TUKUTUKU
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 11,765
- 4,033
Mimi ni muumini mkubwa wa utendaji wa CHADEMA,na hasa utendaji kazi aliouonyesha Dr Slaa.Naamini Chama hiki kinaweza kunifikisha kwenye ndoto yangu ya utumiaji wa rasilimali za nchi kwa faida ya nchi na kupambana na ufisadi.Nimeshindwa kuficha hisia zangu kwa ndugu na jamaa zangu wa karibu.Kuna swali moja huwa wananiuliza ambalo limenishinda kulijibu au huwa nalijibu, lakini si kwa ufasaha.
Swali lenyewe linahusu ratiba ya kampeni ya Dr slaa,wanauliza mbona anakwenda maeneo ambayo alishakwenda?kwa mfano alishakwenda Shinyanga na Mwanza ,lakini mbona bado anakwenda tena, wakati bado kuna maeneo mengine ambayo bado ajakwenda kama Tanga,Pwani,Lindi,Mtwara na Zanzibar.Alipokwenda Tabora mbona hakwenda Sikonge na Urambo?Nimejaribu kutembelea website ya CHADEMA ili niweze kujua ratiba za kampeni za Dr Slaa,lakini sijapata ufafanuzi kwa kuwa website ya CHADEMA,kwa sasa haipatikani.
Wana Jf mwenye maelezo ya kutosha naomba ufafanuzi!
Swali lenyewe linahusu ratiba ya kampeni ya Dr slaa,wanauliza mbona anakwenda maeneo ambayo alishakwenda?kwa mfano alishakwenda Shinyanga na Mwanza ,lakini mbona bado anakwenda tena, wakati bado kuna maeneo mengine ambayo bado ajakwenda kama Tanga,Pwani,Lindi,Mtwara na Zanzibar.Alipokwenda Tabora mbona hakwenda Sikonge na Urambo?Nimejaribu kutembelea website ya CHADEMA ili niweze kujua ratiba za kampeni za Dr Slaa,lakini sijapata ufafanuzi kwa kuwa website ya CHADEMA,kwa sasa haipatikani.
Wana Jf mwenye maelezo ya kutosha naomba ufafanuzi!