Utata katika maisha yangu

Utata katika maisha yangu

mjerumaniwapahi

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2014
Posts
378
Reaction score
270
Habari za jumapili wanajf wenzangu
Mimi ni kijana wa miaka 30, nilipata utata pale nilipomaliza elimu kwani bibi yangu mzaa mama aliniita kijijini
Nilipofika tu bibi aliniambia mjukuu wangu pole kwa mihangaiko yako ya miaka nenda rudi
Mihangaiko yangu ni mingi sana nilifiwa na mzazi wa kiume (baba) nikiwa na miaka 6 na nikafiwa na mama mzazi nilipofika darasa la 7 nikiwa na miaka 15 pia nikiwa mtoto wa pekee katika familia yangu hiyo na baada ya kifo cha wazazi nilisoma kwa mipango ya mungu mpaka nikamaliza masomo
Utata ulikuja pale bibi yangu mzaa mama aliponiambia mjukuu wangu nina siri ya maisha yako ..nikamuomba aniambie hiyo siri akadai niwemvumilivu na atakayo yasema
Bibi aliniambia baba yako aliyefariki siyo baba yako mzazi kwani mama yako aliolewa akiwa mjamzito na baba yako mzazi yupo hai na nitakusaidia kuonana nae ila ibaki siri yenu ndipo nikakubali na juhudi za kuonana zikafanyika na tukaonana na kiukweli mm na huyo mzee tunafana kila kitu kuanzia kimo ,sura, rangi mpaka sauti na tuliongea mengi japo mimi sikuhitaji chochote toka kwake ila tulikubaliana iwe siri tu maana tayar mimi nina ndugu zangu wa marehem baba mwinngine
Na tutabaki kama marafiki tu na huyu baba wa sasa ila tatzo siri hii haiwezi kudumu maana mama angu mdogo anaijua ,bibi na mimi tena... Nijuavyo mm siri ni ya mtu mmoja
Pia marehemu mama angu aliwahi kuniambia nikiwa mdogo kuwa mwanangu nitakuja kukwambia jambo lililojificha katika maisha yako ila alifariki kabla hajaniambia

Hivyo basi ndugu zanguni wanajf mwenzenu huwa naishi kwa utata mno endapo siri hii itajulikana kwa ndugu wa upande wa baba nini kitatokea hali yakuwa wahusika wakubwa walushatangulia mbele ya haki


Pia upande wa baba wa ukubwani wapo ambao walishadokezwa na siri hii na baba yao


Kama una ushari, maoni unaweza kuutoa
Nawatakieni jumapili njema
 
Usiwe na hofu. Huyo babako marehemu na ukoo wake wanajua kila kitu. Hawatashtuka sana siri ikivuja
 
Ushauri wangu ni kidogo tu na unaweza usikufurahishe pia.

Kwanza pole sana! Pili nisikuchoshe, wala usinichoshe; wewe umeshakuwa mtu mzima unayejitambua kutokana na umri ulionao. Kwa ufupi tu, kuendelea kutunza siri inayokufanya uishi kwa wasiwasi huenda wewe ni mnufaika wa hiyo siri kwa namna moja, au nyingine ama kama hunufaiki nayo sioni sababu ya wewe kuogofya na kuendelea kuishi kwa wasiwasi kwenye kivuli cha kuitunza siri ambayo wengine wanaweza kuitoboa. Ushauri vunja ukimya ili uwe huru ufuruhie maisha!
 
me nakushauri uwaue wote wanaofahamu hiyo siri then ubaki pekee yako unayeifahamu siri hiyo.
 
Habari za jumapili wanajf wenzangu
Mimi ni kijana wa miaka 30, nilipata utata pale nilipomaliza elimu kwani bibi yangu mzaa mama aliniita kijijini
Nilipofika tu bibi aliniambia mjukuu wangu pole kwa mihangaiko yako ya miaka nenda rudi
Mihangaiko yangu ni mingi sana nilifiwa na mzazi wa kiume (baba) nikiwa na miaka 6 na nikafiwa na mama mzazi nilipofika darasa la 7 nikiwa na miaka 15 pia nikiwa mtoto wa pekee katika familia yangu hiyo na baada ya kifo cha wazazi nilisoma kwa mipango ya mungu mpaka nikamaliza masomo
Utata ulikuja pale bibi yangu mzaa mama aliponiambia mjukuu wangu nina siri ya maisha yako ..nikamuomba aniambie hiyo siri akadai niwemvumilivu na atakayo yasema
Bibi aliniambia baba yako aliyefariki siyo baba yako mzazi kwani mama yako aliolewa akiwa mjamzito na baba yako mzazi yupo hai na nitakusaidia kuonana nae ila ibaki siri yenu ndipo nikakubali na juhudi za kuonana zikafanyika na tukaonana na kiukweli mm na huyo mzee tunafana kila kitu kuanzia kimo ,sura, rangi mpaka sauti na tuliongea mengi japo mimi sikuhitaji chochote toka kwake ila tulikubaliana iwe siri tu maana tayar mimi nina ndugu zangu wa marehem baba mwinngine
Na tutabaki kama marafiki tu na huyu baba wa sasa ila tatzo siri hii haiwezi kudumu maana mama angu mdogo anaijua ,bibi na mimi tena... Nijuavyo mm siri ni ya mtu mmoja
Pia marehemu mama angu aliwahi kuniambia nikiwa mdogo kuwa mwanangu nitakuja kukwambia jambo lililojificha katika maisha yako ila alifariki kabla hajaniambia

Hivyo basi ndugu zanguni wanajf mwenzenu huwa naishi kwa utata mno endapo siri hii itajulikana kwa ndugu wa upande wa baba nini kitatokea hali yakuwa wahusika wakubwa walushatangulia mbele ya haki


Pia upande wa baba wa ukubwani wapo ambao walishadokezwa na siri hii na baba yao


Kama una ushari, maoni unaweza kuutoa
Nawatakieni jumapili njema
Labda nikishauri kitu ...ndugu Yangu Endelea kutunza kumbukumbu yakuwa baba yako alishafariki ...!! Usiache mbachao kwa msala upitao ...!!
 
Umerithishwa chochote kutoka kwa baba mlezi? Kwa kweli kama umerithi mali yake ndugu zake wanaweza kukusumbua lakini inategemeana na sheria za kabila husika.
 
Huyo baba alikuwa wapi siku zotee??? Mpaka anakujaa leo???
 
Pole sana ndugu yangu, mkasa wako ni kama wangu Mzee wang (alale mahali pema) alimkana mama yangu tangu nikiwa tumboni. Mama yangu akaolewa na mwanaume mwingine (ndiyo namuita baba yangu japo natumia jina la baba aliyenikataa) akiwa na mimba hivyo hivyo.. tangu nizaliwe mpaka leo hii namaliza chuo yeye ndo amenisomesha nakunifikisha hapa bila kunibagua. Mpaka leo huwaga najisemea moyoni sinaga baba mwingine zaid ya huyu aliyenilea tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu.

Piga moyo konde songa mbele, hawakawii kuharibu maisha yako.
 
Kuna rafikia yangu alikuwa na baba wawili. Mmoja alifariki akamwachia uruthi. Huyu wa pili akaendelea nae hadi alipofariki. Alinambia yeye akiambiwa huyu baba yako hakatai anaenda nao sawa.
 
Matatizo yote huku duniani huanzia kwa mwanamke.
Kijana sikia huyo anaweza kuwa your biological father but is not your daddy.
Nashauri baki na familia yako kama kawaida na hata wakigundua hawa wewe huna hatia maana hukuhusika kabisaa .
Wanawake mungu anawaona.
 
Mkuu pole sana,we ni mtu mzima na unakaribia kuwa na mji wako pambana na maisha yako uwe na familia yako;hawa watu wa kufahamiana ukubwani hawatakuwa na tija nawe zaidi ya kuongeza matatizo tu...tafuta mwanamke mstaarabu mjenge maisha yenu na yawe na furaha;kuhusu mambo ya siri sijui ni baba au si baba waachie hao ndugu zako ndio wabebe huo msalaba kwako haikuhusu.Kama kwa sasa utamkubali ni baba yako awe ana investment inayoeleweka na awe tayari kukupatia.
 
Sioni sababu yakuendelea kuiweka siri tena.

Kwasababu usiri ulikuwepo kulinda Heshima na Kukulinda wewe. ..sasa Muhusika mkuu (Marehemu Mama) hatunaye tena. ...kwanini iendelee kuwa siri?

Ningekushauri myaongee kama ni misamaha iombwe usamehe kwa niaba ya wazazi wako maisha yaendelee. ...

Ni chaguo lako kumleta biological father wako kwenye maisha yako....

Haitakuwa vizuri uanze familia yako bado unashikilia siri hii.....

Bailogical father wako kama hakuwepo kwenye maisha yako mpe nafasi awe kwenye maisha ya watoto wako iwapo tu ni kwa manufaaa ya Watoto (wajukuu).
 
Back
Top Bottom