Pole sana kwa yaliyo kukuta mkuu,kwa kawaida kuna mashine ya kutest unga,kulazimishwa kuonjeshwa haikuwa njia sahihi.
Ilikuwa ni kiasi cha kuchota unga kidogo na kuuingiza kwenye mashine na majibu yangepatikana hapo hapo na ungeruhusiwa kuendelea na safari. Au pia kuna vifaa vya kutestia viko kama tester za umeme(au kwa lugha rahisi screw drivers)nikiasi cha kukichukua na kukichoma kwenye mzigo unaoshukiwa na majibu yangepatikana there and then.
Lakini pia kaka kuna wakati ambapo inamlazimu mtu kulazimishwa kuonja alichokibeba ila ni katika situation zifuatazo:
1. Huwezi ukatest maji kwenye mashine na kugundua kama ni acid au any other burning chemical, ili uweze kuyatest ni lazima yaonjwe, na wa kuyaonja ni abiria mwenyewe kwani maji hayo ni ya kwake. Kama itakuwa ni kitu tofauti na maji lazima abiria atagoma kuyaonja.(hii inakuwa pale afisa mkaguzi anapokuwa na mashaka na kimiminika hicho)
2. Kuna baadhi ya watu hubeba dawa zao za kienyeji kwa ajili ya safari, hivyo basi huwezi kuzitest zaidi ya kuwaambia wazionje kama kweli ni dawa na wanazitumia, kama sio dawa za kunywa basi wanashauriwa waziweke kwenye check in luggages.
3. Endapo afisa mkaguzi kawa na mashaka na mzigo wa abiria,baada ya kuutest na kugundua kuwa sio drugs, lakini akawa na mashaka kuwa inaweza kuwa ni sumu ya aina yoyote ile ambayo inaweza kuleta madhara wakati wa safari basi atamuhitaji mwenye mzigo aonje ili kuthibitisha kuwa sio sumu. Endapo itakuwa sumu basi hata muhusika hataweza kuonja.
NB:
MARA NYINGI MASUALA YA USALAMA HAYANA FORMULAR, ILI ABIRIA AWEZE KUSAFIRI LAZIMA AFISA MKAGUZI ARIDHIKE KUWA ALIYEMKAGUA NI SALAMA KABLA HAJAMRUHUSU KUENDELEA NA SAFARI. NI SUALA LA MTU KUJIRIDHISHA.