Naomba wana jamvi nisimulie hapa mambo yaliyonitokea nikiwa naondoka Dar es Salaam kupitia uwanja wetu wa JNIA.
Ilikuwa saa tisa na dakika 45 mchana nikiwa kwenye line ya abiria wanaoondoka kwenda safari zao za nje au ndani pale pale. Kama kawaida nimekaa kwenye line nikapita kwenye office ya anayekagua passport na ticket. Ilipofika wakati wa kukagua mizigo yote tuliweka kwenye screen kama abiria wengine. Nilikuwa na sanduku moja na box moja na mfuko mmoja ambao ulikuwa bado haujafungwa. Huo mfuko ulikuwa ni unga wa sembe ya chapa Mama nilionunua Arusha.
Baada ya mizigo kupita na mimi nilipita then ikafikia wakati wa kuchukua mizigo yangu kwa ajili ya kucheki-in. Kabla sijachukua ule unga security mmoja wa kike akaniuliza, hii nini? Nikamwambia ni unga wa sembe kama ulivyoandikwa kwenye package yake hapo juu. Akaniambia kwa tone ya kufoka, "eleza vizuri usipoteze muda hapa". Nikamjibu, my sister ni unga wa ugali ninakaa mbali na Tanzania huwa nina hamu ya kula chakula cha nyumbani nikiwa huko, na ndiyo maana nimebeba huu unga. Akadakia mwingine wa kiume, "tunashaka ni drugs hii kwa hiyo ili ku test kama ni drugs au siyo drugs fungua na ukate package moja na ulambe" Nikawaambia kipimo cha drug ni kulamba? Hata hivyo mimi ndiye mshukiwa kwa hiyo unaniambia nilambe kama ni drug unadhania nitakupa jibu gani? Lazima nitasema sio drug ili nipite. Kwanza huu ni unga unapaswa kuliwa ukiwa umepikwa nikilamba mbichi nitaumwa na tumbo. Ninasafiri mbali kama masaa 15 kwenye hii flight tafadhali fikirieni na nyie. Akadakia mwingine na kusema "anatubabaisha huyu chukua pass yake nenda ku-cancel flight yake".
Mara wakaitana wengine wawili wakawa wanne. Wakaongeza polisi wengine wawili wenye uniform na vyeo vya Inspector na wawili CID. Yule dada wa kwanza akawa ameshakuja na wembe akakata ile pakti moja wakaniambia lamba haraka au tuna cancel flight yako. Wote sasa wakawa kitu kimoja wakajaza watu. Embarrassment ya ukweli.
Polisi mmoja wa uniform mwenye cheo cha inpector alikuwa mstaarabu saana akawaambia kwa kuangalia tu huu ni unga wa ugali, akaja dada mwingine naye akawaambia mnampotezea abiria muda na kazi imesimama hapa chukua hii pakiti moja pitisha kwenye machine yenyewe mumuachie aende. Wale wa kwanza kabisa na polisi mmoja wa kike mwenye cheo cha inspector wakasema no lazima alambe. Nikachotewa size ya kijiko cha chai nikalambishwa wakafurahi na kuniruhusu niendelee. Ila walichukua pass yangu wakaenda kutoa copy. CCTV camera za airport ni shahidi yangu. Naomba uongozi uangalie muda huo 15:45 hrs kwenye departure siku ya tarehe 13/9/2013.
Maoni yangu ni kuwa ikiwezekana hao wafanyakazi wachukuliwe hatua kwa sababu utendaji kama huo wa kutokutumia akili na unatia hasara nchi na kuwafanya wale watendaji wazuri waonekane pia kama hawajui wanachofanya.
Ilikuwa saa tisa na dakika 45 mchana nikiwa kwenye line ya abiria wanaoondoka kwenda safari zao za nje au ndani pale pale. Kama kawaida nimekaa kwenye line nikapita kwenye office ya anayekagua passport na ticket. Ilipofika wakati wa kukagua mizigo yote tuliweka kwenye screen kama abiria wengine. Nilikuwa na sanduku moja na box moja na mfuko mmoja ambao ulikuwa bado haujafungwa. Huo mfuko ulikuwa ni unga wa sembe ya chapa Mama nilionunua Arusha.
Baada ya mizigo kupita na mimi nilipita then ikafikia wakati wa kuchukua mizigo yangu kwa ajili ya kucheki-in. Kabla sijachukua ule unga security mmoja wa kike akaniuliza, hii nini? Nikamwambia ni unga wa sembe kama ulivyoandikwa kwenye package yake hapo juu. Akaniambia kwa tone ya kufoka, "eleza vizuri usipoteze muda hapa". Nikamjibu, my sister ni unga wa ugali ninakaa mbali na Tanzania huwa nina hamu ya kula chakula cha nyumbani nikiwa huko, na ndiyo maana nimebeba huu unga. Akadakia mwingine wa kiume, "tunashaka ni drugs hii kwa hiyo ili ku test kama ni drugs au siyo drugs fungua na ukate package moja na ulambe" Nikawaambia kipimo cha drug ni kulamba? Hata hivyo mimi ndiye mshukiwa kwa hiyo unaniambia nilambe kama ni drug unadhania nitakupa jibu gani? Lazima nitasema sio drug ili nipite. Kwanza huu ni unga unapaswa kuliwa ukiwa umepikwa nikilamba mbichi nitaumwa na tumbo. Ninasafiri mbali kama masaa 15 kwenye hii flight tafadhali fikirieni na nyie. Akadakia mwingine na kusema "anatubabaisha huyu chukua pass yake nenda ku-cancel flight yake".
Mara wakaitana wengine wawili wakawa wanne. Wakaongeza polisi wengine wawili wenye uniform na vyeo vya Inspector na wawili CID. Yule dada wa kwanza akawa ameshakuja na wembe akakata ile pakti moja wakaniambia lamba haraka au tuna cancel flight yako. Wote sasa wakawa kitu kimoja wakajaza watu. Embarrassment ya ukweli.
Polisi mmoja wa uniform mwenye cheo cha inpector alikuwa mstaarabu saana akawaambia kwa kuangalia tu huu ni unga wa ugali, akaja dada mwingine naye akawaambia mnampotezea abiria muda na kazi imesimama hapa chukua hii pakiti moja pitisha kwenye machine yenyewe mumuachie aende. Wale wa kwanza kabisa na polisi mmoja wa kike mwenye cheo cha inspector wakasema no lazima alambe. Nikachotewa size ya kijiko cha chai nikalambishwa wakafurahi na kuniruhusu niendelee. Ila walichukua pass yangu wakaenda kutoa copy. CCTV camera za airport ni shahidi yangu. Naomba uongozi uangalie muda huo 15:45 hrs kwenye departure siku ya tarehe 13/9/2013.
Maoni yangu ni kuwa ikiwezekana hao wafanyakazi wachukuliwe hatua kwa sababu utendaji kama huo wa kutokutumia akili na unatia hasara nchi na kuwafanya wale watendaji wazuri waonekane pia kama hawajui wanachofanya.