Kamsongole,
Pole na changamoto.
Katika swali/shida yako kuna mambo mawili kama nimekuelewa: 1. Kutibia fibroid 2. Kusave ndoa kwa kupata mtoto.
1. Kwavile daktari alishakufanyia tathmini na kuona kuwa ni lazima utolewe kizazi, inakuwa vigumu kupitia mtandao kutoa tathmini tofauti. Hii inaashiria kuwa umefanyiwa ultrasound na uvime umeonekana kuwa aidha ni mkubwa sana au upo mahali ambapo hauweyi kutolewa na kuacha kizazi au pengine jinsi unavyoonekana umempa hofu daktari kuwa uvimbe huo una hatari ya kuwa kansa. Kwahiyo ushauri ninaokupa kwenye hili, hakikisha daktari anayekushauri ni gynecologist mzoefu na itakuwa vizuri kama gynecologist huyo anakufanyia ultrosound yeye mwenyewe na sio kusoma repost ya ultrasound iliyofanywa na mtu mwingine.
2. Kusave ndoa. Inagwa hujaandika hapa, lakini napata hisia kuwa kilichosababisha kugunduliwa kwa uvimbe ni wewe kwenda hospitali kwa tatizo la kukosa mtoto kwa miaka minne. Kwa vile imeshauriwa utoe kizazi, uwezekano wa wewe mwenyewe kubeba mimba hautakuwepo ukishatoa kizazi, lakini hii haimaanishi kuwa hauna uwezo wa kupata mtoto. Maendeleo ya sayansi ya kitabibu yamefikia hatua ya kuweza kuchukua yai lako na mbegu ya mmeo na kuziunganisha kutengeneza mtoto atakayekulia kwenye tumbo la mwanamke mwingine. Sijajua upatikanaji wa huduma ya namna hii nchini kwetu ukoje na unafuata sheria zipi, lakini iwapo utaamua kutoa kizazi basi ulizia uwezekano huu. Natambua pia kuwa gharama yake ni kubwa.
Upo pia uwezekano wa kuadopt mtoto. Mkiandaliwa vizuri kisaikolojia mnaweza kuendelea kuishi kwa furaha na mtoto wenu mliyemuadopt.
Kuhusu kutoa mimba kama alivyosema mdau hapo juu, chukulia kama changamsha baraza tu. Naamini hata yeye hakuwa serious, alikuwa anatania...
Mwingine yuko kule MMU, yeye mke wake ana uvimbe uliosababishwa na sindano/vidonge vya majira, wamezunguka weeee kwa madaktari, hadi sasa option ni kutoa kizazi kwani hawezi kuzaa tena, nawaonea huruma hawa wadada jamani. Lakini kwa uelewa wangu mdogo fibroid, huwa zinawapata wamama wenye umri wa kati miaka 34 - 40 waliochelewa kuzaa na huwa zinatolewa, sasa huyu mdada sijui ni vipi, lol!
Fibroids huwa ni vigumu au haiwezekani kusema kitu gani specifically kimesababisha. Kwahiyo huyo anayesema zimesababishwa na vidonge anahisi tu.
Vilevile huwa haiwezekani kuwana uhakika wa asilimia 100 kuwa kutokuzaa kumesababishwa na fibroid. Mtu anaweza kuwa na fibroid kubwa kama kicha cha paka lakini akazaa bila matatizo.
Halafu huwa hakuna umri maalum ambao yinatokea ingawa kwa vuile huwa zinakuwa kidogkidogo ndio maana mara nyingi fibroid kubwa wanaonekana nazo watu wenye umri mkubwa.
Kuhusu uhusiano na watu ambao hawajazaa sina evidence za kutosha lakini in theory watu ambao hawajazaa hormones yinaact kwenye endometrium/layer ya ndani ya kifuko cha uzazi na hizi fibroids zinatokea kwenye msuli wa kifuko cha uzazi kwa hiyo sitegemei kuwa na uhusiano wa moja kwa moja. Ingawa sina evidence za kunipa uhakika, ila kungekuwa na uhusiano lazima ningekuwa nimepata kusikia...
Ahsante kwa kunielewesha, kumbe sometimes unaweka siasa pembeni eeh! Thanks sana
habari zenu wadau!! poleni na majukumu..naombeni ushauri wenu wataalamu na wale waliowahi ku experience hili tatizo (hasa wakina dada)..nna dada yangu ana tatizo la kutoka damu mda mrefu, kwa karibu miezi mi nne (4) sasa au zaidi bila kukata, tofauti na ule utaratibu wa kawaida wa hedhi i.e siku 3-5, amekwenda hospitali moja ya wilaya na kuwaona wataalamu wakampatia dawa za kutumia, lakini hakupata ahueni (damu haijakata) akarudi tena hospitali wakajaribu kumfanyia uchunguzi/vipimo wakamwambia anaviotea gani sijui kwenye mfumo wa uzazi, wakampatia tena dawa za kutumia ,but so far hakuna relief yoyote ile..so tunaomba ushauri wenu wadau..siku njema
Mkuu Konya, Poleni sana kwa hilo.
Mpelekeni akapime/akacheck FIBROID. fibroid ni uvimbe unaojiotesha wenyewe kwenye uterus (mfuko wa uzazi) na huwa unakua taratiibu mpaka mnaweza mkadhani ni mimba. Moja ya dalili zake ni hiyo kwamba damu/hedhi inatoka mfululizo au mara kwa mara isivyo kawaida. Tiba yake ya kudumu ni operesheni (kufanyiwa upasuaji) kuondoa huo uvimbe.
USHUHUDA: mwaka juzi tu kuna mama yangu mdogo huko kijijini alikuwa na tatizo hilo la kuvuja damu mara kwa mara, baada ya muda wa miezi kadhaa hivi akaanza kuzidiwa kwa kuishiwa damu mwilini, nusra afariki! wakampeleka kwenye hospitali ya Wilaya kwa vipimo. wakampima na kumueleza kuwa eti ana cancer ya uzazi. so wakampiga dripu ya damu na kumpa dawa za kuwa anatumia akiwa nyumbani. Ndipo tukamfuata na kumleta Dar, akafanyiwa vipimo na kumkuta ana huo uvimbe wa Fibroids (tena uvimbe ulikuwa umeanza kukua) tu, hakuna cha cancer ya uzazi wala nini. Then akafanyiwa upasuaji (operesheni) na kuondoa hiyo Fibroids. Mpaka dakika hii yupo huko kijijini mzima wa afya kabsaaaa kama kawaida. Watalaam wanasema sababu mojawapo inayosababisha Fibroids ni matumizi ya hizi dawa za Uzazi wa Mpango kwa akina mama.
So ushauri wangu ni kwamba, mpelekeni kwenye HOSPITAL KUBWA akafanyiwe vipimo vizuri. Tena fanyeni haraka sana, iyo inshu ni seriouz sana, anaishiwa damu na mnaweza mpoteza. Akina mama wengi vijijini wanafariki kwa hilo tatizo.
Me yangu ni hayo. Humu JF ni junguu kuu, ngojea watalaamu watakuja na kuchangia zaidi.
Zetu Dua kwa mgonjwa.
Mpigie mwenye namba hii 0714755582, mweleze tatizo hili. Nimeshaona akisaidia watu wenye matatizo kama hayo na wamepona.
Pata majibu na maelezo ya maswali yafuatayo kutoka blog ya Afya Njema; Mafanikio Na Utajiri (www.mtsimbe.blogspot.com)
Kwa maoni tuandikie: mtsimbe@gmail.com
Hapo kwenye RED ndipo huwa naanza kustuka mapema kwani wengi wenu ni wasanii wa hali ya juu, Kuna jamaa alikuwa anaongea kwa rafudhi ya kikongo kila siku Mnazi mmoja (Dar) alikuwa anatumia kipaza sauti kuwaeleza watu kuwa umaskini wao unasababishwa na wao wenyewe kwani yeye ana dawa ya Tshs 500/= ambayo inaweza kukuondolea umaskini mara moja !!!!!. Na watu wananunua, we acha tu!!
kwa upande wa Afya nilienda Iringa - karibu na uwanja wa ndege wa Nduli, hapo jumamosi wanauza nyama ya Mbuzi na vitu vingine ni kama mnadani. Sasa kuna mama anauza dawa (kikombe Tshs 500/= ) ya kujikinga na Gauti na magonjwa mengine pia, watu wanazifakamia nyama zisizoiva vizuri eti mama anawapa dawa hakuna shida. Jamaa yangu ambaye ni dr. alisema kuwa baada ya muda mfupi watu wataugua magonjwa hayo kwa kasi kwani ile haina tofauti na babu wa Loliondo.