. Kwani kwa siku hizi ni watu wengi wamekuwa wahanga wa matukio kama hayo hasa wale wanaofanya abortions ambazo sio successful 100% au incomplete.
 
Kuua ni dhambi... lakini pia kutopata mtoto ni majaaliwa ya Mungu. Kuna watu kibao wanaokosa watoto ingawa hawajawahi kufanya abortions....

Anaweza kukaa na siri moyoni akiwa na matumaini ya kupata mtoto hapo baadae... kwanza ajichunguze kama anaweza beba mimba... inawezekana wakati wa abortion walifanya damages kwenye uterus.
 
.........Nimesoma hii story hadi najisikia uchungu,maskini dada wa watu halafu mbaya zaidi hayupo na yule aliosababisha atoe mimba.
Huu ni msalaba mkubwa sana kwake na asimwambie mumewe hii siri inaweza kuhatarisha ndoa.............abaki nayo moyoni na aombe na kutubu kwa Mungu kwa kosa alilolifanya. Mungu wetu ni wa rehema anaweza kumsaidia kupata tena mtoto.
 
Kwa nini utoe mimba? Dhami maana hata mtot anayeuwawa anahaki ya kuishi kama wewe unavyoishi-kama unaenda kwenye starehe unategemea nini?

Majuto ni mjukuu!! La muhimu ni kutubu kwa dhati mbele ya mwenyezi mungu na kuamini kuwa umesamehewa na utapata mtoto tena.Je kama mwanaume ana matatizo na wewe unajihisi tu eti kwa kuwa uliwahi kuabort?
Fanya uchunguzi wa kina dada na mwisho uatakuwa na jibu.Usikimbilie kusema chochote kwanza.Hakikisha kuwa wewe ndo huwezi kuzaa kabisa then u cana dicide.
 
Utoaji mimba una madhara makubwa kiafya na kisaikologia. Mara nyingi mimba ambazo zimetolewa na watu ambao sio wataalamu mahiri wanaweza kuchokonoa na kuharibu kizazi ma matokeo yake mwanamke hawezi kubeba mimba tena. Vile wale watoto waliotolewa mimba wanamlilia Mungu siku siku zote kwa ajili ya haki yao ya kuishi waliyonyang'anywa. Wako watu waliotubu baada ya kutoa mimba na walishuhudia katika maono jinsi watoto hawa wanavyomlilia Mungu. Baada ya toba na maombezi maalumu walirejea katika maisha ya kawaida na wana familia zao.

Ukificha dhambi hutapata msamaha mbele za Mungu. Lakini Mungu asema njoo tusemezane. Ijapokuwa dhambi zenu ni nyekundu kama damu zitasafishwa na kuwa nyeupe kama theluji........ Mshauri rafiki yako akafanye maombi maalumu na kutubu kwani Mungu ni mwingi wa rehema na fadhila
 
true story...


Nimesikitishwa sana na hili; na sio kwa wasioolewa tu hata walioko ndani ya ndoa; Katiaka kuamsaliti mume ndani ya ndoa mwanamke alipata ujauzito na kwa kuficha aibu alishindwa kumpakazia jamaa na kuamua kutoa mimba! Kilichofuatia ni kama kinachomkumba huyu dada! Its very sad!
 
Hivi karibuni nilipokea taarifa za kifo cha Daktari maarufu hapo Dar ambapo kwa inner cycle yetu alifahamika kama Dr. Abortion; NI kajaribu ku-imagine akikutana Muumba huko Mbinguni anajielezaje?......................::twitch::
 
Back
Top Bottom